+ All Categories
Home > Documents > Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini...

Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini...

Date post: 30-Mar-2019
Category:
Upload: hoangnga
View: 326 times
Download: 0 times
Share this document with a friend
64
Transcript
Page 1: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala
Page 2: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au

Nyota Iliyofifia?

Hakimiliki 2017 Evarist Chahali

Kimechapishwa na Evarist Chahali kupitia Smashwords

Smashwords Edition License Notes

This ebook is licensed for your personal enjoyment only. This ebook may not be re-sold or

given away to other people. If you would like to share this book with another person, please

purchase an additional copy for each recipient. If you’re reading this book and did not purchase

it, or it was not purchased for your enjoyment only, then please return to Smashwords.com or

your favorite retailer and purchase your own copy. Thank you for respecting the hard work of

this author.

Page 3: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Farahasi

Kumbukumbu

Shukrani

Kuhusu Mwandishi

Utangulizi

Sura Ya Kwanza

Sura Ya Pili

Sura Ya Tatu

Sura Ya Nne

Sura Ya Tano

Sura Ya Sita

Hitimisho

Vitabu Vingine

Ungana Na Mwandishi Mtandaoni

Page 4: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kumbukumbu

Kwa Marehemu Mzee Philemon Chahali na marehemu Adelina, wazazi wangu mliotangulia

mbele ya haki wakati ninawahitaji sana. Asanteni kwa kunizaa, kunilea, na kunipa imani ya

kuwa mtu ninayetaka kuwa.

Page 5: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Shukrani

Kitabu hiki kinachofanya tathmini ya kina ya miaka miwili ya utawala wa Rais Dokta John

Magufuli ni mwendelezo wa uchambuzi wa siasa za Tanzania kwa mfumo wa vitabu. Kitabu cha

kwanza ‘Uchaguzi Mkuu Tanzania 2015: Magufuli vs Lowassa,’ kilichotoka Oktoba 2015

kilijadili kwa kina kuhusu uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani nchini Tanzania,

uliofanyika mwezi huo. Kitabu cha pili, ‘Dokta John Magufuli: Safari ya Urais, Mafanikio na

Changamoto Katika Urais Wake,’ kilijadili kipindi cha awali cha utawala wa Dokta Magufuli.

Kilichonisukuma kuandikia kitabu hicho cha pili ni pamoja na ukweli kwamba kile cha kwanza

kilichapishwa takriban wiki mbili tu kabla ya Uchaguzi Mkuu na hivyo kuwanyima fursa

wasomaji wengi watarajiwa. Vilevile, kulionekana kuna haja ya kufanya tathmini ya uchaguzi

huo ulioshuhudia mgombea wa chama tawala, Dokta Magufuli akiibuka mshindi.

Kadhalika, mimi ni mwanafunzi wa stadi za siasa, na mara zote nimekuwa nikiamini kwamba

njia mwafaka zaidi ya kuitumia elimu yangu ipasavyo ni kuitumikia nchi yangu kwa njia ya

maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala gazetini au bloguni au kwa makala za

sauti ninazozitoa mara kwa mara. Ninasema ‘maongezi’ kwa vile mimi si mwandishi kitaaluma,

na ninajitambulisha kama mfanya-maongezi (conversationalist) kuliko mwandishi. Kwahiyo,

kitabu hiki ni sehemu na mwendelezo wa maongezi hayo.

Licha ya kuwa mwanafunzi wa stadi za siasa, kitabu hiki, kama zilivyo makala zangu gazetini na

bloguni, sio cha kitaaluma. Ni maongezi kati yangu na Mtanzania wa kawaida, awe mwenye

shahada ya uzamifu kutoka chuo kikuu au mhitimu wa elimu ya msingi. Hii isitafsiriwe kama

kukosa imani katika kujadili masuala mbalimbali kitaaluma bali nimeonelea kuwa ndio njia

mwafaka ya kuongea na watu wengi pasi kuwepo kwa vikwazo vinavyoweza kuwanyima fursa

wenzetu ambao hawakubahatika kielimu. Kitabu hili ni kwa ajili ya kila Mtanzania wa rika

lolote, jinsia yoyote na wa kada yoyote – mwanasiasa au raia anayeichukia siasa, ‘mama ntilie’

au mwanasheria, mwanafunzi au mwalimu, nk.

Kama ilivyokuwa kwa toleo la kwanza, ninatunuku (dedicate) kitabu hiki kwa baba yangu

mpendwa, Marehemu Mzee Philemon Chahali, ambaye pamoja na mkewe, mama yangu

mpendwa, marehemu Adelina Mapango, ambao japo hawapo nasi kimwili, ninaamini kiroho

wanafurahishwa na kazi hii yangu mtoto wao.

Ninamshukuru dada yangu Mary, na wadogo zangu, Sr Maria-Solana na mapacha Peter na Paul

(Kulwa na Doto) kwa upendo wao ulionisaidia mno kuandika kitabu hiki.

Pia, ninawashukuru watu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii, hususan Twitter na

Facebook, kwa kulipokea vema wazo langu la uandishi wa vitabu.

Mapungufu yoyote yaliyomo katika kitabu hiki ni yangu mwenyewe na ninabeba lawama zote.

Kama nilivyotanabaisha hapo juu, mimi si mwandishi kitaaluma. Na pia ninakichukulia kitabu

hiki kama maongezi (conversation) niliyoamua kuyaweka katika maandishi.

Ni matumaini yangu makubwa kuwa licha ya faida tarajiwa ya mjadala wa undani kuhusu

uchaguzi huo mkuu, kitabu hiki kitawahamasisha Watanzania wenzangu kuhusu haja ya kuweka

fikra au mitizamo yetu katika maandishi, sambamba na kuendeleza filosofia isiyo rasmi ya

‘sharing is caring.’

Page 6: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Ninawatakia usomaji mwema.

Evarist Chahali.

Glasgow, Uskochi.

Desemba 9, 2017.

Page 7: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kuhusu Mwandishi

Mwandishi wa kitabu hiki, Evarist Chahali, ni Mtanzania mwenye makazi yake jijini Glasgow,

Uskochi. Ni mhitimu wa Shahada ya kwanza katika Sosholojia (BA in Sociology) aliyoipata

katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania, Shahada ya Uzamili katika Stadi za Vita

(Master of Letters in War Studies) na Shahada ya Uzamili katika Utafiti wa Siasa (Master of

Research in Political Research) alizopata katika Chuo Kikuu cha Aberdeen, Uskochi, ambapo

bado anaendelea na Shahada ya Uzamifu katika Stadi za Siasa (PhD in Political Studies – Part-

Time).

Kwa zaidi ya miaka 10, amekuwa akiandika makala katika magazeti mbalimbali nchini

Tanzania, ambapo huko nyuma aliandikia magazeti ya ‘Kulikoni’ na ‘Mtanzania,’ na kwa sasa ni

mwandishi wa makala katika gazeti la kila wiki linaloongoza nchini Tanzania, la ‘Raia Mwema.

Kadhalika, mwandishi anamiliki blogu ya ‘Kulikoni Ughaibuni’ iliyoanzishwa mwaka 2006.

Awali, mwandishi alikuwa mwalimu katika Shule ya Sekondari ya Ecknforde, Tanga, Tanzania

kabla ya kujiunga na utumishi serikalini katika Ofisi ya Rais wa Jamhuri wa Munngano wa

Tanzania. Hivi sasa, licha ya kuendelea na masomo yake ya Shahada ya Uzamifu (part-time)

anajihusisha ushauri wa kitaalamu katika masuala ya intelijensia na usalama (intelligence and

security consulting), mikakati ya siasa (political strategy consulting) na mahusiano na

mawasiliano ya kimkakati (International PR and strategic communications), akiwa mwanzilishi

na mmiliki wa kampuni ya ushauri wa kitaalam ya AdelPhil Consultancy iliyopo Glasgow,

Uskochi.

Page 8: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Utangulizi

Oktoba 5 mwaka juzi – 2015 – Dokta John Magufuli aliapishwa kuwa Rais wa tano wa Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania. Kabla yake nchi hiyo iliongozwa na Marehemu Julius Nyerere, Ali

Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete.

Kitabu hiki ni mwendelezo wa vitabu vingine viwili vinavyozungumzia siasa za Tanzania

hasa kuhusu uchaguzi na uongozi. Kitabu cha kwanza kilizungumzia uchaguzi mkuu wa mwaka

2015 kabla hakujafanyika, tathmini ya fursa kwa kila mgombea na chama chake.

Kitabu cha pili kilihusu safari ya Dokta Magufuli kutoka kwenye mchakato wa kupitishwa

kuwa mgombea wa chama chake hadi kushinda uchaguzi huo. Kadhalika, kilichambua

mafanikio na changamoto kwa urais wake.

Kitabu hiki kinaendelea vilipoishia vitabu hivyo viwili, kwa kufanya tathmini ya kina ya

miaka miwli tangu Dokta Magufuli aingie madarakani.

Page 9: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Kwanza

Tarehe 25 Oktoba mwaka 2015, Watanzania walipiga kura ya kumchagua Rais mpya Dokta John

Magufuli aliyemrithi mtangulizi wake, Rais wa Nne wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete. Japo

uchaguzi mkuu haukuwa wa kwanza katika historia ya nchi yetu, mazingira yaliyouzunguka na

hali halisi ya Tanzania wakati unafanyika, yaliufanya uwe na umuhimu wa kipekee.

Kisiasa, angalau kwa chama tawala, CCM, yayumkinika kuhitimisha kuwa uchaguzi mkuu

huo ulikuwa wa kwanza kufanyika ambapo ‘nguvu za Baba wa Taifa, Marehemu Mwalimu

Julius Nyerere, hazikuwepo moja kwa moja (directly).’ Mara baada ya kung’atua, Nyerere

‘alimteua’ Ali Hassan Mwinyi kuwa Rais, akitumia nafasi yake kama mwanasiasa mwenye

nguvu zaidi nchini Tanzania. Baada ya Rais Mwinyi kumaliza mihula yake mawili mwaka 1995,

Nyerere alitumia tena nguvu zake kisiasa na kuwezesha msaidizi wake wa zamani, Benjamin

Mkapa kupitishwa na CCM, na hatimaye kushinda urais, madaraka aliyoshikilia kwa mihula

mawili, kama mtangulizi wake, yaani Rais Mwinyi.

Hata hivyo, duru za kisiasa zinaelezwa kuwa nguvu ya kisiasa aliyotumia Nyerere

kumpitisha Mkapa iliwaathiri wanasiasa wawili vijana, Jakaya Kikwete na Edward Lowassa,

ambao miaka 10 baadaye, walifanikiwa kmwingiza mmoja wao Ikulu.

Kwahiyo japo Nyerere hakuwa hai wakati Kikwete anaingia madarakani mwaka 2005, safari

yake ya kuingiza Ikulu ilicheleweshwa kwa miaka 10 na nguvu za kisiasa za Nyerere. Kadhalika,

kushinda urais kwa Kikwete akisaidiwa na rafiki yake Lowassa mwaka huo kulitazamwa kama

‘manufaa’ ya kutokuwepo Nyerere.

Mwaka 2010, Kikwete alishinda tena urais, kama ilivyo kanuni isiyo rasmi ndani ya chama

tawala CCM kwa rais aliye madarakani ‘kuruhusiwa’ kumaliza mihula miwili. Kwahiyo, hata

kama ‘nguvu za Nyerere’ zilikuwepo wakati huo bado zisingemzuwia Kikwete kushinda tena.

Katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu huu hali ilikuwa

tofauti kabisa. ‘Nguvu za Nyerere’ zilionekana bayana kuondoka kabisa. Hata wanasiasa

waliokuwa waamini wa itikadi zake, kwa mfano mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru, sio tu

walionekana wenye mtizamo tofauti lakini baadhi yao, ikiwa ni pamoja na Kingunge

mwenyewe, waliohama CCM na kujiunga na upinzani. Jina la Nyerere limebaki kama heshima

tu lakini lisilo na uwezo wa kubadili chochote ndani ya CCM.

Lakini, tukiacha kumhusisha Nyerere, kinyang’anyiro cha kumpata mgombea wa CCM

wake ambapo hatimaye Dkt Magufuli ‘aliibuka kidedea’ kiliweka historia mpya, ambapo

makada zaidi ya 40 walijitokeza kuwania kuteuliwa. Kuna waliotafsiri iwngi huo ya idadi ya

‘watangaza nia’ kama kukua kwa demokrasia ndani ya chama hicho, huku wengine wakieleza

kuwa wingi huo ni ishara ya uchu wa madaraka, na wengine wakienda mbali zaidi na kudai

kuwa Rais Kikwete aliishusha hadhi ya urais kiasi kwamba ‘kila Dick, Tom na Harry’ alidhani

anaweza kuwa Rais.

Kwa mara ya kwanza, CCM na Watanzania walishuhudia kampeni zisizo rasmi za makada

waliotangaza nia za kuomba kupitishwa na chama hicho hata kabla kutangazwa rasmi kuanza

kwa mchakato huo. Kampeni hizo zilikuwa kali, kana kwamba ni kampeni rasmi za kuwania

urais. Awali, kuna waliohoji iwapo ukali wa mchuano huo ungepelekea chama hicho kupata

Page 10: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

mgombea bora au la, lakini hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Dkt Magufuli tangu aanze

rasmi urais wake zinaweza kutoa jibu kuwa wingi wa waliojitokeza kuwania nafasi hiyo

umeisaidia sana CCM kumpata mgombea, na hatimaye rais, bora.

Jingine kisiasa, ni athari za mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake,

ambapo jina la Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa halikupitishwa, na hatimaye akaamua

kuhama chama hicho na kujiunga na chama cha upinzani, Chadema. Kuhama kwa Lowassa

kutabaki kuwa moja ya kumbukumbu muhimu za uchaguzi huo. Japo kinyume na ilivyotarajiwa

kuwa kuhama kwake kungeambatana na kuhama kwa wanasiasa wengi wa CCM waliokuwa

wanamuunga mkono, ukweli tu kuwa mwanasiasa huyo ambaye kura mbalimbali za maoni

zilimwonyesha akiongoza kwenye uwezekano wa kupitishwa kuwa mgombea wa chama hicho,

kuamua kujiondoa katika chama tawala kulikuwa si jambo dogo hata chembe.

Na baadaye, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye naye alitangaza kujiunga na

Upinzani, na kuweka historia mpya ya mawaziri wakuu wa zamani kuhama CCM na kujiunga na

Upinzani. Baadaye kidogo, mwanasiasa mkongwe na mwasisi wa CCM, Kingunge Ngombale

Mwiru, nae alitangaza kukihama chama hicho tawala, na japo hakujiunga na chama kingine cha

siasa, alipanda majukwaani kumnadi Lowassa.

Uamuzi wa Lowassa kuhamia Chadema, ambayo awali ilifikia maafikiano ya kusimamisha

mgombea mmoja wa urais na vyama vya CUF, NCCR Mageuzi na NLD ambavyo kwa pamoja

viliunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), na kuteuliwa kuwa mgombea urais kwa

tiketi ya UKAWA kulibadili kabisa mwelekeo wa uchaguzi mkuu huo. Yayumkinika

kuhitimisha kuwa kwa mara ya kwanza kabisa, vyama vya upinzani, hususan vilivyounda

UKAWA, na wanachama wake, walionekana kuwa na matumaini makubwa ya kuing’oa CCM

madarakani. Hata hivyo, kuwa na matumaini ni suala moja, na matumaini hayo kutimia ni jambo

jingine kabisa kama ilivyoshuhudiwa katika matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo ambapo

Lowassa alishindwa na Dkt Magufuli.

Lakini eneo jingine lilioufanya uchaguzi mkuu huu kuwa tofauti na chaguzi zilizotangulia ni

matumizi ya teknolojia ya kisasa, hususan mitandao ya kijamii. Kama ilivyokuwa wakati CCM

inafanya mchakato wa kupata mgombea wake wa tiketi ya urais, ambapo watangaza nia

mbalimbali walijiunga na mitandao ya kijamii na baadhi yao kufanya ‘kampeni’ za waziwazi,

kampeni za vyama mbalimbali vya siasa, hususan CCM na UKAWA zilitawala mno katika

mitandao mbalimbali ya kijamii, hususan Twitter, Facebook, Instagram na kwenye blogu.

Kadhalika, teknolojia ya mawasiliano ya kutumiana ujumbe, hususan Whatsapp, ilikuwa nyenzo

kubwa ya ushirikishwaji wa umma katika siasa zinazohusiana na uchaguzi huo. Yayumkinika

kuhitimisha kuwa huo ulikuwa uchaguzi mkuu wa kwanza ambapo teknolojia ya kisasa ilikuwa

na nafasi kubwa, kulinganisha na chaguzi zilizotangulia.

Matumizi ya teknolojia hayakuishia kwenye kampeni tu bali pia hata shughuli nyingine

zilizohusiana na uchaguzi huo na siasa za Tanzania kwa ujumla. Kwa mfano, wakati fulani

niliweza kushiriki moja kwa moja (kwa njia ya Skype) katika mjadala kuhusu hatma ya nchi

uliofanyika jijini Dar es Salaam, wakati mimi nipo Glasgow, hapa Uingereza. Japo kwa mujibu

wa Katiba ya Tanzania, raia wa nchi hiyo walio nje hawaruhusiwi kupiga kura, ukweli kwamba

baadhi yao walishiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali ya mustakabali wa taifa iliwezesha

ushiriki wao katika shughuli za kisiasa (political participation).

Lakini tukiweka kando mazingira hayo ya kisiasa na kiteknolojia, uchaguzi mkuu huu

ulikuwa na umuhimu mkubwa kwa kila Mtanzania, hasa kwa kuzingatia hali halisi iliyokuwepo

wakati unafanyika. Pamoja na taarifa mbalimbali zilizoashiria kuwa Tanzania ilikuwa ikifanya

Page 11: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

vizuri kiuchumi, mamilioni ya Watanzania bado ni masikini mno. Na kana kwamba hiyo

haitoshi, pengo kati ya ‘wenye nacho’ na ‘wasio nacho’ linazidi kuongezeka.

Kibaya zaidi, kadri pengo hilo linavyozidi kukua ndivyo hisia miongoni mwa ‘wasio nacho’

kuwa wengi wa ‘wenye nacho’ ni mafisadi. Kwa lugha nyingine, kwa kiasi kikubwa, utajiri

nchini Tanzania umekuwa ukiangaliwa kwa jicho la mashaka. Hisia hizi zinaathiri umuhimu wa

watu kujituma na pengine kuweza kuingiza kwenye kundi la ‘wenye nacho.’

Wakati hakujawahi kutolewa maelezo ya kueleweka kwanini Tanzania ni masikini licha ya

utajiri mkubwa wa raslimali ilionao, yayumkinika kuhitimisha kuwa ufisadi ni moja ya sababu

ambazo sio tu zinachangia umasikini wa nchi wa nchi yetu bali pia unazidisha hali hiyo.

Kwahiyo moja ya changamoto kwa serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana kwa dhati na

ufisadi.

Suala la kukosekana maelezo kuhusu umasikini unaoikabili nchi yetu lipo pia katika hisia

kuhusu mafanikio ya watu binafsi. Kama kuna wahanga wakubwa wa hisia hizo basi ni wasanii,

ambapo msanii akifanikiwa katika kazi zake, zinasikika tetesi kuwa ni muumini wa kundi la

‘Freemason.’ Kama ilivyo kwa wengi wa wanasiasa wetu kutanabaisha bayana kwanini nchi

yetu ni masikini ndivyo ambavyo baadhi ya wananchi wanashindwa kuelewa kwamba

inawezekana kwa mtu kuwa na mafanikio pasipo kujihusisha na ufisadi au kuwa ‘Freemason.’

Lakini licha ya umasikini mkubwa uliowakabili Watanzania wengi, ambao kwa mtizamo

wangu ninaamini ulichangiwa zaidi na ufisadi, nchi pia ilikabiliwa na matatizo mengine lukuki,

ikiwa ni pamoja na tatizo sugu la nishati isiyo na uhakika kutokana na mgao ‘wa kudumu’ wa

umeme. Matatizo mengine ni pamoja na ukosefu wa ajira, ambapo idadi kubwa ya wahitihimu

hukumbana na soko la ajira lisilowahitaji, matatizo kwenye sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na

miundombinu duni ya elimu na walimu kucheleweshewa mishahara yao. Kadhalika, maeneo

mengi ya Tanzania bado yalikabiliwa na tatizo la huduma ya uhakika ya maji, huku sekta ya afya

nayo ikiwa na matatizo mengi.

Uhalifu pia ulishamiri huku biashara ya madawa ya kulevya ikiimarika mno kiasi cha

kudhani mihadarati ni miongoni mwa ‘exports’ muhimu kwa nchi yetu. Vita dhidi ya madawa ya

kulevya ilikwazwa sio tu na viongozi wa serikali na wanasiasa kwa kutochukua hatua dhidi ya

wahusika bali pia mtizamo wa jamii kwa wahusika ni wa kuwatukuza zaidi (kwa mfano

‘kuwapamba’ kwa jina la ‘wazungu wa unga’ badala ya kuwaona kuwa ni wahalifu).

Sambamba na tatizo la madawa ya kulevya ni ujangili ambao ulichangia sana kuchafua

taswira ya nchi yetu kimataifa. Mabadiliko ya mara kwa mara ya mawaziri wanaoongoza Wizara

na idara zenye dhamana ya maliasili yalishindwa kabisa japo kupunguza tatizo hilo.

Tatizo jingine linalohusiana na uhalifu ni biashara ya ‘kuchukiza’ inayohusisha viungo vya

watu wenye ulemavu wa ualbino. Kama kuna kitu ambacho kiliichafua mno Tanzania ni biashara

hiyo ambapo vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa vilifanya vipindi maalumu kuelezea

kuhusu tatizo hilo. Tatizo hilo lilichangiwa zaidi na ukweli kuwa imani za ushirikina zimeota

mizizi mno katika nchi yetu, na hakuna jitihada za dhati kukabiliana nalo.

Kuna baadhi ya wananchi walikuwa wanaongea kwa mzaha kuwa ‘shughuli pekee

inayolipa, yaani yenye faida, katika nchi yetu ni uhalifu.’ Licha ya biashara ya madawa ya

kulevya na ujangili, nchi yetu pia ilikabiliwa na matatizo ya utakasishaji fedha sambamba na

biashara ya kusafirisha binadamu isivyo halali (human trafficking).

Kwa upande wa umoja wa kitaifa, kusuasua katika kuyashughulikia matatizo yanayoikabili

muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar kuliendelea kuweka muungano huo katika hali ya

hatihati. Na kama ilivyogusiwa katika toleo la kwanza la kitabu hiki, kwamba uchaguzi huo

unngeweza kuwa kama ‘referendum’ ya Muungano, kwa sababu wakati CCM ilibainisha katika

Page 12: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

ilani yake ya uchaguzi kuwa ingeendelea kudumisha muundo uliopo wa serikali mbili, UKAWA

waliweka wazi kwamba miongoni mwa vipaumbele vyao ni muundo wa serikali tatu kama

ulivyopendekezwa na Tume ya kupokea maoni kuhusu Katiba Mpya, maarufu kama ‘Tume ya

Warioba.’ Katika kitabu hicho nilitoa angalizo kuwa hatma ya muundo wa muungano uliopo

ingetegemea chama gani kingechoshinda kati ya CCM na UKAWA, hususan huko Zanzibar.

Kwa bahati mbaya, na kimsingi, kutokana na kasoro za Muungano kutoshughulikiwa kwa

ukamilifu, hadi wakati ninaandika kitabu hiki, hatma ya uchaguzi mkuu huko Visiwani ni tete

kufuatia uamuzi wa Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar kufuta uchaguzi wa Rais wa Zanzibar. Hadi

wakati ninaandika kitabu hiki, bado mgogoro wa kisiasa Visiwani humo unaendelea pasipo dalili

za kupatikana ufumbuzi mapema. Hata hivyo, licha ya kutoa taswira isiyopendeza kuhusu

uchaguzi mkuu kwa Jamhuri nzima, mgogoro huo wa kisiasa huko Zanzibar haukuathiri Dkt

Magufuli kutangazwa mshindi wa urais wa Muungano.

Lakini moja ya vichocheo vya kuporomoka kwa umoja wa kitaifa ilikuwa kupungua kwa

kasi kwa uzalendo. Ni wazi kwamba ni vigumu kwa uzalendo kushamiri kwenye jamii yenye

pengo linalozidi kukua kati ya ‘wenye nacho’ na ‘wasio nacho.’ Kwa bahati mbaya au makusudi,

programu za miaka ya nyuma zilizochangia kukuza uzalendo kama vile wahitimu kujiunga na

Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa sheria zilikuwa za kusuasua.

Umoja wa kitaifa ulihatarishwa pia na tatizo lililozidi kukua pasipo kushughulikiwa

ipasavyo la migogoro ya kidini. Kubwa zaidi katika tatizo hilo ni malalamiko ya muda mrefu ya

Waislam kuwa wenzao Wakristo wanapendelewa na serikali. Japo katika siku za hivi karibuni

tatizo hili limekuwa kimya, ukweli mchungu ni kwamba bado lipo na kuna uwezekano wa

kuibuka tena huko mbeleni. Wakati Awamu zilizotangulia ziliamua kulikwepa tatizo hilo kwa

kutolizungumzia waziwazi, ilani ya uchaguzi ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005

ilibainisha wazi dhamira yake ya kushughulikia kero za Waislamu, na kuahidi kuwa ingewapatia

Mahakama za Kadhi. Hata hivyo, ahadi hiyo imeendelea kuwa ahadi tu na haijatekelezwa hadi

muda huu. Ni wazi kwamba suala hili litajitokeza tena huko mbeleni.

Kushamiri kwa udini pia kulichangia kuathiri umoja wa kitaifa. Udini hujitokeza katika sura

tofauti, na mfano mmojawapo ni hiyo ahadi ya CCM mwaka 2005 kuwa ingewapatia Waislamu

mahakama za kadhi, lengo likiwa ni kuvuta kura za waamini wa dini hiyo. Uchaguzi Mkuu

uliopita, mwaka 2010, ulishuhudia udini ukitumika tena kama turufu ya kisiasa, ambapo

wanasiasa mbalimbali wa CCM waliojaribu kujenga picha kuwa mgombea urais kwa tiketi ya

Chadema, Dokta Willbrord Slaa ni ‘padri anayewakilisha Kanisa, na hafai kuwa rais.’ Mbinu

chafu kama hiyo iliwahi kutumika kwenye chaguzi za nyuma dhidi ya chama cha CUF ambapo

zilifanyika jitihada za kujenga picha kuwa chama hicho ni cha kidini, cha Kiislamu.

Tofauti za kiitikadi ziliendelea kuchangia mpasuko katika nchi yetu ambapo baadhi ya

viongozi wa ngazi za juu wa chama tawala walikuwa wakifanya jitihada za waziwazi kujenga

taswira potofu kuwa vyama vya upinzani ni kama taasisi za kihaini. Tulishuhudia huko nyumba

jinsi baadhi ya viongozi na wanachama wa Chadema walivyonyanyaswa na vyombo vya dola

kwa tuhuma za ugaidi. Kumekuwa na jitihada kubwa za kuwaaminisha Watanzania kuwa

Wapinzani si Watanzania kamili na hawaitakii mema nchi yetu.

Kingine kinachoweza kuingizwa katika kipengele hiki cha mmomonyoko wa umoja wetu

wa kitaifa ni mtizamo fyongo miongoni mwa wanasiasa na wananchi wa kawaida dhidi ya

Watanzania wenzao walio nje ya nchi kwa sababu moja au nyingine. Kama kuna kipindi hali hii

ilijiweka bayana zaidi basi ni wakati wa mjadala kwenye Bunge Maalum la Katiba ambapo suala

la uraia pacha liliigawa jamii, huku wengi wakiwaangalia Watanzania waliopo nje kama wenye

mapungufu katika sifa za utaifa, au kwa lugha nyepesi ‘Watanzania nusu,’ kwa maana kuwa sio

Page 13: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kamili. Mchango wa Watanzania walio nje, au Diaspora kama inavyohamika, umekuwa

ukipuuzwa kwa hoja mbalimbali, kubwa ikiwa ni tishio kwa usalama wa taifa letu, kana kwamba

matishio yaliyopo yamechangiwa na watu wa Diaspora.

Rekodi ya Tanzania katika kuheshimu haki za binadamu ilikuwa sio ya kupendeza hata

kidogo. Vyombo vya dola, hususan Jeshi letu la Polisi, vilikuwa mstari wa mbele katika

kutoheshimu haki za binadamu. Licha ya suala hili kuchangia katika kumomonyoa umoja wetu

kitaifa ambapo mara nyingi wahanga wakubwa walikuwa viongozi na wanachama wa vyama vya

upinzani, pia liliathiri sana imani ya Watanzania wengi kwa vyombo vyao vya dola.

Yayumkinika kuamini kuwa laiti nguvu iliyotumiwa na Jeshi la Polisi katika kudhibiti

maandamano halali ya vyama vya upinzani, kwa mfano, ingeelekezwa katika kukabili uhalifu,

basi tatizo hilo lingepungua kwa kiasi kikubwa.

Kimataifa, Tanzania ya zama za Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na hii ya miaka ya hivi

karibuni ilikuwa ni vitu viwili tofauti. Wakati nchi yetu sio tu ilikuwa miongoni mwa

wapiganiaji wa umoja na ushirikiano katika Bara la Afrika lakini pia ilishiriki katika mapambano

ya ukombozi kusini mwa bara hilo, kwa sasa ni vigumu kuielewa sera ya nje ya Tanzania, kama

ipo. Japo bado tuliendelea kuwa na mchango katika utatuzi wa migogoro kwa nchi jirani, kwa

mfano huko Burundi, sambamba na kuchangia harakati za kimataifa katika utatuzi wa migogoro,

kwa mfano uwepo wa majeshi yetu nchini D.R.C, hatukuweza kurudi kwenye ramani ya

kimataifa kama ilivyokuwa zama za Nyerere, na tatizo kubwa limekuwa kutokuwa na msimamo

imara.

Uwepo wetu katika eneo la Maziwa Makuu na hali ya mashaka inayotawala katika eneo hilo

inatupasa kutukumbusha umuhimu wa kujiimarisha kiulinzi na kiusalama, sambamba na

kudumisha amani yetu kwa kuzingatia kuwa ‘hatuna pa kukimbilia.’ Kulikuwa na shutuma

nyingi dhidi ya taasisi muhimu kwa usalama wa taifa letu, yaani Idara ya Usalama wa Taifa.

Kisiasa, taasisi hiyo ilikuwa ikituhumiwa kutekeleza majukumu yake kana kwamba ni kitengo

cha usalama cha chama tawala. Lakini shutuma kubwa kwa Idara hiyo ni jinsi ilivyoonekana

kushindwa kukabiliana na matishio kadhaa ya usalama kama vile ufisadi. Uimara wa taasisi

hiyo ni muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu kwa sababu uimara wa ndani ndio

unaowezesha kukabiliana vizuri na matishio kutoka nje ya nchi.

Moja ya changamoto zilizotarajiwa kumkabili mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi huo

ni kuyumba kwa thamani ya sarafu yetu. Kwa kuzingatia kuwa uchumi wetu unategemea sana

misaada ya nchi kama China, ambayo wakati Tanzania inaingia kwenye kipindi cha uchaguzi,

ilikuwa kwenye matatizo ya kiuchumi baada ya soko lake la hisa kuyumba, ilimaanisha haja ya

mikakati imara ya kuinusuru sarafu yetu. Hata hivyo, wakati wa kampeni za uchaguzi, suala la

kuyumba kwa thamani ya shilingi halikupewa uzito stahili.

Ni vigumu kuorodhesha matatizo yote yaliyokuwepo wakati Tanzania inaingia kwenye

uchaguzi huo (yanahitaji kitabu kizima) lakini kilicho wazi ni kwamba uchaguzi huo ulikuwa

fursa muhimu kwa Watanzania kumchagua kiongozi atakayewasaidia kuboresha mazingira ya

safari ya kuifikisha nchi yetu mahala inapostahili kuwa.

Kitabu hiki kina sura sita. Sura ya kwanza inamtambulisha kwa kifupi Dokta John Magufuli,

alipotoka na hadi alipofikia hatua ya kuchukua fomu kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania na hatimaye kushinda.

Sura fupi ya pili inazungumzia mchakato wa CCM kumpata mgombea wake wa kiti cha

urais, na jinsi Dokta Magufuli alivyofanikiwa kuibuka mshindi katika kinyang’anyiro hicho

ambacho kilishuhudia makada 43 wa chama hicho wakichukua fomu kuwania nafasi hiyo.

Page 14: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura ya tatu inazungumzia fursa mbalimbali ambazo ziliitengenezea CCM na mgombea

wake Dokta Magufuli mazingira mazuri ya ushindi ktika uchaguzi huo.

Sura ya nne inazungumzia vikwazo mbalimbali kwa CCM na Dokta Magufuli katika

kinyang’anyiro cha urais ambapo kwa mara ya kwanza tangu Tanzania iingie katika mfumo wa

vyama vingi, chama hicho tawala kilikuwa kikikabiliana na muungano wa vyama vinne vya

upinzani, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, huku mgombea wao akiwa mwanasiasa

ambaye kabla ya kuhama CCM alikuwa mwanasiasa maarufu kuliko wote, yaani Lowassa.

Sura ya tano inazungumzia urais wa Dokta Magufuli tangu atangazwe mshindi, hadi muda

huu kitabu hiki kinaandikwa, na jinsi alivyobadilisha kwa kiasi kikubwa, pamoja na mambo

mengine, taswira ya Tanzania ndani na nje ya nchi.

Sura ya sita inajadili changamoto mbalimbali zinazomkabili Dokta Magufuli, ikiwa ni

pamoja na haja ya jamii kubadilika ili kuendana na falsafa ya ‘Hapa ni Kazi Tu,’ sambamba na

mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar. Sura hiyo pia inagusia umuhimu wa mabadiliko katika

sekta ya usalama wa taifa hasa ikizingatiwa kuwa vita aliyotangaza Dokta Magufuli dhidi ya

mafisadi, wauza madawa ya kulevya, majangili, nk inagusa watu wenye nguvu kubwa na ambao

wanaweza kuhatarisha usalama wake binafsi na pengine taifa kwa ujumla.

Sura ya fupi ya mwisho ni ya kuhitimisha kitabu hiki, na kwa kiasi kikubwa inafanya

majumuisho ya masuala mbalimbali yaliyojadiliwa katika sura zilizotangulia.

Page 15: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Pili

Dokta Magufuli na mchakato wa CCM kumpata mgombea wake wa kiti cha urais: Sura hii

inajadili kwa undani mchakato wa chama tawala CCM kumpata mgombea wake kwa tiketi ya

urais ambapo hatimaye Dokta Magufuli aliibuka mshindi, na mwishowe alifanikiwa kushinda

kiti cha urais.

Tofauti na chaguzi zilizopita, kwa mara ya kwanza tangu Tanzania iingie kwenye mfumo

wa vyama vingi, CCM ilikuwa na jina la kada mmoja lililozungumwa mno kuwa na uwezekano

wa kugombea urais katika uchaguzi huu. Jina hilo si jingine bali la kada wa siku nyingi wa

chama hicho aliyeshika nyadhifa mbalimbali katika awamu tofauti, na hatimaye kuwa Waziri

Mkuu, Edward Lowassa. Licha ya utumishi wake wa muda mrefu serikalini, na kama

ilivyoelezwa katika sura zilizopita, mwanasiasa huyo alikuwa sehemu muhimu ya kampeni za

Rais Kikwete kuingiza madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005. Pamoja na

mfanyabiashara Rostam Aziz, Lowassa na Kikwete walifahamika kama viongozi wa

kinachoitwa ‘Mtandao wa Kikwete,’ kikundi kisicho rasmi kilichojumuisha watu kutoka kada

mbalimbali, kikiwa na lengo la kumwingiza Kikwete madarakani kumrithi Raia wa Awamu ya

Tatu, Benjamin Mkapa.

Taarifa zisizo rasmi zinaelezwa kuwa ‘Mtandao’ huo uliundwa mara baada ya Kikwete na

Lowassa kushindwa azma ya mmoja wao kuingiza Ikulu katika uchaguzi wa mwaka 1995,

ambapo inaelezwa kuwa Nyerere alitumia nguvu zake kubwa kisiasa kuwazuwia wanasiasa hao

na papo hapo ‘kumbemba’ mwanasiasa chaguo lake, yaani Mkapa.

Taarifa hizo zilieleza kuwa kulikuwa na makubaliano kati ya Kikwete na Lowassa

kupokezana urais aidha baada ya miaka mitano ya Kikwete madarakani aua atakapomaliza

mihula yote miwli. Hata hivyo, kashfa ya Richmond iliyopelekea Lowassa kujiuzulu ilionekana

kujenga mpasuko sio tu katika ‘makubaliano’ hayo bali pia katika kinachoelezwa kuwa urafiki

wa muda mrefu kati yao.

Tetesi kuwa Lowassa angewania urais zilianza kitambo, lakini zilipata nguvu zaidi wakati

CCM ikijiandaa kwa uchaguzi wa mwaka 2010 ambao kwa mujibu wa taratibu zisizo rasmi

ndani ya chama hicho, rais aliyekuwa madarakani alistahili kupitishwa kugombea tena ili

amalizie awamu yake ya pili. Wakati huo, kulikuwa na tetesi zisizo rasmi kuhusu uwezekano wa

Lowassa kuachana na Kikwete ili nae agombee, lakini tetesi hizo zilipotea haraka kama

zilivyozuka.

Hata hivyo, dalili za Lowassa kujiimarisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka

zilijidhihirisha zaidi katika chaguzi za ndani za CCM mwaka 2012, ambapo makada waliokuwa

wakimuunga mkono walifanikiwa kushinda nyadhifa mbalimbali, huku ikidaiwa kuwa wengi

wao walisaidiwa kifedha na Lowassa na washirika wake. Ushindi huo ulionekana kama mwanzo

wa kilichokuja kufahamika kama ‘kambi ya Lowassa’ ndani ya CCM.

Kadri siku zilivyokwenda ndivyo tetesi za Lowassa kuwania urais zilivyozidi kupamba

moto. Hata hivyo, kadri tetesi hizo zilivyopamba moto ndivyo upinzani dhidi yake, hususan

ndani ya CCM, ulivyozidi kujitokeza, kubwa zaidi likiwa wazo la ‘CCM kujivua magamba,’

lilishikiliwa kwa nguvu kubwa na kada kijana, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye. Wazo

Page 16: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

hilo lilionekana kuwavutia sio wana-CCM tu bali hata wananchi wengine wasiojihusisha na

chama hicho tawala. Kimsingi, ilionekana kuwa chama hicho kimetambua makosa yake na kina

nia ya kujirekebisha. Kadhalika, hatua hiyo ilonekana kutambua jinsi ajenda ya ufisadi

ilivyokuwa ikivipaisha vyama vya upinzani hususan Chadema, huko CCM ikitumia muda

mwingi kujitetea.

‘Kujivua gamba’ ilikuwa moja ya fursa adimu na muhimu kwa chama hicho tawala

kurejesha imani kwa wanachama wake na Watanzania kwa ujumla. Yayumkinika kuhitimisha

kuwa laiti mpango huo ungefanikiwa, CCM isingekuwa inapitia wakati mgumu kwenye kampeni

za kuwania uraia wakati huu ninapoandika kitabu hiki. Urahisi katika utekelezaji wa mpango huo

ulikuwa kwenye ukweli kwamba kuna wana-CCM wengi waliokuwa wakiuafiki, na wananchi

kwa ujumla walikuwa na mtizamo chanya.

Lakini licha ya mpango huo kufanikiwa kiasi kwa kupelekea mmoja ya wanasiasa

waliokuwa na nguvu kubwa ndani ya CCM, Rostam Aziz, kuamua kujiuzulu ubunge na nyadhifa

zake ndani ya chama hicho, kwa kiasi kikubwa kinachotajwa kama ‘nguvu ya Lowassa’

kilifanikiwa kuuzima. Kikwazo kingine kwa mpango huo kilikuwa Rais Kikwete, ambaye pia ni

Mwenyekiti wa CCM Taifa, kuonekana kumtumia Nape kufanikisha mkakati huo pasipo ushiriki

wake yeye (Kikwete) mwenyewe.

Hoja kubwa dhidi ya ‘kujivua gamba’ zilikuwa ni pamoja na kuushutumu mpango huo kuwa

ungepelekea kuigawa CCM, sambamba na kumtuhumu Nape kuwa anamwandama Lowassa kwa

sababu binafsi. Kwa ujumla, wazo hilo zuri liligeuzwageuzwa hadi kuonekana kuwa lingekuwa

na athari zaidi kuliko faida kwa chama hicho.

Kipenga cha mbio za kuwania urais kwa tiketi ya CCM kilipulizwa na rasmi na kada kijana,

Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia na msaidizi wa zamani wa Rais Kikwete, January

Makamba, kutangaza nia ya kuwania urais, takriban mwaka mmoja kabla ya kuanza rasmi kwa

mchakato kamili wa CCM. Tangazo hilo la January liliingiza CCM kwenye zama mpya kwani

huko nyuma suala la kuwania urais lilifanywa kwa siri hadi ulipokaribia muda kwa chama hicho

kuanza mchakato wake.

Licha ya hofu kuwa kwa kutangaza nia ya kuwania urais mapema hivyo January angeweza

kuwapa ‘silaha’ maadui zake kisiasa, Watanzania wengi walilipokea vema tamko lake huku

wengi wakiona kuwa ni vema kwa wanasiasa wanaotaka kuwania urais kujitokeza hadharani

mapema ili wananchi wawafahamu vema. Kwa upande mwingine, tangazo hilo la January

lilikuwa changamoto kubwa kwa Lowassa ambaye jina lake lilikuwa likihusishwa na urais kwa

miaka kadhaa.

Pamoja na kuulizwa mara kadhaa iwapo atawania urais, Lowassa aliendelea kukaa kimya,

hatua inayoweza kuwa ilichangia kutofanikiwa kwa dhamira yake ya kuwa mrithi wa ‘rafiki

yake wa zamani,’ Kikwete. Katika mazingira ya kawaida tu, ilionekana kuwa iwapo mwanasiasa

kijana kama January anapata ujasiri kuwatangazia Watanzania kuwa anataka kuwania urais,

kwanini mkongwe kama Lowassa ashindwe kuwa muwazi kwa wananchi? Yawezekana alikuwa

hajaamua kwa dhati kuchukua hatua hiyo au huenda ulikuwa ni mkakati wenye lengo la

kuwashtukiza watu, lakini vyovyote ilivyokuwa, safari yake ya muda mrefu kutaka urais kupitia

CCM iliisha baada ya jina lake kukatwa na vikao vya mchujo.

Uamuzi wa January kutangaza mapema kuwa atawania urais hatimaye ulipelekea wanasiasa

wengine nao kuanza kuzungumzia hadharani kuwa wana nia ya kufanya hivyo japo hawakuwa

wawazi sana. Pengine kutokana na ugeni wa utaratibu wa wanasiasa kutangaza nia ya urais

kitambo kabla ya mchakato wa uchaguzi kuanza, au pengine kwa sababu za kihafidhina tu,

tangazo la January lilikumbana na vikwazo ndani ya chama chake ambapo ziliibuka tuhuma

Page 17: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kuwa mwanasiasa huyo, na baadaye makada wenzie watano, Lowassa, Bernard Membe, Stephen

Wassira, Waziri Mkuu wa zamani Frederick Sumaye, na William Ngeleja, kukaripiwa na chama

hicho kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kukiuka taratibu na kanuni za CCM za uchaguzi. Pamoja

na kukaripiwa, makada hao ‘walihukumiwa kifungo’ cha miezi kadhaa, japo kiuhalisia takriban

wote waliendelea kujinadi wakati wa ‘kifungo’ hicho.

Mara baada ya chama hicho kufungua rasmi mchakato wa kuomba ridhaa ya kuwania urais

kwa tiketi ya chama hicho, Juni 6, 2015, makada kadhaa walijitokeza kuchukua fomu. Kwa mara

ya kwanza katika historia ya CCM, na ya Tanzania kwa ujumla, makada 43 walichukua fomu.

Orodha ya makada hao ni kama ifuatavyo:

1. Amos Robert Siyatemi

2. Augustine Ramadhani.

3. Balozi Ali Karume

4. Balozi Amina Salum Ali

5. Bernard Membe

6. Boniface Ndengo

7. Charles Makongoro Nyerere

8. Dk. Asha Rose Migiro

9. Dk. Augustine Mahiga

10. Dk. Harrison Mwakyembe

11. Dk. John Magufuli

12. Dk. Khamis Kigwangallah

13. Dk. Mwele Malecela

14. Dk. Titus Kamani

15. Dk. Mohamed Gharib Bilal

16. Dk. Muzzamil Kalokola

17. Edward Lowassa

18. Frederick Sumaye

19. Hassy Kitine

20. Hellen Elinawinga

21. January Makamba.

22. Lazaro Nyalandu

23. Leonce Mulenda

24. Lidephonce Bilohe

25. Luhaga Mpina

26. Maliki Marupu

27. Mathias Chikawe

28. Mizengo Pinda

29. Mohamed Gharib Bilal

30. Monica Mbega.

31. Musa Mwapango

32. Mwigulu Nchemba

33. Patrick Chokala

34. Peter Isaiah Nyalali

35. Peter Nyalali.

36. Prof Mark Mwandosya

Page 18: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

37. Prof. Sospeter Muhongo

38. Ritha Ngowi

39. Samuel Sitta

40. Samwel John

41. Stephen Wassira

42. Veronica Kazimoto

43. William Ngeleja

Hata hivyo, kati ya wagombea hao 43, wanne kati yao hawakurejesha fomu na hivyo

kufanya majina yaliyopelekwa kwenye vikao vya mchujo vya CCM kubaki 38 tu. Wagombea

hao walioshindwa kurejesha fomu ni Dkt Kalokola, Elinawinga, Chalamila na Nyalali.

Zoezi hilo la kuchukua na kurejesha fomu lilishuhudia sehemu kubwa ya watendaji wa

serikali wakiwania kumrithi Rais Kikwete, ambapo Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri

10 na Manaibu Waziri wawili, sambamba na Jaji Mkuu Mstaafu mmoja, Wakurugenzi wakuu

wawili wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, na wengineo.

Wingi huo wa makada ulizua mjadala wa aina yake. Kwa upande mmoja, kuna waliotafsiri

idadi hiyo kubwa kuwa ni dalili za kushamiri kwa demokrasia ndani ya chama hicho, wakirejea

historia ya zama za chama kimoja ambapo jina moja tu la mwanachama mmoja tu liliwasilishwa

kwa ajili ya kupigiwa kura katika vikao vya CCM.

Hata hivyo, baadhi ya watu walitafsiri wingi huo kuwa ni ‘athari’ ya wazi ya miaka 10 ya

Kikwete madarakani. Wenye mtizamo huo walidai kuwa urais wa Kikwete ulishusha hadhi ya

taasisi ya urais kiasi kwamba ‘kila mtu alidhani anaweza kuwa rais.’

Tukirejea kwenye jitihada binafsi za makada kuwania nafasi hiyo, kuna mambo kadhaa

yaliyojitokeza yanayopaswa kugusiwa hapa. Kubwa zaidi lilikuwa jinsi Lowassa alivyoonekana

kupata ufuasi mkubwa, mara baada ya kutangaza nia na katika muda wote aliopita maeneo

mbalimbali kusaka wadhamini. Na japo kanuni za chama hicho zilimtaka mgombea kupata

wadhamini 450 katika mikoa 15, mwanasiasa huyo alipata wadhamini 1,600,000. Kwa jinsi hali

ilivyokuwa wakati huo, isingekuwa jambo la kushangaza kuhisi kuwa kilichokuwa kikisuburiwa

ni Lowassa kuapiashwa tu na kuwa rais.

Hata hivyo, pamoja na dalili hizo za kukubalika na wengi, ndani ya CCM kulikuwa na sauti

kadhaa za upinzani dhidi yake. Kwa mfano, mara kadhaa, ‘hasimu’ wake wa muda mrefu, Nape,

alitoa matamshi yalioashiria kuwa kuna jitihada za kumzuwia Lowassa kuteuliwa kuwa

mgombea urais kwa tiketi ya CCM. Kadhalika, baadhi ya wagombea, kwa mfano Makongoro

Nyerere, Waziri Mkuu wa zamani Sumaye, na Waziri Sitta, walitumia hotuba zao mbalimbali

zilizoashiria kuwa na ujumbe kuwa “Lowassa hafai.”

Katika muda wote huo Rais Kikwete hakuonyesha dalili yoyote iwapo anamuunga mkono

Lowassa au la. Hilo lilichangia kwa kiasi kikubwa kuugeuza mchakato huo kuwa kama

‘referendum’ kwa wanasiasa hao, ambapo kwa upande mmoja, swali lilikuwa, “Je Kikwete

‘atamtosa’ rafiki yake au ‘atambemba’?” Na kwa upande mwingine, swali kuhusu Lowassa

lilikuwa, “atakatwa (katika vikao vya mchujo vya CCM) au hatokatwa?”

Pengine moja ya dalili za awali kuwa licha ya ufuasi mkubwa alioupata wakati anasaka

wadhamini sehemu mbalimbali, na licha ya kutajwa kwa muda mrefu kuwa angegombea urais,

Lowassa hakuwa na hakika iwapo Kikwete atamuunga mkono, ni katika kurejea mara kwa mara

katika mikutano yake kauli kwamba anaamini ‘rafiki yake huyo atamsapoti kama yeye

alivyomsapoti mwaka 2005.’ Haihitaji uelewa mkubwa wa ‘jinsi urafiki unavykuwa’ kutambua

kuwa ‘marafiki walioshibana hawahitaji kukumbushana fadhila walizofanyiana huko nyuma.’

Page 19: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kwamba kama kweli urafiki wa wawili hao ni wa dhati basi watasaidiana tu pasi haja ya

Lowassa kukumbushia msaada wake kwa Kikwete miaka 10 iliyopita.

Kwa upande mwingine, ukimya wa Kikwete tangu ‘rafiki yake’ huyo alipotangaza nia ya

kuwania urais, na kurejea kauli kwamba ‘hana mgombea wake,’ ilianza kujenga hisia kuwa

huenda tetesi kuwa urafiki kati ya wanasiasa hao wawili si mzuri zina ukweli. Hata hivyo, kwa

vile kwa kiasi kikubwa urafiki kati yao umekuwa ni suala la kuhisiwa zaidi kuliko kuthibitishwa

nao hadharani, baadhi ya watu waliamini sio rahisi kwa Kikwete ‘kumtosa’ Lowassa, na

kinachotajwa kama ‘tofauti kati yao’ ni sehemu tu ya mkakati wao.

Wakati ‘safari ya urais wa Lowassa’ ilichangiwa zaidi na jina lake kutajwa kuwa mrithi wa

Kikwete kwa muda mrefu kuliko mwanasiasa mwingine yeyote yule, kada aliyeendesha

‘kampeni’ zake kwa umahiri mkubwa ni January. Awali, alipotangaza nia, takriban mwaka

mmoja kabla ya CCM kuanza rasmi mchakato wa kumpata mgombea wake, baadhi ya watu

walidhani kuwa hakuna na dhamira ya dhati, na pengine ‘anamsafishia njia mgombea

mwingine.’ Hata hivyo, kadri siku zilivyokwenda, na licha ya ‘kebehi’ za mara kwa mara

alizokumbana nazo, mwanasiasa huyo kijana alionekana kutotetereka katika dhamira yake.

Baadaye, January alichapisha visheni yake aliyoiita ‘Tanzania mpya,’ ambayo kwa kiwango

kikubwa ilibainisha matatizo yanayoikabili nchi yetu na namna ya kuyatatua. ‘Kampeni’ ya

January ilifanikiwa zaidi kutokana na mambo makuu mawili, kwanza, ukaribu aliojenga na

vijana hususan katika mitandao ya kijamii, na pili, kuwa mtu anayefikika (approachable) na

wengi. Licha ya sababu hizo mbili, mwanasiasa huyo kijana amejaaliwa kipaji cha kuongea

lugha inayoeleweka kirahisi kwa mtu wa rika na kada yoyote. Jinsi ‘alivyouza’ ajenda yake ya

‘Tanzania mpya’ iliwafanya watu wengi kumwelewa na pia kumsaidia kupata ufuasi mkubwa.

Sambamba na hilo, wasanii kadhaa walionekana kumuunga mkono na hiyo ilisadia kuwavuta

wafuasi wa wasanii hao kumkubali mwanasiasa huyo, msaidizi wa zamani wa Rais Kikwete na

mtoto wa Katibu Mkuu wa zamani wa CCM.

Lakini mchakato huo wa CCM kumpata mgombea wake uliambatana na ‘vituko’ pia,

kikubwa kikiwa uamuzi wa Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

kuwania nafasi hiyo. Miezi machache tu kabla, jina la mwanasiasa huyo msomo lilivuma mno

kufuatia kashfa ya Tegeta Escrow ambayo hatimaye ilipelekea kujiuzulu licha ya awali kudai

kuwa asingefanya hivyo. Lakini pengine hata kama Profesa Muhongo asingehusishwa na kashfa

hiyo, Watanzania wengi walikuwa wanamkumbuka kwa kauli yake kuwa uwezo wa Watanzania

kuwekeza unaishia kwenye juisi na matunda. Alisema hayo alipoombwa na taasisi moja asitishe

zoezi la kutoa vitalu vya gesi asilia kwa wageni hadi sera ya gesi na mafuta iwe tayari ili

kuwezesha Watanzania nao kuingia ubia au kushiriki umiliki wa uchumi wa gesi. Wengi

walijiuliza, “hivi huyu mtu ambaye majuzi tu kulazimika kujiuzulu kwa kashfa ya Tegeta

Escrow, amepata wapi ujasiri wa kuwania urais?” Ni katika mazingira kama hayo, hoja kwamba

kujitokeza kwa wana-CCM wengi kuwania urais imechangiwa na ‘thamani ya urais kushuka’

ilionekana kupata nguvu.

Kingine kilichojitokeza wakati wa ‘kampeni’ za makada mbalimbali wa CCM kuwania urais

ni matumizi ya mitandao ya kijamii. Kama kuna suala moja litakaloingia kwenye historia ya

uchaguzi mkuu nchini Tanzania basi ni hili la jinsi matumizi ya teknolojia ya kisasa, hsusan

mitandao ya kijamii, yalivyowezesha ushirikishwaji wa kisiasa kwa wananchi wengi, wanasiasa

waliokuwa wakiwania kuteuliwa kuwa wagombea urais na wananchi wa kawaida kwa ujumla.

Kwa mara ya kwanza, wananchi waliokuwa mtandaoni walipata fursa ya kuwahoji

wanasiasa hao, sambamba na wao kutumia fursa hiyo kuwaeleza Watanzania mikakati yao

iwapo wangepewa ridhaa na chama hicho kuwa wagombea. Kwa bahati mbaya, kwa kiasi

Page 20: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kikubwa suala hili halijapewa uzito mkubwa, labda pengine kutokana na ukweli kuwa idadi

kubwa ya watumiaji wa mitandao ya kijamii ‘hawachukulii mambo ya mtandaoni kwa uzito

mkubwa.’ Hisia kuwa ‘Watanzania wanaotumia mtandaoni ni asilimia ndogo tu ya Watanzania

wote’ imekuwa kigezo muhimu kwa watu wengi kutoyachukulia yanayojiri mtandaoni kwa uzito

unaostahili. Hata hivyo, ukweli kwamba wanasiasa kadhaa walitambua umuhimu wa teknolojia

hiyo kuwasiliana na wananchi unaonyesha kuwa Tanzania imepiga hatua ya kuridhisha katika

matumizi ya teknolojia ya mawasiliano.

Suala jingine muhimu kabisa ni idadi ya wanawake waliojitokeza kuomba ridhaa ya CCM

kuwania urais, ambapo makada sita wa kike walijitokeza. Makada hao ni Dkt Mwele Malecela,

Dkt Asha-Rose Migiro, Balozi Amina Salum Ali, Monica Mbega, Ritha Ngowi na Hellena

Elinawinga. Kujitokeza kwa idadi hiyo ya kuridhisha ya wanawake kulijenga hisia kuwa iwapo

Tanzania haitopata Rais mwanamke basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata mgombea

mwenza, na pengine hatimaye mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa umakamu wa rais.

Hata hivyo, jambo la kusikitisha ni kwamba kwa kiasi kikubwa makada hao hawakupewa

sapoti ya kutosha na wanawake wenzao, kwenye chama chao na hata ‘mtaani.’ Hii ni

changamoto kubwa kwa wanawake nchini Tanzania kwa sababu licha ya ukweli kwamba

uongozi ni suala la uwezo lakini jamii nyingi duniani, hususan Barani Afrika, zimekuwa

zikikandamiza nafasi za wanawake katika uongozi, na hii ilikuwa fursa nzuri kwa wanawake wa

Tanzania kuwasapoti wanawake wenzao.

Hatimaye, Julai 2,2015 zoezi la kusaka wadhamini na kurejesha fomu za kuwania ridhaa ya

CCM kumteua mgombea wake wa urais lilifikia ukingoni na makada walioweza kurejesha fomu

walifanya hivyo. Kilichosubiriwa kwa hamu kilikuwa uamuzi wa vikao vya chama hicho tawala

kuchuja wagombea wake na hatimaye kumpata mmoja atakayekiwakilisha chama hicho katika

uchaguzi mkuu.

Mara baada ya kikao cha kwanza, cha Kamati ya Usalama na Maadili ya CCM kumaliza

kikao chake, kulisikika uvumi kuwa jina na Lowassa halikupitishwa. Uthibitisho sahihi kuhusu

tetesi hizo ulipatikana Julai 11, 2015 baada ya chama hicho kutangaza rasmi majina matano ya

makada wake waliopitishwa, na ambayo yangepigiwa kura katika Mkutano Mkuu wa CCM.

Taarifa za kukatwa kwa jina la Lowassa zilizokelewa kwa mshtuko mkubwa, na wakati fulani

zilisikika tetesi kuwa ‘wafuasi wa Lowassa’ walipanga kufanya mapinduzi ya kumng’oa

Kikwete na Kamati Kuu ya Chama hicho. Baadhi ya ‘wafuasi’ hao, walijitokeza hadharani

kupinga maamuzi ya chama chao kukata jina la mwanasiasa huyo.

Taarifa zisizo rasmi zinaelezwa kuwa marais wa zamani, Mwinyi na Mkapa walifanya kazi

kubwa kumnusuru Kikwete na uhai wa chama hicho kwa ujumla kwa maelezo kwamba kanuani

na taratibu za chama hizo ziwekwe mbele ya maslahi ya mtu binafsi (Lowassa). Inadaiwa Mkapa

alikwenda mbali na kuwatakia wajumbe wa vikao hivyo wanaodhani kuwa Lowassa

hakutendewa haki aidha warejeshe kadi zao za uanachama wa CCM, kwa maana ya kujiondoa

wenyewe kwenye chama hicho, au waafiki maamuzi ya vikao hivyo.

Hatimaye Julai 11, 2015 Dokta Magufuli alifanikiwa kupita mchujo wa kwanza baada ya

jina lake kuwa miongoni mwa majina matano yaliyopitishwa na Kamati Kuu ya CCM. Makada

wengine walikuwa January Makamba, Bernard Membe, Balozi Amina Salum Ali, na Dokta

Asha-Rose Migiro.

Nyota ya urais kwa Dokta Magufuli iliendelea kung’ara baada ya kufanikiwa kupita mchujo

wa pili ambapo yeye, Balozi Amina na Dokta Asha-Rose walipitishwa, na kuwashinda January

na Membe. Na dalili ya uwezekano wa yeye kuibuka mshindi katika hatua ya mwisho ilionekana

kwenye idadi ya kura walizopata makada ahao, ambapo Dokta Magufuli alipata kura 290,

Page 21: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

akifuatiwa na Balozi Amina (kura 284), Dokta Asha-Rose (kura 280), January (kura 124), na

Membe (kura 120).

Taarifa zinaeleza kuwa kwa vile kambi ya Lowassa iliamini kuwa Membe ndio chaguo la

Kikwete, na January alionyesha upinzani mkubwa kwa ‘mgombea wao,’ kura zao nyingi

zilielekezwa kwa Magufuli, Dkt Asha-Rose na Balozi Amina. Katika duru la mwisho, Magufuli

aliibuka mshindi kwa kura 1560, akifuatiwa na Dkt Asha-Rose alaiyepata kura 702 na Balozi

Amina kuambulia kura 349.

Awali kulikuwa na hisia kuwa kwa vile ‘tatu bora’ ilikuwa na makada wawili wa kike basi

huenda mshindi angekuwa mwanamke pia. Hata hivyo, wachunguzi wa siasa wanadai wakati

Dkt Asha-Rose hakuwa na ushawishi mkubwa wa kumwezesha kusinda nafasi hiyo,

kilichomwangusha Balozi Amina ni hotuba yake ya kuomba kura ambapo alionekana kama

anayetaka ‘kura za huruma kutoka kambi ya Lowassa,’ sambamba na dalili kuwa huenda

‘angamvuta’ Lowassa kuwa nae kama mgombea mwenza endapo mwanamama huyo angeshinda

katika kinyang’anyiro hicho.

Yayumkinika kuhitimisha kuwa mafanikio ya Magufuli hadi kuteuliwa kuwa mgombea

rasmi wa chama hicho yalichangiwa zaidi na ‘siasa za kumzuwia Lowassa’ kwa upande mmoja,

na ‘hasira za kambi ya Lowassa dhidi ya Membe.’ Hata hivyo, kwa kumchagua Magufuli, CCM

iliweza kumpata mgombea ambaye wa kiasi kikubwa alikuwa mmoja wa watendaji wachache

kabisa katika chama hicho wenye kusifika kwa uchapakazi. Tangu jina lake lilipotangazwa

rasmi, sambamba na kada aliyemteua kuwa mgombea mwenza, Samia Suluhu, taswira

iliyojitokeza mtaani iliashiria kuwa chama hicho tawala kisingekuwa na kazi ngumu kumnadi

mgombea huyo ambaye licha ya kusifika kwa uchapakazi, alisifika kwa kuweka mbele maslahi

ya taifa badala ya kuendekeza itikadi za kisiasa, sambamba na kipaji cha kujieleza kwa ufasaha

Kwa upande mwingine, ‘sintofahamu’ ilijitokeza kuhusu hatma ya Lowassa, kada ambaye

sio tu jina lake lilianza kusikika mapema kuwa angewania nafasi hiyo na kujizolea ufuasi

mkubwa lakini pia hadi muda huo alikuwa mwanasiasa mwenye nguvu zaidi ndani na nje ya

chama hicho. Swali kubwa lililotawala vichwa vya Watanzania liligeuka kutoka ‘atakatwa au

hatakatwa (na vikao vya mchujo vya CCM)’ na kuwa ‘atahama CCM au atabaki katika chama

hicho (hasa ikirejewa kauli zake za awali kuwa wanaomtaka atoke katika chama hicho watoke

wao na sio yeye).

Hatimaye, Julai 28, 2015, takriban wiki mbili baada ya jina lake kukatwa na vikao vya

CCM, Lowassa alitangaza kuihama CCM na kujiunga na Chadema. Siku chache baadaye, vyama

vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), vilimpitisha Lowassa kuwa mgombea

wao wa nafasi ya urais.

Katika kuhitimisha sura hii, ni muhimu kupigia mstari jinsi ushindi wa Magufuli, na

kushindwa kwa Lowassa, kulivyoenda kinyume na ubashiri wa wachambuzi mbalimbali wa siasa

za Tanzania, ikiwa ni pamoja nami mwandishi wa kitabu hiki. Kwa upande wangu, nilibashiri

uwepo wa makundi makuu matatu ambayo yangeweza ‘kuzaa’ mgombea urais kwa tiketi ya

CCM. Makundi hayo ni, kwanza, makada wenye nafasi kubwa, ya kati na wenye nafasi ndogo.

Katika kundi la kwanza Katika kundi la kwanza niliwaweka Jaji Ramadhan, Lowassa,

January, Makongoro, Dkt Bilal, Pinda na makada watatu wanawake, yaani Dkt Mwele, Dkt

Asha-Rose na Balozi Amina.

Jaji Ramadhani aliingia kundi hilo kutokana na sababu za wazi. Ushahidi wa kimazingira

wakati huo ulionyesha kama ndio alikuwa mgombea ‘turufu’ kwa CCM, hasa katika kile

kilichotajwa kama ‘kumdhibiti Lowassa.’ Pia kulionekana dalili kuwa Jaji huyo Mkuu mstaafu

alikuwa chaguo la Kikwete kwa kurejea baadhi matamshi yake huko nyuma. Kadhalika, uhaba

Page 22: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

wa makada wa CCM wenye rekodi ya kupendeza japo kidogo ulimfanya Jaji Ramadhani

kuonekana mwenye na nafasi ya juu zaidi.

Kuhusu Lowassa, sababu mbili zilizopelekea kuingizwa kundi hilo la kwanza ni, kwanza,

historia yake na Kikwete, angalau hadi wakati huo. Mtizamo maarufu wakati huo ulikuwa

kwamba laiti sakata la Richmond lisingetokea na Lowassa kulazimika kujiuzulu, basi muda huo

ingekuwa inasubiriwa kutawazwa kwake tu, yaani kupasisha utawala kwa mtu pasi haja ya

uchaguzi.

Mengi ya yalikuwa yakisemwa kuhusu uhusiano wake na Kikwete hayakuwahi

kuthibitishwa, lakini iliyumkinika kuhisi kuwa kadri Lowassa alivyomsaidia Rais Kikwete

mwaka 2005 ndivyo Kikwete alivyotarajiwa ‘kulipa fadhila’ katika uchaguzi mkuu huu.

Sababu ya pili ilikuwa uwezo wake mkubwa kifedha ambao kwa kiasi kikubwa ulichangia

kile kilichoonekana kama kukubalika kwake kwa wananchi wengi. Ilikuwa muhimu sana

kutopuuza nafasi ya fedha katika kinyang’anyiro hicho hasa kwa kuwa chaguzi nyingi za CCM

hutawaliwa mno na nguvu ya fedha kiasi hata uchaguzi wa viongozi wa chipukizi wa chama

hicho uliwahi kuhusishwa na matumizi makubwa ya fedha.

Kwa upande wa January, aliingia katika kundi hili kwa sababu kuu mbili. Kwanza, alikuwa

kada wa kwanza kutangaza hadharani nia yake ya kuwania urais. Hatua hii ilionekana kumsaidia

sana kutambulika kwa watu wengi hususani miongoni mwa vijana wanaotumia mitandao ya

kijamii. Sambamba na hilo, kada huyo kijana alijizolea ufuasi mkubwa miongoni mwa wasanii

maarufu na wenye mashabiki wengi ambao licha ya kumsapoti pia walikuwa wakimnadi

hushusan katika mitandao ya kijamii.

Sababu ya pili ilikuwa nguvu kubwa mno aliyotumia ‘kujinadi’. Licha ya kuandika kitabu

kinachoelezea ajenda yake ya ‘Tanzania Mpya,’ mwanasiasa huyo alifanya kazi kubwa ya

kujinadi, huku akisaidiwa na wasanii kadhaa ‘wenye majina makubwa.’ Kimsingi, kada

mwingine pekee anayelingana na Makamba kwa ‘kampeni’ kubwa alikuwa Lowassa, ambaye

hata hivyo, tofauti na Makamba, alikuwa akifanyiwa zaidi ‘kampeni’ hizo na wapambe kuliko

yeye mwenyewe.

Kuhusu Makongoro, kikubwa kinachomwingiza Makongoro katika kundi hili ni ukweli

kwamba yeye ni mtoto wa Nyerere, na takribani kila Mtanzania anayeitakia mema nchi yetu

bado anamlilia Mwalimu Nyerere. Kwa kuwa mtoto wa Baba wa Taifa, kulikuwa na hisia

kwamba ‘tunaweza kumpata Nyerere mwingine,’ jambo ambalo ilikuwa kama ndoto njema ya

Watanzania wengi.

Lakini kingine ni ukweli kuwa Makongoro alikuwa muwazi mno katika kuikosoa CCM, na

alijitahidi sana kutotoa ahadi kwa kigezo kuwa ahadi za mgombea wa chama hicho shurti

ziendane na ilani ya uchaguzi ya chama hicho ambayo ilikuwa haijatolewa hadi muda huo.

Kuhusu Bilal na Pinda, kitu pekee kilichofanya waingie katika kundi hilo ni ukweli kwamba

walikuwa wasaidizi wa karibu wa Rais Kikwete katika miaka 10 iliyopita. Kwa taratibu zisizo

rasmi katika siasa za Afrika, hakuna Rais anayemaliza muda wake atakayethubutu kumkabidhi

madaraka kwa mtu asiyemjua, na Kikwete na makada hao walikuwa wakijiuana vizuri kutokana

na ukaribu wao kikazi. Kadhalika, Uzanzibari wa Bilal ulitarajiwa kuwa ‘mtaji’ kwake pia iwapo

ingeamuliwa na CCM kuwa mgombea wake ajaye wa urais ajaye Zanzibar.

Kwa Pinda, mara kadhaa alionekana ‘kubebeshwa lawama’ katika masuala ambayo pengine

lawama zilipaswa kwenda kwa bosi wake, yaani Rais Kikwete. Ilidhaniwa kwamba kwa

‘kukubali ‘kurushiwa risasi ili kumkinga Rais wake, huenda Kikwete angelipa fadhila kwa

kumnadi awe mrithi wake.

Page 23: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kwa upande wa makada watatu wanawake, niliwapa nafasi sawa Dkt Mwele, Dkt Asha-

Rose na Balozi Amina kutokana na kila mmoja kuwa na ‘turufu’ zake. Kwa Dkt Mwele, licha ya

kuendesha ‘kampeni’ yake kistaarabu sana, alikuwa na faida ya kuwa ‘mgeni’ katika siasa, kwa

maana isingikuwa rahisi kuhusishwa na mapungufu yaliyoelekezwa kwa makada wengine

waliokwishashika nyadhifa katika chama hicho. Kwa Migiro, ilitarajiwa kuwa wasifu wake

kama mmoja wa wanawake wachache wenye nguvu katika ngazi za juu za chama hicho, na

wadhifa wake wa zamani kama Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ungeweza

kumsaidia.

Kwa Balozi Amina, ‘turufu’ zake ilitarajiwa kuwa Uzanzibari wake, utumishi wake wa

muda mrefu katika taasisi za kimataifa, na ukweli kwamba hilo lilikuwa jaribio lake la pili

kwania fursa hiyo.

Kundi la pili lilijumuisha makada walioonekana kuwa na nafasi ya kati. Binafsi, nilibashiri

kuwa kundi hilo lingeweza kutoa ‘surprise candidate’ angalau kuingiza kwenye ‘tano bora,’ na

nilikuwa sahihi kwani Dokta Magufuli alitoka kwenye kundi hilo, kada ambaye licha ya

kutanguliza maslahi ya taifa mbele ya itikadi za kisiasa, alikuwa akisifika kwa uchapakazi.

Pamoja na Dokta Magufuli, kada mwingine katika kundi hilo alikuwa na Membe, ambaye tetesi

zilikuwa zikidai kuwa alikuwa akiungwa mkono na familia ya Kikwete, sambamba na ukweli

kuwa nafasi yake ya Uwaziri wa Mambo na Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ilimweka karibu

sana na mkuu huyo wa nchi. Hata hivyo, licha ya awali kupewa nafasi ya kutoa upinzani mkali

kwa Lowassa, kauli zake angalau mara mbili kuwa angekuwa tayari kumuunga mgombea

mwingine endapo yeye asingepitishwa zilitoa taswira kuwa huenda alishajikatia tamaa.

Mwigulu aliingia katika kundi hilo kutokana na ukweli kwamba kulinganisha na ‘watangaza

nia wengine,’ alikuwa na rekodi ya kipekee katika kupambana na vyama vya upinzani.

Kada wingine alikuwa Balozi Mahiga, ambaye licha ya kuwa mwanadiplomasia wa

kimataifa kwa muda mrefu aliwahi pia kuwa Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa. Tatizo kwa

Balozi Mahiga lilikuwa kutojulikana sana katika medani za siasa za Tanzania, na japo ukweli

kuwa aliwahi kuwa bosi wa ‘mashushushu’ ulitarajiwa kumsaidia kama ‘mgombea mwenye

uwezo wa kukabiliana na tatizo la ufisadi,’ lakini pia ilidhaniwa kuwa sifa hiyo ingeweza

kumkwamishwa na waliohofia kuwa na ‘rais shushushu.’

Mwingine katika kundi hilo alikuwa Profesa Mwandosya, mmoja wa makada waliojaribu

bila mafanikio kuchuana na Kikwete katika kinyanga’anyiro cha CCM kumpata mgombea wake

mwaka 2005. Hata hivyo, nguvu aliyokuwa nayo wakati huo ilikuwa imepungua sana

kulinganisha na mwaka 2015.

Kundi la tatu lilijumuisha makada wengine wote waliochukua fomu kuwania ridhaa ya

chama hicho tawala kuwateua kuwa mgombea wake katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Katika kundi hili kulikuwa na wanasiasa kama Waziri Mkuu wa zamani, Sumaye ambaye

aliingia kundi hili kwa sababu tayari alikuwa ‘na maadui wengi’ ndani ya CCM, hivyo ni

ingekuwa vigumu mno kupitishwa kuwa mgombea wa chama hicho. Baadaye Sumaye alitangaza

kuhama chama hicho na kujiunga na UKAWA, na suala hilo litajadiliwa kwa kirefu katika sura

ijayo.

Makada wengine, kama Ngeleja na Profesa Muhongo, waliingia katika kundi hilo la

wagombea wenye nafasi finyu kutokana na ukweli kwamba hadi muda huo majina yao yalikuwa

yakifahamika zaidi kuhusiana na skandali kuliko utendaji kazi wao. Kwa upande wa Dk.

Mwakyembe na Sitta, nafasi zao zilionekana kuwa finyu kutokana na kilichotajwa mara kadhaa

kuwa na ‘uhasama wake na Lowassa’ ambao ulitarajiwa ungepelekea upinzani mkali dhidi yao.

Page 24: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Moja ya maswali ambayo hadi leo ‘hajayajapatiwa majibu’ ni jinsi Jaji Ramadhan

alivyoishia kukatwa jina lake licha ya kupewa nafasi kubwa kama ‘mtu pekee anayeweza

kupambana na Lowassa.’ Kimsingi, uamuzi wake wa kutangaza nia ya kugombea urais

uliwashtua wengi hasa ikizingatiwa kuwa rekodi yake ‘safi’ kama Jaji Mkuu wa zamani, afisa

wa zamani wa ngazi ya juu jeshini, na kiongozi wa kidini, ingeweza aidha kuchafuliwa wakati

wa kampeni au kuingiza doa iwapo jina lake lingeishia kukatwa. Kwa bahati mbaya, Jaji

Ramadhan anaweza kukumbukwa zaidi kwa kutamani urais lakini jina lake halikupitishwa,

kuliko rekodi yake ya kuvutia.

Kwa hitimisho, sura hii imezungumzia kwa undani mchakato wa Chama cha Mapinduzi

CCM kumpata mgombea wake Dokta Magufuli, ambaye baadaye aliibuka mshindi wa kiti cha

urais; masuala kadhaa yaliyojitokeza kabla, wakati na baada ya chama hicho kuruhusu makada

wake kuwania nafasi hiyo, na jinsi vikao vya chama hicho vilivyowexza kumpitisha mgombea

wao, Magufuli.

###

Page 25: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Tatu

Changamoto zilizomkabili Magufuli (na CCM) katika uchaguzi mkuu: Pamoja na fursa nyingi

zilizoitengenezea mazingira mazuri ya ushindi CCM na mgombea wake Dokta Magufuli, chama

hicho kiliingia katika uchaguzi huo huku kikikabiliwa na changamoto na vikwazo kadhaa.

Kikwazo kikubwa zaidi ni kilikuwa kwa chama hicho kuhusishwa kwake na kila ‘baya’

lililoihusu Tanzania. Orodha ilikuwa ndefu, lakini kama kuna tuhuma ‘iliyoitafuna’ zaidi CCM

ni suala la ufisadi. Na licha ya tuhuma hizo za ufisadi kuiandama CCM katika awamu zake

mbalimbali, hali katika awamu mbili za Rais Kikwete ilikuwa mbaya mno.

Licha ya yeye binafsi kuonekana kama mwanasiasa ‘msafi’ na mchapakazi, mtihani

mkubwa kwa Dokta Magufuli (na chama chake kwa ujumla) ulikuwa katika kuwaaminisha

wapigakura uwezekano kwa chama hicho kingeweza kubaki hai pasipo kujihusisha na ufisadi.

Kwa muda mrefu, hali ndani ya CCM ilikuwa mbaya mno kiasi kwamba wakati chama hicho

kilipokuja na mkakati wa ‘kujivua magamba,’ watu wengi walidai jaribio hilo lingekiuwa chama

hicho katika namna ileile ya ‘kumuua kobe ukijaribu kumng’oa gamba.’

Kama kuna ajenda moja iliyodhaniwa ingeweza kumnyima Dokta Magufuli na CCM

ushindi ni suala hilo la ufisadi. Na licha ya Lowassa kuandamwa na tuhuma za ufisadi alipokuwa

CCM, chama hicho tawala kilipata wakati mgumu kuzungumzia ‘ufisadi mmoja tu’ huku

chenyewe kikiandamwa na lundo la tuhuma za ufisadi. Na kwa upande mwingine, hoja mbadala

dhidi ya chama hicho ilikuwa ‘ufisadi wa Lowassa si usafi wa CCM.’

Moja ya virutubisho vilivyoufanya ufisadi kuwa kama sehemu ya uhai wa CCM ni

kulindana. Kimsingi, laiti ‘sera ya kulindana’ isingekuwepo, basi CCM isingehangaishwa na

Lowassa katika uchaguzi huo kwa sababu ingeweza kuchukua hatua katika nyakati mbalimbali

dhidi yake kutokana na kuhusishwa kwake na tuhuma za ufisadi.

Kushindwa kwa chama hicho na serikali yake kuchukua hatua dhidi ya ufisadi kulitajwa

kuwa ni moja ya sababu za kukua kwa tatizo hilo, kwa sababu ‘mafisadi watarajiwa’ hawakuwa

na cha kuwaogopesha kufanya majaribio ya ufisadi mpya, kwa kuzingatia kuwa wengi wa

waliokwishafanya hivyo hawakuchukuliwa hatua zozote.

Kibaya zaidi, CCM iliingia kwenye uchaguzi huo huku tuhuma nyingi za ufisadi zikiwa

hazijapatiwa majibu wala hatua kuchukuliwa. Licha ya suala la Richmond kujitokeza mwaka

2006, taarifa mbalimbali kuhusu suala hizo hazikuwa na majibu ya maswali kadhaa

yaliyowasumbua Watanzania wengi. Kwa mfano, wakati Lowassa akituhumiwa kuwa ‘mhusika

mkuu’ katika kashfa hiyo, wapo waliohoji je ‘bosi’ wake, yaani Rais Kikwete, hakuwa na

ufahamu wowote kuhusiana na suala hilo?

Kwa upande wa kashfa ya EPA, hadi wakati wa uchaguzi huo serikali ya CCM ilikuwa

imegoma katakata kuwajulisha Watanzania kuhusu mmiliki wa kampeni ya Kagoda, iliyotajwa

kuwa mnufaika mkubwa wa ufisadi huo. Kwenye kashfa ya Escrow, bado kulikuwa na lundo la

maswali kuhusu, kwa mfano, wakati majina ya waliopewa mgao kupitia Benki ya Mwananchi

yalifahamika, wanufaika wa mgao uliotajwa kuwa mkubwa zaidi kupitia benki ya Standard

Chartered walikuwa hawajatajwa hadharani. Katika kashfa ya Operesheni Tokomeza, Serikali ya

Page 26: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

CCM ilifanya ‘kioja cha mwaka’ kwa kuwasafisha wahusika pasipo kutoa maelezo ya

kuridhisha.

Kushamiri kwa ufisadi, sambamba na kutokuwepo jitihada za dhati kupambana na tatizo

hilo kulionekana kungeweza kuwashawishi baadhi ya wapiga kura, hata waliokuwa wana-CCM,

kukinyima kura chama hicho tawala au mgombea wake Dokta Magufuli.

Licha ya ufisadi wa EPA, Richmond, Escrow na kashfa ya Operesheni Tokomeza, kulikuwa

pia na kashfa nyingine kama ya Meremeta, Tangold, Mwananchi, mgodi wa Kiwira, na

nyinginezo zilizoonekana ‘kuzikwa kienyeji’ bila serikali ya CCM kubainisha majina ya

wahusika wala kuchukua hatua stahili dhidi yao. Tatizo hapo lilikuwa sio tu kashfa hizo

zingeweza kuiathiri CCM katika uchaguzi huo bali pia hofu kuwa zingeweza kuibuka upya huko

mbeleni.

Tukiweka kando kashfa za ufisadi, tangu kustaafu kwa Nyerere, Tanzania iliendelea

kushuhudia ongezeko la uhalifu mkubwa, hususan tatizo sugu la biashara ya madawa ya kulevya,

biashara ya usafirishaji binadamu, utakatishaji fedha na ujangili. Matatizo haya ambayo

yalikuwepo hata kabla ya Kikwete kuingiza madarakani, yalishamiri zaidi katika utawala wake,

ambapo licha ya kuchafua jina la Tanzania kimataifa, nchi yetu ilifikia hatua ya kuonekana kama

ina-export uhalifu (kwa mfano, kuna idadi kubwa tu ya Watanzania waliofungwa katika

magereza ya nchi mbalimbali duniani kwa makosa ya madawa yakulevya)

Kana kwamba matatizo hayo hayakuwa mabaya kwa hadhi ya nchi yetu, kwa muda mrefu

Tanzania ilijikuta ikipata sifa mbaya kutokana na mauaji ya albino, ambapo vyombo vya habari

mbalimbali vya kimataifa vilikuwa vikifuatilia unyama uhalifu huo wa kinyama kwa karibu.

Jitihada za serikali kupambana na tatizo hilo zilikuwa hafifu, huku tuhuma zikielekezwa kwa

wanasiasa ambao baadhi yao walituhumiwa kuwa wateja wa waganga wa kienyeji wanaotumia

viungo vya albino kutengeneza dawa za asili. Japo CCM haikuweza kuhusishwa moja kwa moja

na tatizo hili, ukweli kwamba lilijiri wakati wa utawala wake ungeweza kuwapa nguvu UKAWA

kukibana chama hicho, kwa hoja kwamba kilishindwa kuwalinda maalbino.

Licha ya kuonekana kama ‘kisiwa chama amani na utulivu,’ Tanzania chini ya utawala wa

CCM ilikuwa na rekodi isiyopendeza kuhusu haki za binadamu. Wakati uhalifu wa mauaji ya

albino uliangukia katika eneo hilo, jeshi la polisi lilikuwa likilaumiwa mara kwa mara, hususan

na vyama vya upinzani, kwa ‘kutumia nguvu kubwa zaidi ya akili’ katika matukio kadhaa

yaliyopelekea vifo na majeruhi. Kwa vile CCM ilikuwa kama ina ‘kinga’ dhidi ya vitendo hivyo

vya polisi, ilionekana kutofanya jitihada za kutosha kupambana na ukiukwaji huo wa haki za

binadamu. Kimsingi, chama hicho tawala kilikuwa kikionekana kama kinafurahia mwenendo wa

jeshi la polisi, ambapo wakati fulani, aliyekuwa Waziri Mkuu (2008-2015) Mizengo Pinda alitoa

ruhusa kwa polisi kuwapiga raia badala ya kusisitiza haja ya kuzingatia haki za binadamu.

Yayumkinika kuhitimisha kuwa moja ya sababu za uhusiano hafifu kati ya wananchi wengi

na jeshi la polisi ilikuwa kwa chombo hicho cha dola kupuuzia haki za binadamu hususan pale

maslahi ya chama tawala yalipoguswa. Ni katika mazingira hayo, jeshi hilo lilibandikwa jina la

‘poli-CCM’ likimaanisha ‘polisi wa CCM.’ Chuki za wananchi dhidi ya jeshi hilo lililoonekana

kuipendelea CCM zilihofiwa kuwa zingeweza kukiathiri chama hicho kwenye uchaguzi huo.

Kiuchumi, wakati CCM iliweza kujinadi kwa kutumia takwimu mbalimbali zilizoonyesha

kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa kuboresha uchumi wake, hali halisi ‘mtaani’ ilikuwa

tofauti kabisa. Ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, kipato kisichoendana na hali halisi ya maisha

pamoja na matatizo mengine kama hayo yalipelekea kushamiri kwa rushwa na uhalifu

mwingine. Tofauti za kipato kati ya ‘wenye nacho’ na ‘wasio nacho’ sio tu ilizidi kukua mwaka

Page 27: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

hadi mwaka lakini pia iliongeza hamasa kwa ‘wasio nacho’ kutafuta njia za kuweza kumudu

maisha yao, ambapo mara nyingi kimbilio lilikuwa kwenye uhalifu, ufisadi na rushwa.

Utawala wa CCM ulishuhudia watu kutoka kada mbalimbali katika jamii wakikimbilia

kwenye siasa, kutokana ana siasa kugeuka kuwa ‘ajira ya uhakika zaidi’ kuliko zote. Wasomi

mbalimbali wamekuwa wakiachwa kazi za taaluma na kuingiza kwenye siasa, na kinyume cha

matarajio ya wengi kuwa ujio huo wa wasomi ungechochea maendeleo, wengi wao wameishia

kukumbwa na kashfa za ufisadi kiasi cha kushamiri kwa hisia miongoni mwa Watanzania kuwa

‘wasomi wetu ni miongoni mwa wanaomchangia matatizo katika nchi yetu.’ Ilidhaniwa kuwa

UKAWA ingeweza kuinyooshea kidole CCM ikiituhumu kwa ‘kuzalisha ukame wa

wanataaluma’ na kisha ‘kuwaharibu wanataaluma wanaoingia katika siasa kupita chama hicho,

kwa kuweka kando eilu yao na kukumbatia ufisadi.’

Changamoto nyingine kwa Dokta Magufuli na CCM ilikuwa kuhusu kutochukuliwa hatua

madhubuti kutatua baadhi ya kero sugu zilizokuwa zikiikabili Tanzania. Na moja ya kero hizo

sugu ilikuwa ‘mgao wa kudumu wa umeme.’ Tatizo la mgao wa umeme lililochangiwa kwa kiasi

kikubwa na ufisadi mfululizo linawaathiri na kuwakera Watanzania wengi. Kibaya zaidi, badala

ya utawala wa CCM kuwekeza nguvu kumaliza tatizo hilo, jitihada za baadhi ya watendaji wake

zilielemea zaidi katika kutumia tatizo hilo kama njia ya kufisadi zaidi. Kimsingi, Shirila la

Umeme Tanzania (TANESCO) lilikuwa kama ‘ng’ombe asiye na lishe lakini aliyekamuliwa

maziwa mfululizo hadi kutoa damu badala ya maziwa.’ Hujuma mfululizo dhidi ya Shirika hilo,

katika awamu mbalimbali za utawala wa CCM zilichangia mno kufanya mgao wa umeme kuwa

kama ‘stahili’ ya Watanzania. Wakati wa kampeni za uchaguzi, haikuwa jambo la kushangaza

kukutana na mabandiko kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii yakieleza bayana ‘nitainyima

kura CCM kwa sababu ya mgao wa umeme.’

Wakati wa kampeni za kuwania urais mwaka 2005, moja ya ahadi za CCM na Kikwete

ilikuwa kuzalisha ajira milioni mbili. Kama lengo hilo lilifikiwa au la, tafsiri ya mtaani ilikuwa

kama kuzalishwa kwa ‘ajira’ nyingi za uhalifu kuliko ‘ajira halali.’ Kulikuwa na ongezeko la

idadi ya waliojiingiza katika siasa na kugeuka mamilionea kutokana na marupurupu makubwa

kwenye ubunge, ongezeko la ‘wauza unga,’ majangili, mafisadi, na wahalifu wengine kwa

ujumla. Ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira ulipelekea uhalifu kuwa kama ‘ajira halali’ na

njia halali ya kutengeneza kipato.

Uchaguzi mkuu huo utabaki kwenye kumbukumbu kama uliohusisha matumizi makubwa ya

teknolojia, hususan mitandao ya kijamii. Wakati maendeleo hayo yalitoa fursa sawa kwa CCM

na UKAWA, ilitarajiwa kuwa umoja huo wa Wapinzani ungeweza kunufaika zaidi kwa sababu

mitandao hiyo ya kijamii inatumika kama nyenzo muhimu ya mawasiliano kati ya viongozi na

wanachama, na miongoni mwa wanachama, na hivyo kukabiliana na kikwazo cha vyombo vya

habari vya umma kuelemea CCM.

Hata hivyo, pengine kwa kujiamini kuwa walikuwa na fursa kubwa kuishinda CCM, na

kudhani umaarufu wa mgombea wao, Lowassa, ungejinadi wenyewe na hatimaye kumudu

kumshinda mpinzani wake, Dokta Magufuli, wana-UKAWA hawakuitumia ipasavyo mitandao

ya kijamii kulinganisha na wana-CCM.

Kadhalika, wakati kabla ya uchaguzi huo, CCM na wafuasi wake ilikuwa ikilaumiwa na

wapinzani kuwa ‘ilipendelea kutumia vitisho au lugha kali kila ilipohojiwa kuhusu tuhuma

mbalimbali,’kampeni za uchaguzi huo zilishuhudia kinyume cha hali hiyo, ambapo wengi wa

wafuasi na baadhi ya viongozi wa UKAWA waligeuka hodari wa matusi na kumwandama kila

mtu aliyejaribu kuibua maswali halali kuhusu sera zao, Lowassa, nk.

Page 28: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

CCM ilifanikiwa mno katika matumizi ya mitandao ya kijamii kwenye kampeni zao,

ambapo kwa kiasi kikubwa walielemea zaidi kumnadi mgombea wao Dokta Magufuli na

wagombea ubunge, tofauti na UKAWA walionekana sio tu kujiamini kwa kutomnadi Lowassa

vya kutosha bali ‘kuwekeza’ zaidi kwenye matusi huku wakisahau wagombea wao wa ubunge na

udiwani.

Changamoto nyingine kwa Dokta Magufuli na CCM ilikuwa kile Waingereza wanaita

‘guilty by association,’ yaani kuhusishwa na kosa kutokana na kuhusiana na mtenda kosa. Katika

hilo, utawala wa CCM ulibebeshwa lawama za ubadhirifu mkubwa uliofanywa kwenye taasisi

mbalimbali, hususan vyama vya ushirka ambavyo baadhi ya viongozi wake walionekana kama

wakilindwa na chama hicho tawala, hususan kutokana na michango yao ya fedha kwa chama

hicho. Tatizo la ubadhirifu katika vyama vya ushirika sio tu liliwaathiri sana wakulima vijijini

bali pia lilikuwa na athari kwa uchumi wa taifa letu ambalo linategemea kilimo kama uti wa

mgongo. Vyama vingi vya ushirika vilionekana huko vijijini kama taasisi za CCM, na ilikuwa

rahisi makosa yaliyofanywa na vyama hivyo kuhusishwa na chama hicho tawala.

Licha ya vyama vya ushirika, uendeshaji wa serikali za mitaa ulikuwa umegubikwa na

tuhuma mbalimbali za ufisadi, sambamba na watendaji wa serikali hizo kujiona kama miungu-

watu, na kutokuwa na msaada wa kutosha kwa wananchi. Chuki za wananchi dhidi ya watendaji

wa serikali za mitaa wenye tuhuma za ubadhirifu au wasio na utendaji kazi bora zilionekana

kuwa zingeweza kuiathiri CCM pia, hasa ikizingatiwa kuwa ni vigumu kuchora mstari

unaotenganisha chama hicho tawala na serikali za mitaa.

Tatizo la umungu-mtu lilikuwepo pia ndani ya CCM yenyewe na katika serikali zake. Kwa

upande mmoja tatizo hili lilichangiwa na ufisadi ambapo ‘jeuri ya fedha’ iliwapa kiburi

watendaji wakiamini kuwa fedha walizonazo ni kinga dhidi ya kuchukuliwa hatua. Kwa upande

mwingine, utoaji ajira kwa misingi ya undugu au urafiki uliwajengea kiburi baadhi ya watendaji

wanaoamini kuwa hata wakiboronga ‘watalindwa na aliyewaweka hapo.’ Sababu kama hizi

zilihisiwa kuwa zingeweza kuwafanya baadhi ya wapigakura waamue ‘kufanya majaribio kwa

utawala wa UKAWA’ hasa kutokana na kutapakaa kwa hisia kuwa ni vigumu kwa CCM

kupambana na mengi ya matatizo yanayoikabili yenyewe kama chama, na nchi kwa ujumla.

Umungu-mtu na viongozi kuwa mbali na wananchi pia ulikuwa matokeo ya mfumo

uliorithiwa kutoka zama za chama kimoja. Wakati huo, kauli ya kiongozi ilikuwa kama ‘amri ya

mungu,’ ni sahihi na isiyoweza kupingwa. Ujio wa mfumo wa vyama vingi haukufanikiwa

kuondoa kasumba hiyo, ambayo pia ilichangia viongozi kutofahamu fika matatizo ya wananchi

kutokana na kutokuwa karibu nao.

Kadhalika, mabadiliko yaliyoitoa CCM kutoka ‘chama cha wakulima na wafanyakazi’ na

kuwa ‘chama cha wafanyabiashara na wasomi’ yalionekana kuwa yageaweza kutoa fursa kwa

vyama vya upinzani, hususan UKAWA, kuwaunganisha ‘wakulima na wafanyakazi

waliotelekezwa na CCM,’ na kupata kura kutoka kwa makundi hayo mawili yenye asilimia

kubwa ya Watanzania.

Ukweli kwamba huo ulikuwa uchaguzi mkuu wa kwanza kwa CCM kukumbana na

muungano imara wa upinzani, ulioongozwa na Lowassa, mwanasiasa aliyekuwa na nguvu

kubwa alipokuwa ndani ya CCM, ulitarajiwa ungeweza kukifanya chama hicho tawala kisijue

jinsi ya kuukabili upinzani huo ‘wa aina mpya.’ Kwa kiasi fulani, ushindi wa CCM dhidi ya

vyama vya upinzani katika chaguzi mbalimbali huko nyuma ulichangiwa na mazingira ya

‘chama kikongwe na imara’ kuchuana na upinzani dhaifu na uliogawanyika. Ilidhaniwa kuwa

mbinu zilizotumiwa na CCM katika chaguzi za mwaka 1995, 2000, 2005 na 2010 zisingeweza

Page 29: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kufanikiwa kwenye uchaguzi wa mwaka huo kutokana ushirikiano wa vyama vya upinzani

vilivyounda UKAWA.

Lakini kwa upande mwingine, ilidhaniwa kuwa mazowea ya kushinda kila uchaguzi mkuu

yangeweza kuijengea CCM hali ya kujiamini kupita kiasi, na hivyo kuzembea, na kutoa fursa

kwa UKAWA kushinda uchaguzi huo.

Licha ya tuhuma za mara kwa mara za ufisadi zilizouandama utawala wa Kikwete, moja ya

matatizo yaliwagusa wengi ni ombwe la uongozi wa taifa. Wakati Wapinzani walimtuhumu Rais

Kikwete kuwa ni dhaifu, wananchi wengi walimwona kama ‘mpole kupita kiasi,’ japo wakati

anaingia madarakani kwa mara ya kwanza, mwaka 2005 alitahadharisha kuwa ‘tabasamu lake

lisieleweke vibaya.’ Ombwe hilo la uongozi ambalo lilijitokeza mara baada ya Nyerere kustaafu

na hatimaye kufariki, lilizidi kukua, awamu moja baada ya nyingine. Kuna nyakati ambapo nchi

ilionekana kama ‘inajiendesha kwa auto-pilot,’ aidha kwa vile Rais alikuwa kwenye safari zake

mfululizo nje ya nchi au watendaji wa serikali walikuwa ‘wamebanwa na jukumu la kuvuna

shamba la bibi, kula keki ya taifa,’ yaani kufanya ufisadi. Ilitarajiwa kuwa UKAWA wangeweza

kunufaika katika hili iwapo wangemudu kuonyesha mlolongo wa kukua kwa ombwe la uongozi,

na kujenga hisia kuwa CCM ikishinda itaendeleza ombwe hilo badala ya kuliondoa.

Hata hivyo, licha ya changamoto hizo zote kwa Dokta Magufuli na CCM kwa ujumla,

mpinzani wake, Lowassa, na UKAWA walioshindwa kabisa kulishawishi kundi muhimu la

wapigakura – wasiofungamana na chama chochote – ambalo yayumkinika kuamini kuwa ndilo

lililomwezesha Dokta Magufuli na CCM kushinda uchaguzi huo uliojaa ushindani mkubwa.

Kama kuna kitu kilichomwangusha sana Lowassa, na UKAWA kwa ujumla, katika

uchaguzi huo ni viongozi na wafuasi wake kujiamini kupita kiasi. Kujiamini huko kuliandamana

na jeuri ya aina flani, ambapo viongozi na wafuasi hao hawakutaka kusikia ushauri wowote hata

kama ulikuwa wa manufaa kwao.

Kujiamini huko ‘kulikopitiliza’ kulichangiwa na sababu kuu mbili. Kwanza, umaarufu wa

Lowassa kabla hajajiunga na Upinzani. Ni kweli kwamba hadi wakati anajiondoa CCM,

mwanasiasa huyo alikuwa maarufu kuliko yeyote yule ndani ya chama hicho tawala. Hata hivyo,

UKAWA walipotoka kudhani kuwa umaarufu wa Lowassa akiwa CCM ungeendelea baada ya

kuhamia Upinzani. Hilo lilithibitika katika ukweli kwamba ahadi kuwa ‘mamia ya viongozi wa

CCM wangemfuata Lowassa huko UKAWA’ iliisha kuwa porojo tu. Makada waliomfuata huko

Upinzani hawakuwa na nguvu ya kutosha kuiyumbisha CCM au kuiimarisha UKAWA.

Sababu ya pili, ni imani potofu kuwa ‘CCM ilikuwa inachukiwa mno’ kiasi kwamba

wapigakura wangemchagua Lowassa hata asingejinadi vya kutosha. Na kwa hakika, kampeni ya

Lowassa ilikuwa kama mzaha mbaya kwenye uchaguzi. Licha ya hotuba zake kuwa fupi mno,

alishindwa kabisa kuelezea kaulimbiu yake kuu ya ‘mabadiliko.’ Wakati kwa hakika Watanzania

wengi walikuwa wakihitaji mabadiliko, lakini ilihitajika zaidi ya maneno matupu jukwaani

kuwaaminisha wananchi kuwa watu walewale kama Lowassa na Sumaye walioitwa mafisadi na

wapinzani haohao wanaowanadi, wangeweza kweli kuleta mabadiliko waliyohubiri.

Kwa kuhitimisha, sura hii imejadili changamoto mbalimbali zilizomkabili Dokta Magufuli

na chama chake katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Kama sura hii na

iliyotangulia zinavyoonyesha, uchapakazi wa Dokta Magufuli ulikuwa turufu muhimu kwake na

kwa CCM pia. Alikuwa mgombea ambaye ‘anauzika’ kirahisi licha ya ukweli kwamba chama

chake kiliwekeza nguvu kubwa kumnadi. Lakini kama kanuni za kisiasa zinavyotanabaisha,

uimara wa mgombea hutegemea udhaifu wa mpinzani wake. Na kwa bahati nzuri, mpinzani

mkuu wa Dokta Magufuli, yaani Lowassa, alikuwa mgombea dhaifu aliyekuzwa na sifa za

kufikirika ambazo ziliishia kumuumbua wakati wa kampeni. Kimsingi, ushindani kati ya Dokta

Page 30: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Magufuli na Lowassa aulikuwa kati ya mwanasiasa ‘msafi’ anayesifika kwa uchapakazi dhidi ya

mwanasiasa aliyesifika zaidi kwa tuhuma za ufisadi, zilizopelekea kujiuzulu Uwaziri Mkuu

mwaka 2008.

Kana kwamba ubora huo wa Dokta Magufuli dhidi ya udhaifu wa Lowassa ulikuwa

hautoshi, ukweli kwamba Chadema, chama kilichompokea Lowassa na kumfanya mgombea

wake wa urais kwa tiketi ya UKAWA, kilikuwa mstari wa mbele kwa takriban miaka 9

kumwandama Lowassa kwa kumuita fisadi sugu, ulitosha kabisa kuwarahisishia maamuzi

wapigakura kuhusu mgombea gani ni sahihi kwao.

Usaliti wa Chadema ulionekana pia katika jinsi ‘ilivyomtenda’ aliyekuwa Katibu wake

Mkuu, na mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Dokta Willbrord

Slaa. Baada ya kujiweka kando kwa takriban mwezi mzima mara baada ya Lowassa kujiunga na

Chadema, Dokta Slaa alijitokeza hadharani na kueleza sababu zilizopelekea yeye kutoafikiana na

uamuzi wa chama chake kumpitisha Lowassa kuwa mgombea wake wa urais. Pamoja na mambo

mengine, Dokta Slaa alielezea bayana kuwa kada huyo wa zamani wa CCM aliihadaa Chadema

kwa kuahidi kuwa idadi kubwa ya viongozi wa chama chake cha zamani wangejiunga na chama

hicho, na hivyo kuiongezea uwezekano wa kuiangusha CCM. Dokta Slaa, ambaye alikuwa na

mchango mkubwa katika kuiimarisha Chadema na kuifanya ionekane mtetezi wa wanyonge

hususan dhidi ya ufisadi, alihitimisha kuwa Lowassa alikuwa ni ‘liability’ na sio ‘asset’ kwa

Chadema na UKAWA, kitu ambacho hatimaye kilithibitika baada ya matokeo ya uchaguzi huo

kutangazwa.

Hatua hiyo ya Dokta Slaa kujitokeza hadharani kueleza kilichojiri hadi akajiweka kando

ilipelekea viongozi wakuu wa Chadema na wafuasi wao kumwandama na kumdhalilisha kwa

kiasi kikubwa, huku wakimtuhumu kuwa alinunuliwa na CCM ili kumkwamisha Lowassa. Kosa

walilofanya Chadema, na pengine UKAWA kwa ujumla ni kupuuzia umuhimu wa Dokta Slaa

katika siasa za upinzani nchini Tanzania. Kutokana na umakini wake na msimamo wake

usioyumba, uamuzi wake wa kutangaza hadharani ‘usaliti wa Chadema’ ulikuwa na athari

kubwa kwa chama hicho kikuu cha upinzani, na umoja wa UKAWA kwa ujumla. Katika

mazingira ya kawaida tu, mwanasiasa anayeheshimika kitaifa anapokikosoa chama chake

hadharani hususan wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu, inaweza kukigharimu chama husika.

Kwa upande mwingine, kosa la msingi walilofanya Chadema na UKAWA kwa ujumla

kumpitisha Lowassa kuwa mgombea wao wa kiti cha urais ni ukweli kwamba ni miujiza pekee

ingeweza ‘kumsafisha’ Lowassa ndani ya miezi mitatu, ilhali wapinzani haohao waliojitwisha

kibarua cha kumsafisha ndio waliokuwa mstari wa mbele kwa miaka tisa mfululizo ‘kumchafua.’

Suala jingine la muhimu kuhusu uchaguzi huo lililkuwa nafasi ya utafiti wa kura za maoni

(opinion polls). Baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, taratibu tafiti za kura za

maoni zilianza kujichomoza, lakini zilikabiliwa na upinzani mkali kwa madai ya kukibeba

chama tawala. Iwapo madai hayo yalikuwa na ukweli au la, suala lililojitokeza wazi ni kuwa

wananchi wengi hawakutilia maanani matokeo ya tafiti hizo, pengine kutokana na hisia za

upendeleo kwa chama tawala au ugeni tu wa utaratibu huo.

Katika uchaguzi huo kulifanyika tafiti tatu za kura za maoni. Katika tafiti hizo, ya taasisi za

Twaweza, IPSOS (Synovate) na TADIP, mbili zilionyesha CCM na mgombea wake anaongoza

kwa mbali huku tafiti ya tatu ikionyesha mgombea wa UKAWA akiongoza.

Katika utafiti wa kura za maoni wa Twaweza, Magufuli aliongoza kwa asilimia 65 ilhali

Lowassa akipata asilimia 25, na katika utafiti wa IPSOS (Synovate) Magufuli alipata asilimia 62

na Lowassa asilimia 31, huku utafiti wa kura za maoni wa taasisi ya TADIP ukionyesha Lowassa

akipata asilimia 54 dhidi ya asilimia 40 kwa Magufuli.

Page 31: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Tafiti zote hizo za kura za maoni zilishutumiwa vikali, huku mbili zilizoonyesha Magufuli

akiongoza zikituhumiwa kuwa ‘zilipikwa na CCM,’ ilhali ule ulioonyesha Lowassa anaongoza

ukilaumiwa kwa madai kuwa taasisi iliyofanywa utafiti huo ilikuwa inamilikiwa na Chadema.

Matokeo ya uchaguzi huo yalipotangazwa, yaliakisi kwa kiasi kikubwa matokeo ya utafiti

wa kura za maoni wa Twaweza na IPSOS (Synovate). Katika matokeo hayo, Dokta Magufuli

alipata jumla ya kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46 ya kura 15,589,639 huku Lowassa

akiambulia kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.

Kwa mujibu wa takwimu, takriban Watanzania milioni 23,161,440 walijiandikisha kupiga

kura katika uchaguzi huo. Kwa kuzingatia kwamba idadi kubwa ya wapigakura hao sio

wanachama wa chama chochote cha siasa, yayumkinika kuhitimisha kuwa ushindi kwa Magufuli

na CCM au Lowassa na UKAWA ungeamuliwa na kundi hilo. Kimahesabu, takwimu

zilizokuwepo zilionyesha kuwa idadi ya jumla ya wanachama wa CCM ni milioni 8 hivi, ambao

ni sawa na takriban asilimia 34.5 ya jumla ya Watanzania waliojiandikisha kupiga kura. Kwa

makadirio, idadi ya jumla ya wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA ni pungufu ya hao

wa CCM, na hiyo ingeweza kufanya kundi la wapigakura wasiofungamana na chama chochote

kuwa zaidi ya asilimia 50.

Kilichoupa uzito zaidi kundi hilo la wapigakura wasiofungamana na upande wowote ni

ukweli kwamba lingeweza kuwa kubwa zaidi kutokana na mabadiliko yaliyojitokeza ndani ya

CCM na UKAWA kabla ya uchaguzi. Kwa upande wa CCM, kuondoka kwa Lowassa

kungeweza kuwafanya baadhi ya wana-CCM kutoiunga mkono CCM lakini bila kuchukua

uanachama huko UKAWA. Hawa wangeweza kuingia katika kundi hilo la ‘wasioungamana na

chama chochote,’ licha ya kuendelea kuwa wana-CCM.

Kwa upande wa UKAWA, ilihisiwa kuwa kuna baadhi ya wanachama wa vyama

vilivyounda umoja huo ambao sio tu hawakuridhishwa na suala la ushirikiano wa vyama hivyo,

lakini pia wale ambao walichukizwa na ujio wa Lowassa, au kukerwa na sababu zilizopelekea

Prof Ibrahim Lipumba (mwenyekiti za zamani wa CUF) na Dkt Slaa kujiengua katika uongozi.

Katika hawa, ilidhaniwa kuna ambao wangeweza kuamua kujiunga na CCM, lakini uwezekano

mkubwa ulikuwa ni kwa wengi wao kubaki wanachama wa vyama hivyo lakini wasiounga

mkono ugombea wa Lowassa. Kwahiyo nao wangeweza kuingizwa katika kundi la

‘wasiofungamana na chama chochote,’ licha ya kuendelea kuwa wananchama katika vyama

vyao.

Hadi kufikia hatua ya kuhitimisha toleo la kwanza la kitabu hiki, ambalo lilichapishwa

takriban wiki mbili kabla ya uchaguzi huo, mimi kama mwandishi nilisimamia kwenye kufanya

uchambuzi bila kuelemea upande wowote. Nilijitahidi kuelezea mapungufu ya pande zote mbili,

sambamba na fursa walizonazo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Nilifanya hivyo kwa

sababu lengo la kuandika toleo hilo halikuwa kufanya simulizi, au kukampenia chama au

mgombea fulani bali kuweka kumbukumbu sawia, pamoja na kuwasaidia wasomaji kufanya

maamuzi sahihi wakati wa kupiga kura.

Na uamuzi wa kuvizungumzia vyama viwili tu, yaani CCM na UKAWA (kama muungano

wa vyama) ulitokana na ukweli kuwa kwa vyovyote vile, mshindi katika kiti cha urais angekuwa

aidha Dokta Magufuli au Lowassa, huku ushindi kwa upande wa vyama kwa jumla kingekuwa

aidha CCM au UKAWA katika umoja wao. Kwahiyo, ilionekana bayana kuwa hatma ya

Tanzania ilikuwa mikononi mwa Magufuli na CCM yake na Lowassa na UKAWA yake, na

hivyo kulazimika kuwajadili wagombea hao na vyama hivyo.

Hata hivyo, na bila kupendelea upande wowote, nilibainisha bayana kuwa mazingira

yaliyokuwepo yaliipa nafasi kubwa CCM na mgombea wake Dokta Magufuli kuibuka mshindi

Page 32: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

katika uchaguzi huo. Nilielezea sababu kadhaa ambazo zingezoweza kuisadia CCM na Dokta

Magufuli kushinda. Na nilifanya hivyo pia kwa UKAWA na Lowassa. Kwa kukilinganisha fursa

na vikwazo kwa kila upande haikuwa ngumu kubashiri ushindi kwa CCM na Dokta Magufuli.

Nilieleza pia kwamba ushindi kwa CCM na mgombea wake ungeweza kutokana zaidi na

nilichokiita ‘sababu za kimfumo,’ kwamba mfumo uliokuwepo katika kipindi cha kuelekea

uchaguzi ulimtengenezea mazingira mazuri Dokta Magufuli na chama chake, ilhali ushindi kwa

Lowassa na UKAWA ulitegemea zaidi mapungufu ya CCM, sio tu katika kujinadi bali pia

kupata mwanya wa kuwashawishi wapigakura wengi zaidi katika kundi muhimu la

‘wasiofungamana na chama chochote,’ ambalo niliamini kuwa lingeamua mshindi katika

uchaguzi huo.

Nilieleza pia kuwa kwa vile ‘wapigakura wasiofungamana na chama chochote’ ndio

wangeamua mshindi katika uchaguzi huo, ilikuwa rahisi zaidi kwao kumwamini Dokta Magufuli

kutokana na rekodi yake, kuliko Lowassa. Kwa kuwalinganisha wagombea hao wawili, Dokta

Magufuli angeweza na aliweza kutembea ‘kifua mbele’ kuonyesha mafanikio ya utendaji kazi

wake, kubwa zaidi likiwa kumudu kutumikia awamu mbili tofauti kwa ufanisi mkubwa. Hali

ilikuwa tofauti kwa Lowassa, kwa sababu vyovyote ilivyokuwa, tuhuma dhidi yake kuhusu

kashfa ya Richmond sio tu ilikuwa vigumu kufutika bali pia ilikuwa sio rahisi kwa Chadema na

UKAWA kwa ujumla kumsafisha mwanasiasa huyo ndani ya miezi matatu ilhali walitumia

takriban miaka tisa ‘kumchafua.’

Kibaya zaidi, wakati Dokta Magufuli aliungwa mkono na takribani wana-CCM wote,

tukiweka kando waliojiweka kando kutokana na jina la Lowassa kukatwa na vikao vya mchujo

vya chama hicho, na baadaye kukihama chama hicho tawala, Lowassa hata kama angeungwa

mkono na asilimia kubwa ya wana-UKAWA, wengi wa hao waliomuunga mkono walitumia

muda mrefu huko nyuma ‘kumchafua’.

Hoja hapa ni kwamba, wakati waliomuunga mkono Dokta Magufuli ni watu ‘waliomuunga

mkono muda wote,’ kwa maana ya ufuasi wao kwa CCM, kwa upande wa Lowassa, wengi wa

waliomuunga mkono ni ‘watu wapya,’ ambao huko nyuma walifanya kila jitihada ‘kumchafua.’

Ilikuwa rahisi kwa kundi la ‘wapigakura wasiofungamana na chama chochote’ kushawishiwa na

‘waliomuunga mkono Magufuli tangu mwanzo’ kuliko hao ‘waliomuunga mkono Lowassa muda

huo lakini huko nyuma walimbomoa.’

Kimsingi, CCM haikuhitaji kuwashawishi wanachama wake kumuunga mkono Dokta

Magufuli, kwa sababu alikuwa ‘mwenzao.’ Kwa upande wa Lowassa, sio tu zilihitajika jitihada

za kuwashawishi baadhi ya wana-UKAWA kuwa ‘actually tulikosea kumwita huyu mtu fisadi,’

lakini pia kuwaaminisha kuwa ‘atasimama nao hadi dakika ya mwisho,’ kwa kuzingatia hofu

kwamba ‘huenda Lowassa ametumwa na CCM ili kuuwa upinzani.’

Ndio, ilikuwa rahisi kwa UKAWA kudai kuwa ‘fisadi pekee hakuwa Lowassa tu, na ufisadi

CCM haukuwa Richmond pekee,’ lakini kwa upande mwingine, ukiangalia watu waliotajwa

kuwa karibu na Lowassa na wale walio karibu na Dokta Magufuli, mpigakura ‘asiyefungamana

na chama chochote’ angeweza kushawishika kirahisi kumchagua mgombea huyo wa CCM

kuliko Lowassa, kwa sababu wengi wa ‘waliomzunguka Lowassa,’ waliomfuata kutoka CCM na

baadhi ya waliotajwa kumuunga mkono bila kujitangaza hadharani, walikuwa watu wenye

rekodi zisizopendeza. Hili liliweza kujenga hofu kwamba, laiti mgombea huyo wa UKAWA

angeshinda, angeweza kuwawekea kando ‘wenye vyama vyao,’ na kuwateua ‘maswahiba zake’

waliotajwa kumsaidia katika kampeni zake.

Kwenye suala la mgombea gani kati ya Lowassa na Dokta Magufuli alikuwa na nafasi ya

kuleta mabadiliko halisi ndani ya chama chake na kwa taifa kwa ujumla, ilionekana kuwa

Page 33: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

ingekuwa rahisi kwa Dokta Magufuli angalau kuahidi hilo kwa sababu kimsingi tatizo la CCM

lilikuwa ukosefu tu wa nia ya kufanya mabadiliko kusudiwa, kwani uwezo na sababu

zilikuwepo. Kwa upande wa Lowassa, hiyo tu kuamini kwamba kuwa hivi sasa yeye ni mtu

tofauti na yule aliyekuwa CCM ilikuwa ‘mtihani’ tosha.

Lakini kingine, Lowassa alishindwa kabisa kuelezea kwa undani kuhusu ajenda yake ya

mabadiliko, hali iliyopelekea hisia kuwa huenda yeye mwenyewe hakuamini katika mabadiliko

aliyohubiri. Kimsingi, mabadiliko yaliyotarajiwa na Watanzania, hususan wafuasi wa UKAWA,

sio jambo jepesi kama lilivyozungumzwa majukwaani.

Ingekuwa sio jambo la faida kwa wapigakura na Watanzania kwa ujumla pekee bali

lingeweza kumsaidia Lowassa na UKAWA endapo dhana hiyo ya mabadiliko ingefafanuliwa

kwa upana zaidi. Kwa mfano, mgombea huyo angeweza kueleza kuhusu ratiba ya mabadiliko

hayo, sambamba na kutanabaisha ni maeneo yapi yatakayoanza kushughulikiwa. Orodha ya

maeneo yaliyopaswa kukumbwa na mabadiliko hayo ni ndefu, na pasipo mipango ya kueleweka,

basi hata Lowassa angeshinda katika uchaguzi huu, angeweza kumaliza vipindi viwili vya urais

pasipo kutimiza ahadi ya kuleta mabadiliko.

Kulikuwa na haja kwa Lowassa na UKAWA kwa ujumla kujifunza kutoka katika ahadi ya

Kikwete wakati wa kampeni zake kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 ambapo alitoa

ahadi ya ‘jumla jumla’ ya ‘Maisha Bora kwa Kila Mtanzania.’ Japo ‘maisha bora’ ni rahisi

kuchanganuliwa kuliko ‘mabadiliko,’ kwa kiasi kikubwa Kikwete alimaliza mihula yake miwili

huku wananchi wengi wakidhani ahadi hiyo ya maisha bora ilikuwa ‘hadaa’ tu. Hata hivyo,

tatizo lililoifanya ahadi hiyo kutoonekana kama imetekelezwa ni kutokana na ‘ujumla jumla’

wake.

Kwa kuhubiri mabadiliko pasipo kuelezea kwa undani, ilihisiwa kuwa ‘urais wa Lowassa’

ungekumbwa na matatizo mapema kutoka kwa wananchi ambao wangekuwa wakitarajia, kwa

mfano, mara baada ya mwanasiasa huyo kuingiza Ikulu, kila mwananchi angeweza kujimudu

kiuchumi, ajira zingepatikana mara moja kwa wasio na ajira, na matarajio mengine lukuki. Si

kwamba wazo la mabadiliko lilikuwa baya au lisilohitajika bali lilistahili kutolewa maelezo ya

kina hususan mipango na ratiba thabiti ya utekelezwaji wake.

Lakini hata kama ingekuwa rahisi kwa Lowassa kueleza kuhusu ajenda ya mabadiliko kwa

upande wa kiutawala au sera, kikwazo kingeweza kuwa upande wa mabadiliko kijamii. Kwa

mfano, mwanasiasa huyo angepaswa kueleza ana mkakati gani ya kubadili kasumba iliyoota

mizizi katika nchi yetu ya ‘kuwapa wahalifu heshima wasiyostahili’? Ilikuwa jambo la kawaida

katika maeneo mengi ya Tanzania yetu kuona muuza madawa ya kulevya akitukuzwa na kupewa

‘wadhifa’ wa ‘mzungu wa unga’ badala ya kuitwa mhalifu. Kadhalika, ilizoeleka kuona

wabadhirifu makazini wakipewa ‘wadhifa’ wa ‘mapedejee.’

Licha ya tabia hizo, kuna masuala yanayopewa uzito mkubwa katika jamii ilhali yale ya

muhimu yakipuuzwa. Kwa mfano, watu wapo tayari kuchangia mamilioni ya shilingi kama

michango ya harusi lakini wanashindwa kuchangiana ada za watoto wao mashuleni. Laiti

ushirikiano unaoonyeshwa kwenye klabu za starehe, kile wenyewe wanaita ‘kuzungusha raundi

za kinywaji’ ungehamishiwa kwenye ushirika kwenye miradi ya maendeleo, basi pengine

mabadiliko yaliyohubiriwa na Lowassa yangekuwa yameanza kitambo.

Kuna tatizo la vijana wengi kutafuta njia za mkato za mafanikio, hali inayowavutia matapeli

kubuni miradi mbalimbali ya ‘kula fedha za bure.’ Ni watu wangapi waliopoteza fedha zao

katika ‘miradi ya kitapeli’ kama vile ‘Dollar Jet,’ ‘DECI,’ na mingineyo?

Licha ya miradi ya kitapeli wa utajiri wa ‘chapu chapu,’ kuna imani katika vitu visivyo na

mwelekeo kama ilivyokuwa katika suala la ‘kikombe cha babu,’ mtumishi wa Kanisa huko

Page 34: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Samunge, mkoani Arusha aliyeahidi tiba ya magonjwa mbalimbali, na kupelekea maelfu kwa

maelfu ya Watanzania kujazana huko. Hadi leo idadi ya waliopoteza maisha kwa kuamini ‘tiba

ya kikombe cha babu’ haijawekwa hadharani lakini yayumkinika kuhisi kuwa ni kubwa.

Kuna tatizo kubwa la imani za ushirikina ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi

zinazoongoza duniani kwa imani hiyo. Je mabadiliko ya kisera yanaweza kuwafanya waamini

wa ushirikina wabadilike? Licha ya ushirikina, kuna vijana lukuki wanaoamini kuwa njia ya

mkato ya mafanikio ni kujiunga na kikundi cha ‘Freemasons,’ huku takriban kila kijana

anyejituma na kufanikiwa kimaisha akihisiwa kuwa mfuasi wa kundi hilo. Kibaya zaidi, ilifika

mahala baadhi ya vijana kujizushia kuwa wao ni freemasons ili ‘waonekane kuwa wanakaribia

kupata utajiri punde.’

Kama kuna eneo linalohitaji mabadiliko ya haraka ni katika suala la rushwa. Utafiti mmoja

uliofanyika mkoani Arusha ulionyesha kuwa zaidi ya asilimia 50 ya waliohojiwa waliamini

kuwa ‘rushwa ilikuwepo, ipo na itaendela kuwepo milele.’ Sawa, rushwa ilikuwepo kitambo na

itaendelea kuwepo lakini si kwa kiwango kilichokuwepo wakati huo. Na uwepo wake wa muda

mrefu haukumaanisha wananchi wakubaliane nayo, kwani hata maradhi kama malaria na ukimwi

yamekuwapo kitambo lakini jitihada za kupambana nayo zinaendelea.

Kwahiyo, ajenda ya Lowassa kuhusu mabadiliko, licha ya uzuri wake, licha ya kuwa na

mkanganyiko mkubwa, haikupatiwa maelezo ya kutosha. Na ni katika mazingira haya,

waliomlaumu Lowassa kuhusu ‘hotuba zake za dakika chache’ walipata uzito katika lawama

hizo kwa sababu kuna masuala kadhaa yaliyohitaji kuelezwa kwa kirefu, kubwa likiwa ni hilo la

ajenda ya mabadiliko.

Katika kuhitimisha toleo la kwanza la kitabu hiki, nilieleza bayana ugumu wa kufanya

ubashiri wa uhakika kuwa nani kati ya Dokta Magufuli na Lowassa angeibuka mshindi. Hata

hivyo, ‘nilijifunga kitanzi’ kwa kueleza waziwazi kuwa mazingira yaliyokuwepo muda huo

yaliashiria kuwa mgombea huyo wa CCM na chama chake walikuwa na nafasi kubwa ya

ushindi. Nilikumbushia kuwa japo kulikuwa kuna idadi kubwa ya Watanzania waliochoshwa na

CCM lakini kuchoshwa pekee hakutoshi kukiondoa chama madarakani. Na kama alivyosema

Dkt Slaa wakati anatoa maelezo kuhusu kujitenga kwake na Chadema, mabadiliko ya kweli

yanahitaji mikakati makini ya watu makini. Na kwa kiasi kikubwa tu, si Lowassa wala UKAWA

waliokuwa watu makini wenye mikakati makini kuleta mabadiliko waliyoyahubiri.

Page 35: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Nne

Urais wa Dokta Magufuli na utekelezaji wa ‘Hapa ni Kazi Tu’: Siku moja tu baada ya kuapishwa

kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta Magufuli alionyesha dalili

kuwa kaulimbiu yake ya ‘Hapa Ni Kazi Tu’ haikuwa porojo. Badala ya kutumia siku ya kwanza

ofisini kwake Ikulu, Rais alifanya ziara ya kushtukiza katika Wizara ya Fedha, na alitembea kwa

miguu.

Siku nne baadaye, Dokta Magufuli alifanya tena ziara ya kushtukiza, safari hii katika

Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambako alishuhudia utoaji mbovu wa huduma na kuchukua

uamuzi wa kuvunja bodi ya hospitali hiyo na kumtimua kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu.

Kadhalika, Rais aliagiza mashine za vipimo vya CT-Scan na MRI zitengenezwe haraka.

Akiwa madarakani ndani ya wiki tatu tu, Dokta Magufuli alichukua hatua kadhaa za kubana

matumizi yasiyo ya lazima. Hatua hizo ni pamoja na kufuta safari zote za nje kwa watumishi wa

serikali isipokuwa kwa kibali maalum kutoka kwake au Katibu Mkuu Kiongozi. Uamuzi huo wa

kufuta safari za nje ulipelekea kufutwa kwa majina 50 ya watumishi wa serikali waliotakiwa

kuhudhuria Mkutano wa Nchi za Jumuiya ya Madola, na kuwabakiza wanne tu, hatua iliyookoa

takriban shilingi bilioni 700.

Kadhalika, mara baada ya kuzindua Bunge, Rais aliamua kuwa shilingi milioni 225

zilizochangwa kwa ajili ya sherehe ya uzndizu wa bunge hilo zitumike kununulia vitanda kwa

ajili ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Akionyesha dhamira ya dhati ya kubana matumizi, Dokta Magufuli alifuta sherehe za

maadhimisho ya miaka 54 ya uhuru na badala yake akaagiza sherehe hizo ziazimishwe kwa

kufanya usafi wa mazingira nchi nzima. Uamuzi huo wa kufuta sherehe za uhuru uliokoa shilingi

bilioni 4, ambazo Rais aliagiza zielekezwe kwenye matengenezo ya Barabara ya Morocco, jijini

Dar es Salaam.

Historia ya utendaji kazi wa Dokta Magufuli yaonyesha kuwa ni mtu wa vitendo zaidi

kuliko maneno. Hata hivyo, historia pia yaonyesha kuwa anapoongea, maneno yake huwagusa

wengi. Na katika kuthibitisha hilo, hotuba aliyoitoa wakati anazindua Bunge inabaki kuwa moja

ya hotuba za kihistoria.

“Hotuba hii ya Rais Magufuli ni moja ya hotuba bora kabisa katika historia ya siasa za

Tanzania.” Hili lilikuwa hitimisho langu katika mtandao wa kijamii wa Twitter mara baada ya

hotuba hiyo.

Na kwa hakika watu kadhaa waliafikiana na hitimisho hilo. Kilichovutia wengi waliosikia

hotuba hiyo sio tu mpangilio wa hotuba yenyewe bali pia jinsi kila alilotamka lilivyoonyesha

bayana kuwa lilitoka moyoni mwake kwa dhati kabisa.

Rais alianza hotuba yake hiyo kwa kuorodhesha matatizo mbalimbali aliyobaini wakati wa

kampeni zake Urais ambapo alizunguka takriban Tanzania nzima. Alitoa uchambuzi wa kina wa

matatizo hayo kabla ya kuelezea kwa undani ni kwa jinsi gani serikali yake itayashughulikia.

Ilikuwa ni zaidi ya hotuba ya kisiasa, na pengine ingeweza kabisa kuwa mhadhara wa kitaaluma

uliofanyika katika lugha nyepesi na ya kueleweka.

Page 36: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Moja ya vitu vilivyovutia sana katika hotuba hiyo ni jinsi Rais Dokta Magufuli alivyoweza

kutoa jibu la swali ambalo kwa miaka kadhaa lilionekana kuwatatiza viongozi wetu mbalimbali:

“Kwanini Tanzania ni masikini licha ya utajiri lukuki wa raslimali ilionao.” Alieleza bayana na

kwa kirefu jinsi ufisadi, rushwa na uhalifu vilivyochangia kukwamisha maendeleo ya taifa letu.

Kadhalika, alifafanua, kwa kutumia takwimu halisi, jinsi mabilioni ya fedha yalivyotumika

visivyo kwa matumizi yasiyo muhimu na yaliyo nje ya uwezo wa taifa letu masikini.

Kwa hakika ilikuwa hotuba ya kihistoria iliyofunika kabisa utovu wa nidhamu wa hali ya

juu ulioonyeshwa awali na wabunge wa upinzani ambao walitumia muda mwingi kabla ya

hotuba hiyo kuzomea na baadaye kuamiriwa kutoka nje ya ukumbi huo.

Lakini kwa vile sio rahisi kumridhisha kila mtu, baadhi ya waliosikiliza hotuba hiyo walidai

kuwa eti “haina tofauti na hotuba nyingine kadhaa zilizokuwa nzuri kuzisikiliza lakini zikaishia

kuwa maneno matamu tu.” Wengine walikwenda mbali zaidi na kudai kuwa hata mtangulizi wa

Dokta Magufuli, yaani Rais Mstaafu Kikwete, naye pia alianza urais wake kwa hotuba za kutia

moyo kama hizo lakini mengi ya aliyoahidi, hususan lile la ‘Maisha Bora kwa Kila Mtanzania,’

yaliishia kuwa ahadi tu.

Sikukubaliana kabisa na wakosoaji hao, japo hoja zao zinaweza kuwa na mantiki kidogo. Ni

kweli kwamba ukosefu wa hotuba za kuvutia si moja ya matatizo yanayoikabili nchi yetu. Wengi

wa wanasiasa na viongozi wetu ni mahiri sana wa maneno lakini tatizo huwa katika kutafsiri

maneno yao kuwa vitendo.

Wakosoaji hao hawapo sahihi kwa sababu hotuba hiyo ilikuwa ya kutoka moyoni mwa

Dokta Magufuli, na haikuhitaji ‘sayansi ya roketi’ kubaini hilo. Ilikuwa hotuba ya kiongozi

anayeguswa na yanayoisibu nchi yake, kiongozi mwenye uelewa wa changamoto zinazoukabili

uongozi wake, na mwenye dhamira thabiti ya kukabiliana na changamoto hizo.

Kuna mbinu moja muhimu ya kubaini iwapo mtu anaongea ukweli au anahadaa, nayo ni

kumwangalia usoni. Tangu kuanza kwa kampeni zake za urais na hadi wakati wa hotuba hiyo

Bungeni, uso wa Dokta Magufuli wakati anaongea unaonyesha bayana kuwa kila neno linalotoka

mdomoni mwake ni la dhati, linatoka moyoni na si sehemu ya porojo tulilozowea kutoka kwa

wengi wa wanasiasa na viongozi wetu. Mtaalam yeyote wa kubaini ukweli na uongo

hatoshindwa kubaini uthabiti wa kauli za Dokta Magufuli upo wazi kwa yeyete anayemwangalia

usoni wakati anaongea.

Lakini pia, hotuba hiyo ilikuwa mwendelezo wa ishara nzuri zilizoanza kujitokeza siku moja

tu tangu Rais Magufuli aingie ofisini, ambapo alifanya ziara ya kushtukiza Wizara ya Fedha,

kabla ya kufanya ziara nyingine kama hiyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Na siku hiyo

ya uzinduzi wa Bunge, aliwakumbusha Watanzania enzi za (Waziri Mkuu wa zamani) hayati

Edward Sokoine, aliyesifika kwa uchungu wa mali za umma, baada ya kuamuru zaidi ya shilingi

milioni 200 zilizochangwa kwa ajili ya hafla ya mchapalo ya sherehe za uzinduzi wa Bunge

jipya zielekezwe kwenye ununuzi wa vitanda katika hospitali ya Muhimbili, na kiasi kidogo tu

kitumike kwa ajili ya hafla hiyo.

Kimahesabu, chini ya wiki tatu tangu aingie madarakani, Rais Magufuli aliokoa jumla ya

shilingi milioni 900 kutokana na hatua alizochukua dhidi ya matumizi yasiyo ya lazima. Kwa

kasi hii, kulikuwa na kila sababu ya kutarajiwa kuiona Tanzania ikipaa kiuchumi, na hatimaye

Watanzania kunufaika na neema lukuki ambayo nchi yao imejaaliwa kuwa nayo.

Wakati tangu wakati alipoteuliwa na CCM kuwa mgombea wa chama hicho katika nafasi ya

urais, Watanzania wengi hawakuwa shaka kuhusu uchapakazi wa Dokta Magufuli, ‘mtihani’ wa

awali ulikuwa kuhusu nani angemteua kuwa Waziri Mkuu. Hatimaye alimteua mwasiasa

asiyefahamika sana lakini anayesifika kwa uchapakazi, Khassim Majaliwa. Na haikuchukua

Page 37: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

muda kuthibitishwa kuwa chaguo la Dokta Magufuli kwa Waziri Mkuu Majaliwa lilikuwa sahihi

kwani mara tu baada ya kuapishwa, alichukua hatua kadhaa zilizoonyesha kuwa yeye na ‘bosi’

wake ni ‘dream team.’

Moja ya hatua za awali za Waziri Mkuu Majaliwa ni ziara ya ghafla katika Bandari ya Dar

es Salaam, ambako alibaini upotevu wa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya shilingi

bilioni 80. Baadaye alifanya kikao na uongozi wa Bandari hiyo na ule wa Mamlaka ya Mapato

(TRA) na kuwasimamisha kadhi maofisa kadhaa wa taasisi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na

Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade. Kadhalika, Waziri Mkuu alimwagiza Mkuu wa Jehsi la

Polisi kuwakamata maofisa hao ili waisaidie polisi katika uchunguzi.

Ufanisi mkubwa uliopatikana kwa Dokta Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa wakisaidiwa

na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefui, kumudu kufanya kazi bila ya baraza

la mawaziri, ulipelekea baadhi ya wananchi kutamani kusiwepo kabisa baraza hilo kwani

matunda ya viongozi hao yalionekana bayana. Hofu kubwa kuhusu baraza la mawaziri ilikuwa

katika uwezekano wa kurejea sura zilizozoeleka aidha kwa uzembe au ufisadi.

Japo hili litaongelewa kwa kirefu baadaye, kinachoweza kuelezwa kama ‘doa la kwanza’

katika utawala wa Dokta Magufuli ni pale alipotangaza baraza lake la mawaziri. Kwa vile

ilichukua zaidi ya mwezi mzima kuunda baraza hilo, matarajio ya wananchi wengi yalikuwa

makubwa katika kuona ‘sura za kuleta matumaini’ na zenye uwezo wa kuendana na kasi ya Rais

wao.

Baraza hilo lilitangazwa kwa awamu mbili, huku wizara chache zikiachwa ‘viporo.’ Jina la

waziri lililoonekana kugusa hisia za wengi, huku baadhi wakihoji busara za Dokta Magufuli, ni

la Profesa Sospeter Muhungo, mwanasiasa msomi ambaye alilazimika kujiuzulu katika utawala

wa Rais Kikwete kufuatia kashfa ya Tegeta Escrow.

Kilichowakera baadhi ya wananchi kuhusu Profesa Muhongo sio tu kuhusishwa kwake na

kashfa hiyo ya Escrow, ambayo baadaye ilipelekea kujiuzulu kwake, bali pia kauli yake maarufu

ya dharau kuwa Watanzania wanaweza kufanya biashara ya juisi tu na sio kumudu uwekezaji

mkubwa kama katika sekta ya gesi na mafuta. Hadi alipoteuliwa tena na Dokta Magufuli,

Profesa Muhongo hakuwahi kuikana kauli hiyo wala kuifafanua. Kwa maoni ya wengi, alipaswa

kuwaomba msamaha Watanzania kwa kuwadhalilisha.

‘Doa’ jingine kwa Dokta Magufuli ni pale alipotangaza majina ya kuziba ‘wizara viporo,’

ambapo miongoni mwa walioteuliwa alikuwa Profesa Jumanne Maghembe, aliyekabidhiwa

Wizara ya Maliasili na Utalii. Si tu kwamba Waziri huyo mpya alishawahi kushika wadhifa huo

huko nyuma pasipo mafanikio makubwa, na baadaye alihamishwa kutoka Wizara hiyo, bali pia

aliwahi kutajwa na uongozi wa CCM kuwa ni mmoja wa ‘mawaziri mizigo,’ yaani wasio na

ufanisi katika utendaji kazi wao.

Pengine kuthibitisha kuwa uteuzi wa maprofesa hao wawili ulikuwa na walakini, wote

wawili wameshatoka madarakani wakati kitabu hiki kinaandikwa. Profesa Muhongo alilazimika

kujiuzulu tena (kama alivyolazimika kujiuzulu katika serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais

Kikwete) baada ya Kamati iliyoundwa na Rais kuchunguza mchanga wenye madini (makinikia)

kutoa taarifa inayoonesha upotevu wa Sh trilioni 1.439 baada ya uchunguzi, kupima mchanga

ulio kwenye kontena 277 zilizozuiwa kusafirishwa nje ya nchi tangu Machi mwaka huu.

Kwa upande wa Profesa Maghembe, jina lake halikuwemo katika mabadiliko madogo ya

Baraza la Mawaziri la Dokta Magufuli yaliyofanyika Oktoba mwaka huu. Japo hakuna maelezo

yaliyokwishatolewa kuhusu uamuzi wa Dokta Magufuli kumwondoa Profesa huyo katika

Uwaziri, yayumkika kuamini kuwa uamuzi huo ulitokana na uendaji kazi usioridhisha.

Page 38: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Hata hivyo, pamoja na uwepo wa Profesa Muhongo na Profesa Maghembe katika kabineti

ya kwanza ya Dokta Magufuli, taarifa kwamba mawaziri wote walisainishwa mikataba maalum

‘inayowanga,’ kwa maana kuwa pindi wizara zao zikiboronga wao ndio watakuwa wa kwanza

kuwajibishwa, ziliwapa matumaini wananchi kuwa hata mawaziri wanaoangaliwa ‘kwa jicho la

walakini’ wangeweza kuwa wachapakazi wazuri kwani kinyume cha hivyo wangetimuliwa.

Na katika kuonyesha mabadiliko angalau ya kimtizamo, Profesa Muhongo alitangaza

kuwakaribisha wazawa katika uwekezaji katika sekta ya umeme, hatua iliyotafsiriwa kuwa

huenda amebadili mtizamo wake kuhusu uwezo wa Watanzania kuishia kwenye kutengeneza

juisi tu na si katika uwekezaji mkubwa.

Kwa upande wake, Profesa Maghambe alinukuliwa akieleza bayana kuzitambua

changamoto zinazoikabili sekta ya maliasi na utalii na kuapa kupambana nazo vilivyo, huku

akipigia mstari matumizi ya teknolojia ya kisasa katika kukabiliana na tatizo sugu la ujangili.

Kadhalika, uamuzi wa Dokta Magufuli kumteua Dokta Philip Mpango, mchumi wa zamani

katika Benki ya Dunia, na mchapakazi ‘aliyefanya miujiza’ kwa kuiwezesha Mamlaka ya

Mapato kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 1.3 kwa mwezi mmoja tu baada ya kuteuliwa ukaimu

Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo, uliwapa matumaini makubwa Watanzania kuwa baraza lake

la mawaziri lingeendana na faslafa yake ya ‘Hapa Ni Kazi Tu.’

Kumpatia Dokta Mpango Wizara nyeti ya Fedha na Mipango ilionekana kama ‘kuuwa

ndege wawili kwa jiwe moja.’ Kwa upande mmoja, mafanikio aliyoyaonyesha katika muda

mfupi tu akiwa kaimu Kamisha Mkuu wa TRA, yaliashiria kuwa Dokta Magufuli ameipatia

Tanzania mtu sahihi kabisa anayeweza kulisaidia taifa kiuchumi, hususan kukabiliana na tatizo

sugu la ukwepaji kodi. Kanuni za kiuchumi kuhusu ukusanyaji kodi zipo bayana: taifa lisilo na

ufanisi katika ukusanyaji kodi na matumizi yake lazima litayumba kiuchumi. Kwa muda mrefu,

tatizo kwa nchi hiyo halikuwa kwenye makusanyo ya kodi pekee bali pia matumizi yasiyoendana

na kidogo kilichokusanywa katika kodi. Mara baada ya kuingia madarakani, Dokta Mpango

alieleza bayana kuwa asingekubali kuona ama kuendelea kuwafumbia macho watu ambao

wangebainika kuitumia TRA kama pango la kujinufaisha kiuchumi.

Kwa upande mwingine, ukweli kwamba mchumi huyo aliwahi kufanya kazi kwa ufanisi

katika Benki ya Dunia ulimaanisha kuwa Tanzania sio tu ilimpata mtu mwenye uelewa mkubwa

wa masuala ya uchumi kimataifa bali pia mwenye uzoefu na hadhi iliyotarajiwa kuleta matokeo

chanya katika mahusiano na nchi nyingine katika uchumi wa dunia.

Kama kulikuwa na hofu yoyote kuhusu baadhi ya walioteuliwa kuwa mawaziri au manaibu

waziri, basi uteuzi wa makatibu wakuu na manaibu wakuu uliongeza matumaini zaidi kwa

Watanzania. Timu ya watendaji hao wakuu kitaalamu katika wizara ilijumuisha maprofesa 7,

madokta 14, wahandisi 6, ma-meja jenerali wastaafu wawili na mabalozi wa zamani wawili.

Kuchanganya na maprofesa, madokta na wahandisi kadhaa waliosheheni katika kabineti yake ya

kwanza, ilitarajiwa kuwa hakutokuwa na fursa ya uzembe katika serikali ya Dokta Magufuli.

Kitu kimoja kikubwa muda mfupi tu baada ya Dokta Magufuli kuingia madarakani ni

matumaini ya wananchi wengi kurejea kwa kasi. Matumaini hayo yalitokana na dalili za awali

kuwa kiongozi huyo alikuwa akitekeleza kaulimbiu yake ya ‘Hapa Ni Kazi Tu’ kwa vitendo

pasipo porojo.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge, Rais alitanabaisha kuwa kazi yake ni ‘kutumbua

majipu,’ na ghafla neno hilo likatokea kupata umaarufu mkubwa, huku mafisadi, wala rushwa,

wazembe na kadhalika wakianza kuitwa ‘majipu.’

Sambamba na umaarufu wake ulionekana kukua kwa kasi nchini Tanzania, Dokta Magufuli

pia alijipatia umaarufu mkubwa duniani kufuatia hatua zake mbalimbali za ufanisi alizochukua

Page 39: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

tangu alipoingia madarakani. Licha ya hatua kadhaa za kubana matumizi, Dokta Magufuli pia

alichukua hatua dhidi ya watendaji wenye mapungufu, huku miongoni mwa ‘wahanga’ wa awali

akiwa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuwia na Kupambana na Rushwa

(TAKUKURU), Dokta Edward Hoseah, ambaye wadhifa wake huo ulitenguliwa na Rais.

Wiki tatu tu tangu baada ya kuapishwa kuwa Rais, mtandao wa kijamii wa Twitter

‘ulitikiswa’ na ‘trend’ maarufu kabisa ya #WhatWouldMagufuliDo, yaani ‘Je Magufuli

angefanyaje,’ ambapo watumiaji wa mtandao huo kutoka sehemu mbalimbali duniani

walionyesha mapungufu yanayofanywa na viongozi wa nchi zao, na kujiuliza Magufuli

angefanya pindi angekuwa kiongozi katika nchi hizo.

Kana kwamba hiyo haitoshi, vyombo mbalimbali vya habari duniani viliripoti kuhusu

ufanisi wa Dokta Magufuli, huku baadhi ya wanahabari wakiwashauri viongozi wa nchi zao

kuiga mfano wa kiongozi huyo.

Katika hali inayoweza kuonekana kama miujiza, ilifikia hatua kundi la wananchi nchini

Kenya kuandamana wakidai ‘Magufuli awe rais wao’ wakionyesha kuchoshwa na tuhuma

mbalimbali zinazouandama utawala wa Rais Uhuru Kenyatta.

Kadhalika, watumiaji mbalimbali wa mitandao ya kijamii kutoka kila kona ya dunia

walimtumia Dokta Magufuli kama ‘reference’ (kielelezo) kudai uwajibikaji kwa viongozi katika

nchi zao.

Kwa hakika ukiondoa zama za ‘mwanasiasa wa kimataifa’ marehemu Baba wa Taifa, Julius

Nyerere, Tanzania ilikuwa haijawahi kushuhudia kiongozi wake akipata umaarufu dunia nzima

kama inavyotokea kwa Dokta Magufuli katika siku zake za mwanzo za urais wake. Na hisia

miongoni mwa Watanzania wengi siku hizo zilikuwa kwamba huenda nchi yao ilikuwa

imefanikiwa kupata mrithi halisi wa Nyerere, sambamba na mrithi wa marehemu Sokoine,

Waziri Mkuu aliyesifika kwa uchapakazi na kuichukia rushwa kwa dhati.

Kilichotia matumaini makubwa zaidi kuhusu uchapakazi wa Dokta Magufuli,

kilijidhihirisha katika hotuba yake aliyoitoa alipokutana na uongozi wa Jumuiya za

wafanyabiashara wakubwa, ambapo licha ya kuwaamuru waliokwepa kodi kujisalimisha ndani

ya siku 7, aliwasihi watumie uwezo wao kuiletea Tanzania maendeleo kusudiwa. Alieleza kuwa

anaamini kabisa kuwa nchi yetu ina uwezo wa kuwa mingoni mwa nchi wafadhili, na

kutanabaisha anatamani kuona hilo linatokea huko mbeleni.

Sura ya sita katika kitabu ‘Dokta John Magufuli: Safari Ya Urais, Mafanikio Na

Changamoto Katika Urais,” kilichochapishwa siku 55 tu baada ya Rais Magufuli kuingia

madarakani, iligusia changamoto mbalimbali ambazo mwandishi alidhani zingeweza kumkabili

kiongozi huyo, licha ya kilichoonkena mafanikio makubwa katika siku zake za awali.

Moja ya changamoto hizo ilikuwa ukweli kwamba Dokta Magufuli asingeweza kufanikiwa

peke yake pasipo ushirikiano wa Watanzania wote. Mfano ulikuwa kwenye mapambano dhidi ya

rushwa, ambapo mwandishi alikumbusha kuwa mara nyingi Watanzania wamekuwa

wakikumbushwa kuhusu umuhimu wa kujenga kasumba ya kudai haki na stahili zao (kwa

amani) badala ya kuona haki au stahili zao ni kama fadhila au upendeleo flani. Kwa kutambua na

kudai haki au stahili zao, wananchi wangeweza kumsaidia Rais wao kwa ‘kulazimisha’ huduma

bora na ufanisi pasipo haja ya yeye au wasaidizi wake kuingilia kati. Na uzuri wa kufanya hivyo

ni kwamba ingezua ‘domino effect,’ kwamba mafanikio katika eneo moja yangeweza

kuhamasisha taasisi nyingine zilizozembea kubadilika pia.

Ilielezwa kwamba isingekuwa rahisi kwa Rais Magufuli au wasaidizi wake kwenda kila

sehemu kuwezesha au kuharakiasha upatikanaji wa huduma. Jukumu hilo lingepaswa kusaidiwa

na wananchi wenyewe ambao mara nyingi ndio wahanga wakubwa wa huduma mbovu.

Page 40: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kadhalika, watoa huduma wangeanza kutambua kuwa hizo ni zama mpya, mambo yamebadilika,

kwahiyo shurti nao wabadilike.

Kadhalika, mchango wa wananchi wote ungehitajika katika kupambana na ufisadi, rushwa

na uhalifu mwingine. Wakati Rais aliahidi kukabiliana na ‘mapapa’ wa uhalifu kama kwenye

biashara hatari ya madawa ya kulevya, pasipo wananchi kumsaidia kwa kuwatenga wahusika na

kuwaripoti - badala ya kuwasujudia na kuwapa majina ya heshima kama ‘wazungu wa unga’ au

‘mapedejee’ – ingepunguza ufanisi wa jitihada hizo, na Tanzania ingeendelea kuumizwa na

vitendo hivyo viovu.

Kadhalika, ilishauriwa kuwa ili kauli-mbiu ya ‘Hapa Ni Kazi Tu’ iweze kuleta matokeo

kusudiwa na kuwa ya ufanisi ingebidi kila Mtanzania kuachana na dhana fyongo ya kusaka

mafanikio kwa njia za mkato, kwamba kungekuwa na haja ya kurejea zama za Ujamaa na

Kujitegemea ambapo waliokula bila kuvuja jasho waliitwa ‘kupe.’ Kila mtu alipaswa achape

kazi, kuacha kufanya ‘ujanja ujanja,’ kuona fahari kuwa na shughuli halali badala ya kuamini

kuwa ufisadi, rushwa, uhalifu, nk ndio njia rahisi na sahihi za kufikia mafanikio kwa haraka.

Changamoto nyingine kubwa, na iliyotarajiwa kugusa mahusiano kati ya Tanzania na nchi

wahisani ilikuwa mgogoro wa kisiasa huko Zanzibar uliosababishwa na uamuzi wa Tume ya

Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kufuta matokeo ya uchaguzi wa Rais wa huko, na kuagiza uchaguzi

huo urudiwe tena. Na uliporudiwa, chama kikuu cha upinzani cha CUF kilisusia uchaguzi huo,

na hadi muda huu chama hicho kimegoma kuitambua serikali ya CCM huko Zanzibar..

Licha ya Katiba ya Muungano na ile ya Zanzibar kumnyima Dokta Magufuli nafasi kubwa

ya kuliingilia tatizo hilo kwa undani, si yeye wala Rais wa Zanzibar Dokta Ali Mohammed

Shein anayeonekana na kuwa na nia ya kusaka suluhisho la kudumu la mgogoro huo wa kisiasa.

Kwa upande mwingine, mgogoro mkubwa unaoendelea CUF ambao umezua makundi

makuu mawili – linalomuunga mkono Mwenyekiti wa Taifa aliyotangaza kujiuzulu kabla ya

kurejea madarakani ‘kimabavu,’ Profesa Ibrahim Lipumba, na lile la Katibu Mkuu wa chama

hicho, Seif Sharif Hamad – unaweka mazingira magumu ya kusaka mwafaka katika mgogoro wa

kisiasa huko Visiwani.

Changamoto nyingine ya wazi kwa Dokta Magufuli na serikali yake ilikuwa tatizo la

ufisadi, rushwa na uhalifu kwa ujumla. Japo katika hotuba yake ya uzinduzi wa Bunge, Dokta

Magufuli aliongelea changamoto hiyo kwa urefu na mapana, na kueleza bayana kuwa vita hiyo

ni ngumu na anahitaji Watanzania wamwombee, bado kulikuwa na hofu kwamba huenda

asingepata kuungwa mkono vya kutosha na baadhi ya wana-CCM waliokuwa wakikumbatia

ufisadi, rushwa, na uhalifu mwingine.

Katika kitabu hicho, mwandishi alishauri kwamba ili Dokta Magufuli afanikiwe kukabiliana

na changamoto hizo, licha ya dua na sala za Watanzania kwake, na licha ya wao kumuunga

mkono kwa kuchukia vitendo hivyo na kupambana navyo, silaha kubwa ambayo angeihitaji zaid

ni Idara ya Usalama wa Taifa. Tasnia ya usalama wa taifa ina kanuni moja kuu: ‘kukua kwa

matishio kwa usalama wa taifa (kama ufisadi, rushwa, madawa ya kulevya, ujangili, nk) ni ishara

ya wazi ya mapungufu ya kiufanisi ya idara ya usalama ya taifa husika.’

Kwa maana hiyo, kushamiri kwa maovu hayo katika Tanzania yetu kulikuwa ishara za wazi

za mapungufu ya kiutendaji ya taasisi hiyo nyeti. Kwa muda mrefu, mwandishi, kama mtumishi

wa zamani wa taasisi hiyo, na kwa sasa msadi (consultant) katika fani hiyo, amekuwa akihimiza

haja ya kufanyika mageuzi ya kimfumo na kiutendaii kwa taasisi hiyo muhimu.

Moja ya mapendekezo hayo ni haja ya kuwepo kile wazungu wanaita ‘oversight,’ yaani

chombo au utaratibu unaoweza angalau kuwahoji watendaji wakuu wa Idara hiyo. Kwa hali

iliyokuwepo, taasisi hiyo inaonekana kutumia nyenzo yake muhimu kiutendaji kazi, ya usiri,

Page 41: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kuficha mapungufu yake, sambamba na kutochukua hatua stahili dhidi ya matishioya usalama

kwa taifa.

Kwa uelewa wa mwandishi, miongoni mwa vikwazo vya ufanisi kwa taasisi hiyo ni ajira

zilizokuwa zinazotolewa kiupendeleo. Mwandishi alishauri kwamba njia rahisi ya kukabiliana na

tatizo hili ni kuwa na utaratibu wa wazi wa ajira kama ilivyo kwa taasisi kubwa za usalama

duniani, kwa mfano CIA, NSA, MI6, MI5 na GCHQ. Ajira ya uwazi maana yake ni matangazo

ya ajira hizo kuwekwa bayana, na taratibu za ajira kuzingatia sifa, vipaji na uwezo badala ya

undugu au kujuana. Afisa usalama wa taifa anayeamini kuwa ajira yake ni matokeo ya ‘msaada

wa flani’ anaweza kuwa na mapungufu makubwa katika uzalendo, ambao ni nguzo kuu katika

utumishi kwa taasisi za usalama wa taifa dunian kote.

Kadhalika, ilishauriwa kwamba kuna haja kwa Idara hiyo kupewa nguvu zaidi ya kuishauri

tu serikali. Kama ilivyo kwa taasisi nyingi kubwa za usalama wa taifa duniani, kulikuwa na haja

ya kuangalia uwezekano wa kuiwezesha Idara ya Usalama wa Taifa kuwa na mamlaka ya

kukamata (power of arrest), hasa ikizingatiwa kuwa mbinu zinazotumiwa na maafisa usalama wa

taifa ni za hali ya juu zaidi ya polisi, TAKUKURU au taasisi nyingine za usalama.

Ilielezwa kuwa umuhimu wa mabadiliko kwa taasisi hiyo si tu kwa minajili ya kumsaidia

Dokta Magufuli katika utekelezaji wa majukumu yake, lakini pia ukweli kwamba vita

aliyotangaza dhidi ya mafisadi, wafanyabiashara ya madawa ya kulevya, majangili, nk ilikuwa

dhidi ya watu hatari. Ukweli kwamba uhalifu waliokuwa wanafanya watu hao ni sehemu

muhimu ya uhai wa watu hao ulimaanisha kwamba wangemtazama Dokta Magufuli kama

kizingiti katika maisha yao ya kihalifu, na wangeweza kuwa na dhamira ya kumdhuru.

Ili kuwadhibiti, taasisi pekee ambayo ingeweza kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi ni Idara

hiyo ya Usalama wa Taifa. Lakini ili iweze kufanya hivyo kwa ufanisi, sharti yenyewe iwe ‘safi.’

Taarifa za ndani zilionyesha kuwa kwa muda mrefu baadhi ya watendaji wa taasisi hiyo

walikuwa wakitumika kwa maslahi ya watu binafsi. Pasipo kuchukua hatua madhubuti, ‘rogue

elements’ ndani ya taasisi hiyo zilionekana kuweza sio tu kukwaza jitihada za Dokta Magufuli

kupambana na wahalifu bali pengine hata kujaribu kumdhuru.

Kimfumo, mwandishi alishauri kuwa ni muhimu kwa Idara ya Usalama wa Taifa

kutojihusisha na siasa. Hili lilikuwa tatizo la muda mrefu na liliathiri sana ‘professionalism’

katika taasisi hiyo muhimu. Wakati siasa ni moja ya maeneo ya kushughulikiwa na taasisi hiyo,

kuchanganya taaluma na siasa kulipelekea kile kinachoitwa kibaiolojia kama ‘symbiotic

relationship,’ yaani uhusiano wa kutegemeana kati ya wanasiasa na taasisi hiyo. Moja ya athari

kubwa ilikuwa uwezekano wa taasisi hiyo kutumika kwa maslahi binafsi ya wanasiasa au

watendaji wa serikali.

Changamoto nyingine ni ndani ya CCM, chama ambacho kwa muda mrefu kimewakumbatia

mafisadi, wauza madawa ya kulevya, majangili, na wahalifu wengineo. Kama ilivyo kwa Idara

ya Usalama wa Taifa na siasa, uhusiano kati ya CCM na baadhi ya watu wasio na wasifu wa

kupendeza katika ujamii nao umekuwa symbiotic, ambao baadhi ya watu wanaofahamika kuwa

ni mafisadi au wanaojihusisha na uhalifu wamewekeza fedha zao katika chama hicho tawala kwa

aidha kukichangia fedha au kuwafadhili wagombea wa chama hicho katika kuwania nyadhifa

mbalimbali.

Hata hivyo, pamoja na changamoto hizo nilizoainisha hapo juu, mwandishi alikuwa na

matumaini makubwa kuwa Dokta Magufuli na timu yake ingefanikiwa sio tu kukabiliana na

changamoto hizo bali pia kumudu kuifikisha Tanzania mahala inapostahili kuwa. Ilitarajiwa

kuwa chini ya utawala wa Dokta Magufuli, zama za Tanzania kuwa miongoni mwa nchi

masikini kabisa duniani licha ya utajiri lukuki iliojaaliwa kuwa nao, zingeanza kuelekea

Page 42: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

ukingoni. Pia zilianza kujitokeza hisia kwamba huenda huko mbeleni Tanzania ingeweza kuwa

moja ya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi duniani, na pengine kuingia katika kundi la nchi

wafadhili.

Kitabu hicho kilihitimishwa kukumbushia kuwa takriban muda wote akiwa kwenye kampeni

zake, na takriban katika hotuba zake alizotoa baada ya kuapoishwa kuwa rais (hadi wakati kitabu

hicho kinachapishwa), neno ambalo Dokta Magufuli alikuwa akilitaja sana ni MUNGU. Hii

ilionekana kuwa ishara nzuri na muhimu, kwa sababu takriban robo tatu ya Watanzania ni

washika dini wanaomtumainia Mwenyezi Mungu katika maisha yao ya kila siku. Kwa hiyo, kwa

Dokta Magufuli kumtaja Mungu mara kadhaa katika hotuba zake, ilileta hisia kuwa sio tu taifa

hilo limepata kiongozi mchapakazi lakini pia mcha Mungu. Na hiyo ilipelekea kumkumbuka

marehemu Nyerere ambaye inaelezwa kwamba moja ya sababu za mafanikio katika uongozi

wake ilikuwa ucha-Mungu wake.

Page 43: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Tano

Kwa jinsi hali ya Tanzania ilivyokuwa hususan kabla Dokta Magufuli haijaingia madarakani,

kulikuwa na ulazima kwa kiongozi huyo kuja na mikakati kabambe ya kuiondoa Tanzania katika

mwelekeo mbaya. Pamoja na viongozi wakuu wawili wa Awamu ya Nne, Rais Jakaya Kikwete

na Waziri Mkuu wake Mizengo Pinda kutamka bayana kuwa hawaelezwi kwanini Tanzania ni

masikini, haikuhitajika japo utafiti kubaini kwamba kushamiri kwa rushwa na ufisadi

kulichangia umasikini kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande mmoja, sera za kiuchumi za watangulizi wa Rais Magufuli, yaani marais

Mwinyi, Mkapa na Kikwete, ziliwapendeza nchi na taasisi wahisani, na Tanzania ilikuwa moja

ya nchi iliyonufaika kwa kiasi kikubwa na misaada ya kimataifa. Wakati fulani, Tanzania

ilikuwa nchi ya tatu nyuma ya Afghanistan na Iraq kunufaika na misaada ya kimataifa. Hata

hivyo asilimia kubwa ya misaada hiyo iliisha mifukoni mwa mafisadi.

Kwa upande mwingine, watangulizi hao wa Dokta Magufuli hawakufanya jitihada za

kutosha kuandaa na kutekeleza sera madhubuti za kuondoa masikini. Pamoja na kutofanikiwa

vya kutosha, sera mbalimbali za kiuchumi katika serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya

Nyerere zililenga kuondoa umasikini kwa kuweka njia kuu za kiuchumi katika miliki ya umma.

Japo kuna wanasiasa ‘wajanja’ waliotumia fursa hiyo kujinufaisha, Tanzania chini ya utawala wa

Nyerere ilikuwa nchi ambayo ya usawa kwa kiasi cha kuridhisha.

Wakati serikali ya Awamu ya Pili chini ya Rais Mwinyi ilihusika na ‘kifo cha itikadi ya

Ujamaa na Kujitegemea’ kupitia kiitwacho ‘Azimio la Zanzibar,’ serikali ya Awamu ya Tatu

chini ya Rais Mkapa iliweka mbele zaidi maslahi ya wawekezaji kuliko wananchi wazawa. Na

baada ya Rais Mkapa kuondoka madarakani, ilibainika kuwa nyuma ya pazia la uwekezaji

kulikuwa na dalili za ufisadi.

Kama hali ilikuwa mbaya katika Awamu ya Pili na ya Tatu, basi hali ilikuwa mbaya zaidi

katika serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Kikwete. Moja ya sababu kubwa zilizotengeneza

mazingira mabovu kwa utawala huo ni kampeni ya Kikwete kuingia Ikulu ambayo ilihusisha

kundi lililofahamika kama ‘wanamtandao,’ lililojaa watu wa aina mbalimbali, wengi wao

wakiwa na wasifu usiopendeza. Kundi hilo lilipigana kufa na kupona kuhakikisha kuwa

mgombea wao Kikwete anaingia madarakani. Inaelezwa kuwa jitihada za kundi hilo zilianza

mara baada ya jaribio lililoshindikana la Kikwete na aliyekuwa mshirika wake mkubwa,

Lowassa, kuwania urais mwaka 1995. Inaelezwa kuwa Nyerere aliingilia kati jaribio hilo na

hatimaye ‘kumpitisha mgombea wake’ yaani Mkapa.

Baadhi ya wanamtandao walimpigania Kikwete kwa matarajio ya kulipwa fadhila mara

baada ya mwanasiasa huyo kuingia madarakani. Na kwa upande mwingine, Kikwete aliingia

madarakani akiwa na deni kubwa la fadhila kwa wanamtandao. Ndio maana haikushangaza

kuona miezi michache tu baada ya kuingia madarakani, serikali yake ikaanza kuandamwa na

kashfa mbalimbali za ufisadi.

Yayumkinika kuhitimisha kuwa japo tatizo la ufisadi lilianza kuchipuka kwa kasi katika

serikali ya Awamu ya Pili chini ya Rais Mwinyi, na kupata nguvu zaidi kupitia sera za uwekezaji

Page 44: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

za serikali ya Awamu ya Tatu ya Mkapa, zama za Kikwete sio tu ziliimarisha ufisadi bali pia

ziliufanya kuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya Mtanzania.

Ni katika Awamu hiyo ambapo uhalifu kwa maana ya rushwa na ufisadi, ujangili, biashara

ya madawa ya kulevya, nk viligeuka kuwa kama shughuli halali. Katika utawala wa Kikwete,

kuna wakati bidhaa kwa iliyosafirishwa nje (export) na iliyoingizwa Tanzania kutoka nje

(import) ilikuwa madawa ya kulevya.

Kushamiri kwa vitendo vya kihalifu katika utawala huo vilijenga saikolojia isiyopendeza

mingoni mwa Watanzania kwamba njia yenye ufanisi zaidi kufikia mafanikio ni kujihusisha na

vitendo hivyo vya kihalifu. Kwa kushindwa kuchukua hatua stahili dhidi ya mafisadi, wauza

madawa ya kulevya, majangili, nk ilifika mahala ikaonekana kana kwamba vitendo hivyo

vimehalalishwa, na hiyo ikahamaisha watu wengi zaidi – hususan vijana – kujiingiza kwenye

vitendo hivyo.

Kwahiyo kimsingi hayo ndio mazingira ambayo Dokta Magufuli alikumbana nayo wakati

anaingia madarakani. Lakini ukweli kwamba mwanasiasa huyo alikuwa mmoja ya mawaziri

katika serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Kikwete, sambamba na taswira iliyojengeka kuwa

CCM – chama ambacho Dokta Magufuli alipitia kugombea urais – kilikuwa ‘kichaka cha

kuhifadhi mafisadi, ulileta hofu baadhi ya Watanzania kuwa huenda utawala mpya usingeweza

kuleta mabadiliko yoyote ya maana.

Lakini kama ilivyoelezwa awali kwamba katika kampeni zake za kuwania urais, Dokta

Magufuli alionekana kuelemea zaidi kwenye maslahi ya taifa kuliko kuweka mbele itikadi za

chama chake CCM. Kadhalika, mwanasiasa huyo alionyesha ujasiri mkubwa kwa kukiri makosa

ya chama chake huku akienda mbali zaidi na kuonyesha jinsi angeweza kuyarekebisha makosa

hayo.

Na kama ilivyokuwa katika kampeni za urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010

ambapo ajenda kuu ilikuwa ufisadi uliokigubika serikali ya Kikwete na CCM kwa ujumla, huku

chama kikuu cha upinzani Chadema kupitia mgombea wake Dkt Slaa kikiwa kimejitanabaisha

kama wapambanaji wakubwa dhidi ya ufisadi, kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 nazo

zilishuhudia ajenda ya ufisadi ikiwa na umuhimu wa kipekee.

Kwa upande mmoja, wakati Dokta Magufuli alipata ujasiri wa kueleza bayana jinsi ufisadi

ulivyoshamiri ndani ya chama chake, jinsi unavyowaathiri Watanzania, na jinsi ambavyo

angeshughulikia tatizo hilo, kwa upande mwingine, umoja wa vyama vya upinzani wa UKAWA

‘ulipatwa na kigugumizi’ kuongelea suala hilo kwa sababu zilizo wazi. Itakumbukwa kuwa kwa

takriban miaka 9 mfululizo, vyama vya upinzani hususan Chadema vilikuwa vikimwandama

aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika serikali ya Kikwete, Lowassa, kuwa ni kielelezo cha

ufisadi ndani ya CCM. Na kwa hakika, ufuatiliaji wa Chadema ulichangia uamuzi wa Lowassa

kujiuzulu Uwaziri Mkuu mwaka 2008 kutokana na kuhusishwa na kashfa ya Richmond.

Kutokana na uamuzi wa Lowassa kujiunga na upinzani baada ya kutofanikiwa azma yake ya

kuwania urais kupitia CCM, iliwawia vigumu UKAWA kuongelea ajenda ya ufisadi kwani wao

walikuwa na mchango mkubwa katika kujenga dhana kwamba ‘Lowassa ni fisadi.’

Kwa wapinzani kukwepa ajenda hiyo muhimu, ilimpa fursa nzuri Dokta Magufuli kuielezea

kama tatizo linalohitaji ufumbuzi na kueleza mikakati yake ya kukabiliana nalo.

Japo ni kweli kwamba nyota ya Lowassa ilikuwa inang’ara mno hadi wakati anajiondoa

CCM, Chadema na UKAWA kwa ujumla walijinyima fursa nzuri mno ya kuibana CCM kuhusu

ufisadi hasa ikizingatiwa kuwa jitihada za Chadema dhidi ya tatizo hilo zilikuwa zikiungwa

mkono na Watanzania wengi.

Page 45: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Kulikuwa na tatizo jingine kuhusu Lowassa. Katika vitabu vyangu viwili kuhusu uchaguzi

mkuu wa mwaka 2015, nilielezea kosa la kiufundi lililofanywa na Lowassa katika safari yake ya

kuwania urais. Ikumbukwe kuwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ilikuwa kama

kilichobaki ni suala la muda tu kabla mwanasiasa huyo kutangazwa rais. Kadhalika, kadri

uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ulivyokuwa unazidi kujongea ndivyo umaarufu wa Lowassa

ulivyozidi kuongezeka.

Lakini badala ya kutumia fursa hiyo vizuri, mwanasiasa huyo alionekana kama

aliyebweteka, huku akikataa kutamka bayana iwapo angegombea urais. Aliendelea na hali hiyo

hadi katikati ya mwaka 2014 ambapo mwanasiasa kijana January Makamba alitangaza rasmi nia

yake ya kuwania urais. Ghafla, ile dhana kuwa ‘Lowassa ndio rais ajae wa Tanzania’ ikaingiliwa

na jina la mwana-CCM mwingine, yaani January.

Taratibu yakaanza kuibuka majina ya makada wengine wa chama hicho tawala waliotangaza

nia zao za kuwania urais. Lowassa alipoamua kutangaza rasmi nia yake, ule mvuto uliokuwepo

awali ulishaaza kupungua, huko wanasiasa kama January wakizidi kupaa kwa umaarufu.

Kwamba huenda Lowassa alijiamini kupita kiasi ndio maana hakuona umuhimu wa

kutangaza mapema dhamira ya kuwania urais, au iwapo maandalizi yake yalikuwa duni na

hatimaye kupelekea jina lake kutopitishwa na chama chake, ni vigumu kueleza kwa uhakika.

Lakini yayumkinika kuhitimisha kuwa Lowassa aliyejiunga na Chadema na baadaye kuwa

mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA hakuwa na umaarufu/mvuto mkubwa kama ule aliokuwa

nao baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Kwahiyo, kwa kiasi flani safari ya Dokta Magufuli ilirahisishwa na makosa ya kimkakati

yaliyofanywa na Chadema/UKAWA. Kadhalika, ajenda mbadala ya ‘mabadiliko’ ambayo

Lowassa alikuja nayo katika kambi ya upinzani haikuwa na mwelekeo, na hadi tarehe ya

uchaguzi mkuu ilipofika, ajenda hiyo ilibaki kuwa kauli-mbiu.

Tukiweka kando mazingira hayo yaliyomwingiza madarakani Dokta Magufuli, miaka

miwili ya uongozi wake imekuwa na mafanikio kadhaa na kasoro kadhaa pia. Sura hii itajikita

kwenye mafanikio pekee.

Moja ya mafanikio makubwa kabisa ya serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dokta Magufuli

ni vita dhidi ya ufisadi. Japo ni mapema mno kuhitimisha kuwa ushindi kamili umeshapatikana

katika vita hiyo, angalau kuna dalili za kuridhisha.

Mafanikio makubwa zaidi kwenye vita dhidi ya ufisadi ni ya kisaikolojia zaidi kuliko

kisheria. Hapa inamaanisha kwamba japo kuna idadi ndogo tu ya watu waliokamatwa au

kuondolewa madarakani kwa tuhuma za ufisadi, kwa mara ya kwanza na baada ya miaka mingi

Watanzania wameanza kupatawa na uoga wa kujihusisha na vitendo vya uhalifu kama ufisadi,

rushwa, ujangili, biashara ya madawa ya kulevya, na kadhalika.

Ni rahisi kumzuwia mtu asifanye kitendo flani lakini ni ngumu mno kumjengea mtu imani

kuwa kitendo hicho anachopaswa kutofanya sio kizuri. Kwa zaidi ya miaka 30 tangu Nyerere

ang’atuke, idadi kubwa tu ya Watanzania ilikuwa ikiishi kwa imani kwamba vitendo vya uhalifu

ni njia muhimu ya kumudu maisha yao. Na kwa upande mwingine, wengi wao waliamini kuwa

vitu kama rushwa ni majaliwa (fate) yao. Kwamba visingeondoka hata zingefanyika jitihada

kiasi gani.

Licha ya ukweli kwamba dhamira ya kupambana na ufisadi kwa dhati ilikuwa ndogo katika

zama za Mwinyi, Mkapa, na zaidi wakati wa Kikwete, asilimia kubwa tu ya wananchi

‘walisherehesha’ matendo ya kihalifu kama vile ufisadi na biashara ya madawa ya kulevya.

Kuthibitisha hilo, mafisadi walipewa heshima ya kuitwa ‘mapedejee’ badala ya ‘wala rushwa’ au

Page 46: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

‘wabadhirifu,’ kama sio ‘wahalifu.’ Na kwa upande wao, wauza madawa ya kulevya walipewa

heshima mtaani kwa kuitwa ‘wazungu wa unga.’

Watu waliojihusisha na uhalifu huo waliheshimiwa mno katika jamii, na wananchi wengi

waliona ufahari kuwa karibu na wahalifu hao. Ilisikitisha zaidi kuona wauza unga

wakinyenyekewa licha ya ukweli kwamba biashara haramu waliyokuwa wakifanya ilikuwa

ikipelekea vifo vya mamia ya vijana wanaotumia madawa ya kulevya. Kadhalika, mafisadi

walioitwa ‘mapedejee’ pia walichangia majanga kadhaa katika jamii kwa sababu fedha

walizokwapua zilipangwa kutumika kuwahudumia wananchi.

Kutochukuliwa hatua stahili kwa wahalifu hao kulipelekea dhana kwamba kuwa fisadi, au

muuza madawa ya kulevya, au jangili, ni ‘kuwa mjanja,’ kitu kilichowafanya vijana wengi

kupainia kuingia kwenye magenge ya kiharamia kama hayo badala ya kufikiria vitu vya

maendeleo kama kujiendeleza kimasomo au kutafuta ajira.

Kwa upande mwingine, mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi, biashara haramu ya madawa

ya kulevya yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kurejesha heshima ya kazi halali. Katika kilele cha

matendo hayo ya kihalifu, kuwa mwajiriwa wa umma au sekta binafsi au hata kujiajiri

kulionekana kama ‘uwendawazimu.’ Waajriwa walioonekana ‘wenye akili’ ni wale waliokuwa

kwenye ‘sehemu za ulaji,’ yaani maeneo ya kazi yaliyowapa fursa ya kufanya ufisadi.

Sambamba na kuahidi kupambana na rushwa na ufisadi na uhalifu mwingine, Dokta

Magufuli pia aliahidi kuanzisha mahakama maalum ya kushughulikia kesi za ufisadi. Mahakama

hiyo imeshaanzishwa japo mwenendo wake hadi wakati ninaandika kitabu hiki bado ni

‘wakusuasua.’ Hata hivyo, hatua tu ya kuanzisha mahakama hiyo inaashiria kuwa dhamira ya

Dokta Magufuli kupambana na rushwa haikuwa hadaa zilizozoeleka katika kampeni za uchaguzi

mkuu.

Changamoto kwa mahakama hiyo ‘changa’ ni nyingi, kubwa zaidi ikiwa uwezo duni wa

wanasheria wa serikali ambao wana ‘rekodi nzuri tu’ ya kupoteza kesi muhimu. Lakini jingine ni

urasimu uliopo katika mchakato wa kuwafikisha watuhumiwa katika mahakama hiyo.

Sambamba na hilo ni mapungufu yanayoikabili Taasisi ya Kupambana na Kuzuwia Rushwa

(TAKUKURU), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali.

Hata hivyo, changamoto hizo zipo ndani ya uwezo wa serikali ya Dokta Magufuli kuzitatua.

Kwa vile kushamiri kwa vitendo vya kihalifu kama vile ufisadi, rushwa, biashara ya

madawa ya kulevya na ujangili kulikuwa na mchango mkubwa kuvunja moyo ari ya kuchapa

kazi, jitihada za Dokta Magufuli kupambana na vitendo hivyo kumewezesha kuamsha ari ya

uchapakazi miongoni mwa Watanzania wengi. Kwa upande mmoja, jitihada za serikali ya

Awamu ya Tano kupambana na vitendo hivyo kumefanikiwa kwa kiwango cha kuridhisha

kuziba mianya ya ‘watu kuishi kiujanja ujanja’ au kwa kutegemea njia zisizo halali. Taratibu,

kipato halali – hata kama ni kidogo – kinaanza kuonekana kuwa ndio njia sahihi ya kumudu

maisha.

Kwa upande mwingine, kuondoa utegemezi kwa njia zisizo halali kumechangia kwa kiasi

cha kuridhisha kurejesha heshima ya kazi halali, kitu kilichopotea kwa takriban miaka 30. Na sio

kurejesha tu heshima ya kazi halali bali pia jitihada hizo zimefanikiwa kwa kiasi cha kuridhisha

kurudisha nidhamu ya watumishi wa umma kuanzia ngazi za juu hadi chini.

Katika siku za mwanzo za urais wake, Dokta Magufuli alifanya ziara kadhaa za kushtukiza

ambazo zilipelekea kuwakumbusha watumishi wa umma wajibu wao, sambamba na kuchelewa

‘kutumbuliwa,’ msamiati uliopata umaarufu baada ya ujio wa kiongozi huo, na uliomaanisha

kuondoa wazembe, mafisadi na watu wasiotekeleza wajibu wao ipasavyo.

Page 47: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Hata kabla hajaunda Baraza lake la Mawaziri, Dokta Magufuli alifanya ziara mbili kubwa za

kushtukiza ambapo Novemba 6, 2015 ikiwa ni siku moja tu baada ya kuapishwa alitembea kwa

miguu kutoka Ikulu hadi Wizara ya Fedha ambako alipita katika ofisi moja baada ya nyingine na

baadaye alifanya kikao na watendaji. Novemba 9 alifanya ziara nyingine ya kushtukiza katika

Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alivunja Bodi ya Wakurugenzi, alimwondoa Kaimu

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk. Hussein Kidanto na kuamuru mashine muhimu za vipimo za

CT-Scan na MRI kutengenezwa haraka huku akitoa sehemu ya mshahara wake kumlipia

mgonjwa mmoja aliyekuwa anahitaji kufanyiwa kipimo cha CT-Scan.

Japo kuna waliotafsiri kuwa ziara hizo za kushtukiza ni za kusaka umaarufu, kiongozi huyo

alipata watetezi wengi walieleza bayana kwamba hata kama jitihada zake ni za kusaka sifa,

hakuna tatizo kwani matokeo mazuri yalianza kuonekana bayana. Ziara hizo za kushtukiza

ambazo baadaye zilifanywa pia na baadhi ya mawaziri wake baada ya kuunda baraza lake la

mawaziri, zilipelekea ‘watumishi wa umma waliojisahau’ kutambua kuwa zama zimebadilika na

wanapaswa kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi.

Pia juhudi hizo za Dokta Magufuli zilipelekea ‘vigogo’ wa taasisi mbalimbali kama vile

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuswekwa ndani,

kusimamishwa, kutenguliwa teuzi zao na wengine kufikishwa mahakamani kwa makossa

mbalimbali, yakiwemo uzembe, rushwa na ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Miongoni mwa waliokumbwa na rungu la Dokta Magufuli ni pamoja na aliyekuwa

Kamishna Mkuu wa TRA Rished Bade, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya

Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Dickson Maimu, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa

TAKUKURU Edward Hosea, aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Sylvester

Ambokile, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Viwango (TBS), Joseph Masikitiko, Mkurugenzi

Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Raslimali za Meli (RAHCO) Benhadard Tito, na wengineo kadhaa.

Hatua hizo za Dokta Magufuli sio tu zimesaidia kurudisha nidhamu kwa watumishi wa

umma na kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi bali pia zimeiacha historia mpya

katika uwajibishaji, hasa ikizingatiwa kwamba kwa muda mrefu hatua iliyozoeleka katika

uwajibishaji ni kumhamisha kiongozi kutoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine.

Mafanikio mengine ya Dokta Magufuli ni utekelezaji wa ahadi yake ya ‘elimu bure’ kuanzia

chekechea hadi kidato cha nne. Kimsingi, sera hii ni kama inairejesha Tanzania katika zama za

itikadi ya Ujamaa ambapo elimu ilikuwa ikitolewa bure hadi kiwango cha chuo kikuu. Mageuzi

ya kiuchumi yaliyoanza katikati ya miaka 1980s yalipelekea serikali kujiondoa katika utoaji wa

baadhi ya huduma kwa jamii, sambamba na kuanzishwa kwa sera ya wananchi kuchangia

gharama za utoaji huduma kwa jamii (cost sharing). Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika ni

pamoja na sekta ya elimu ambapo wazazi walitakiwa kuchangia gharama mbalimbali za masomo

ya watoto wao. Kutokana na kuzidi kuongezeka kwa umasikini, baadhi ya wazazi hawakuweza

kumudu gharama za kuwapelekea watoto wao shule au za watoto hao kuendelea na masomo

katika ngazi mbalimbali.

Kwahiyo, sera hii ya elimu bure kuanzia ngazi ya chekechea hadi kidato cha nne inairejesha

Tanzania katika zama ambazo fursa ya elimu ilikuwa kwa kila mwanafunzi bila kujali uwezo wa

kiuchumi wa mzazi wake. Wakati ni muhimu kuhakikisha elimu inayotolewa ni ya kiwango

sahihi, fursa kubwa kwa wanafunzi wengi kujiunga au kuendelea na elimu ni suala lenye

umuhimu kwa taifa.

Pengine ingekuwa vema sera hiyo ingesubiri kuboreshwa kwa miundombinu katika sekta ya

elimu lakini kufanya hivyo kungewanyima nafasi mamilioni ya watoto wa Kitanzania kuanza au

Page 48: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kuendelea na masomo yao. Uamuzi wa kutekeleza sera hiyo huku miundombinu katika sekta ya

elimu ikiboresha ni bora zaidi.

Yafahamika kwamba kuna changamoto nyingi, kubwa zaidi zikiwa uhaba wa nyenzo kama

madarasa, madawati, vitabu vya kiada, na kadhalika, sambamba na upungufu wa walimu

unaoambatana na maslahi duni ya walimu hao. Hata hivyo, changamoto hizo hazipaswi kugubika

ukweli kwamba sera ya elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato ya nne ni ukombozi mkubwa

kwa Watanzania. Nyingi ya changamoto zinazoikabili sera hiyo zimekuwepo kwa muda mrefu,

na kinachohitajika ni jitihada endelevu za kuboresha sekta ya elimu kwa ujumla sambamba na

kufanyia kazi changamoto zinazoikabili sera ya elimu bure.

Eneo jingine ambalo Dokta Magufuli amefanikiwa ni kubana matumizi ya serikali. Katika

hotuba yake ya kuzindua Bunge, kiongozi huyo aliweka hadharani takwimu zilizoomyesha jinsi

pato la taifa lilivyokuwa likiteketea katika matumizi mbalimbali ya serikali yanayoweza

kukwepeka. Moja ya maeneo yaliyokuwa yakiligharimu mno taifa ni safari za nje za watumishi

wa serikali. Dokta Magufuli alipiga marufuku safari hizo isipokuwa zitakazoidhinishwa kwa

kibali maalumu na Katibu Mkuu Kiongozi.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na serikali, uamuzi wa Dokta Magufuli kubana safari

za watumishi wa serikali kwenda nje ya nchi umepelekea serikali kutumia shilingi bilioni 25 tu

katika miaka mwili iliyopita kulinganisha na zaidi ya shilingi bilioni 216 katika mwaka wa

fedha 2014/2015.

Hayo ni mafanikio makubwa hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba Tanzania ni nchi

masikini ambayo asilimia kubwa ya bajeti yake inategemea misaada ya nchi na mashirika

wahisani. Kwahiyo kila shilingi inayookolewa kupitia hatua za kubana matumizi ina faida

kubwa.

Sambamba na kubana matumizi ya serikali, serikali ya Dokta Magufuli imekuwa na

mafanikio ya kuridhisha katika ukusanyaji mapato hasa kupitia kodi mbalimbali. Miongoni mwa

sababu zilizokuwa zikichangia umasikini wa Tanzania ni pamoja na mianya lukuki ya ukwepaji

kodi sambamba na misahama mingi ya kodi iliyotolewa kwa ufisadi.

Katika mwaka wake wa kwanza madarakani, Mamlaka ya Mapato (TRA) ilikusanya wastani

wa trillion 1.1 kila mwezi kuanzia mwezi Novemba 2015 hadi Septemba 2016, ongezeko la

asilimia 28.1 kutoka wastani wa shilingi bilioni 867 kwa mwezi katika kipindi cha mwezi

Novemba, 2014 hadi Septemba 2015.

Jitihada za ukusanyaji mapato ya serikali zinazoendana na serikali kupunguza matumizi

yake zimechangia kuifanya Tanzania chini ya utawala wa Dokta Magufuli kuwa miongoni mwa

nchi zinazofanya vema kiuchumi duniani. Kwa mujibu wa takwimu Julai mwaka huu, nchi hiyo

ilikuwa miongoni mwa nchi 5 za Afrika zilizokuwa zikiongoza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi

(Ivory Coast 7.9%, Tanzania 7.1%, Senegal 6.6%, Djibouti 6.5%, na Ethiopia 6.5%).

Kwa mujibu wa bajeti ya serikali ya mwaka 2017/2018 iliyosomwa Julai mwaka huu,

mapato ya serikali kuanzia Julai 2016 hadi Aprili 2017 yalikuwa shilingi trilioni 20,710.5 sawa

na asilimia 70 ya lengo la mwaka la shilingi trilioni 29, 536.9.

Kadhalika, matumizi ya serikali katika kipindi hicho yalikuwa shilingi trilioni 20,036.5

ambapo vipaumbele vikuu vya bajeti hiyo vilikuwa katika ujenzi na ukarabati wa barabara kuu

za mikoa na Halmashauri; miradi ya ujenzi wa barabara ikiwa ni pamoja na ulipaji madeni ya

wakandarasi na wahandisi washauri; miradi ya uzalishaji umeme; uboreshaji wa njia za kupitisha

umeme na usambazaji wa umeme vijijini; mikopo ya elimu ya wanafunzi wa elimu ya juu;

malipo ya awali ya ujenzi wa reli kwa kiwango cha ‘standard gauge’ awamu ya kwanza katika

eneo la Dar es Salaam hadi Morogoro; ununuzi wa ndege mbili na malipo ya awali ya ununuzi

Page 49: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

wa ndege nne; usambazaji wa maji mijini na vijijini; na uboreshaji huduma za afya katika ngazi

zote ikiwa ni pamoja na ununuzi wa madawa.

Mafanikio mengine ya Dokta Magufuli na serikali yake ni vita aliyoanzisha dhidi ya

watumishi hewa na wale waliokuwa na vyeti vya kugushi. Japo zoezi hili lililaumiwa kwamba

lilifanywa kiubaguzi kutokana na ukweli kwamba liliwalenga watumishi wa umma wa kadi za

chini tu, lilisaidia serikali kuokoa jumla ya takriban shilingi bilioni 370. Katika kila shilingi

inayookolewa na serikali, ni muhimu kutazama kwa kuzingatia ukweli kuwa Tanzania bado ni

miongoni mwa nchi masikini zaidi duniani. Kwahiyo kila shilingi inayookolewa ina umuhimu

mkubwa kwa wananchi.

Eneo jingine ambalo kwa muda mrefu limekuwa likiikosesha Tanzania fedha nyingi ni

katika raslimali zake mbalimbali hususan madini na maliasili. Dokta Magufuli na serikali yake

amefanikiwa kwa kiasi cha kuridhisha kupigania maslahi ya taifa katika sekta za madini na

maliasili. Hadi wakati huu ambapo kitabu hiki kinaandika, tayari serikali ya Dokta Magufuli

imefanikiwa kufikia makubaliano na kampuni kubwa ya madini duniani, Barrick Gold ya

Canada, ambayo ni yenye hisa kubwa kwenye kampuni kubwa zaidi ya uwekezaji katika sekta

ya madini nchini Tanzania, Acacia Mining.

Makubaliano hayo yalifikiwa kutokana na uamuzi wa Dokta Magufuli kuzuwia makontena

kadhaa ya makinikia yaliyokuwa yakisafirishwa kwenda nje, na baadaye kuunda tume mbili za

kuchunguza jinsi Tanzania ilivyokuwa ikikoseshwa mapato katika uwekezaji kwenye sekta ya

madini.

Katika makubaliano hayo, Barrick ilikubali kuilipa Tanzania hisa asilimia 16 na mgao wa

asilimia 50 ya mapato ya mauzo ya dhahabu kutoka migodi inayomilikiwa na Acacia. Mbali ya

malipo hayo, kampuni hiyo pia ilikubali kutoa dola milioni 300 kama malipo ya nia njema

kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kutokana na biashara za kampuni hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti ya moja ya tume hizo mbili, Tanzania ilikuwa imepoteza takriban

shilingi trilioni 188 katika kipindi cha miaka 19 kati ya mwaka 1998 hadi mwaka huu kupitia

usafirishwaji nje wa makinikia ya dhahabu na shaba.

Pamoja na hatua hiyo, serikali ya Dokta Magufuli imefanikiwa kuzifanyia marekebisho

sheria zinazohusiana na raslimali za taifa ili ziwe na manufaa stahili kwa Tanzania. Kadhalika,

jitihada hizo za kulinufaisha taifa kupitia raslimali zake zimeelekezwa pia kwenye sekta ya

maliasili na utalii ambapo hatua kadhaa zinachukuliwa, ikiwa ni pamoja na ‘kutumbuliwa’ kwa

aliyekuwa Waziri wa Maliasi ya Utalii, Profesa Maghembe.

Vilevile, kwa mara ya kwanza, mgogoro wa muda mrefu na uliotawaliwa na tuhuma

mbalimbali za ufisadi katika eneo la Loliondo unaelekea kupatiwa ufumbuzi baada ya Waziri

mpya wa Maliasi na Utalii, Dokta Hamis Kigwangalla kuamuru kufutwa kwa vibali vyote vya

uwindaji nchi nzima.

Mafanikio mengine yaliyopatikana ndani ya miaka miwili ya utawala wa Dokta Magufuli ni

pamoja na ujenzi wa hosteli mpya za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zenye uwezo

wa makazi kwa wanafunzi 3840. Ikumbukwe kuwa moja ya adha kubwa za elimu katika chuo

kikuu hicho kikubwa kuliko vyote chini Tanzania ni uahaba wa makazi kwa wanafunzi.

Kadhalika, Novemba 2016 Dokta Magufuli alitoa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa

nyumba mpya zitakazotumika kwa makazi ya askari wa gereza la Ukonga, Dar es Salaam.

Pengine kutokana na ukweli kwamba huko nyuma Dokta Magufuli alikuwa Waziri wa

Ujenzi kwa muda mrefu, tangu aingie madarakani amekuwa na kiu kubwa ya kukufua Shirika la

Ndege la Tanzania. Tayari serikali yake imeshanunua ndege 2 na kutoa malipo ya awali ya ndege

nyingine 4. Kwa pamoja, gharama ni shilingi 234.9 kiasi ambacho kw upande mwingine

Page 50: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kimezua mjadala miongoni mwa Watanzania huku baadhi yao wakihoji iwapo ndege hizo ni

kipaumbele kikubwa zaidi ya sekta kama elimu na afya ambazo ‘zinasuasua’ kutokana na uhaba

wa fedha.

Katika suala la ujenzi na miundombinu, Dokta Magufuli amefanikiwa kuanzisha miradi

mbalimbali, kwa mfano, ujenzi wa flyover Tazara na Ubungo, jijini Dar; Upanuzi wa Uwanja wa

Ndege wa Mwanza; Upanuzi wa kisasa wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius

Nyerere jijini Dar; upanuzi wa Barabara ya Morocco jijini Dar; kuzindua ujenzi wa reli yenye

kiwango cha ‘standard gauge’; barabara ya kuunganisha wilaya za Kibondo mkoani Kigoma na

Kauliua mkoani Tabora; Ujenzi wa barabara ya Mtwara -Tandahimba; ukarabati wa reli kati ya

Tanga na Moshi. Ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi bandari ya

Tanga.

Mradi mwingine mkubwa ni ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa huko Chato – eneo

analotoka Dokta Magufuli – na kama ilivyotarajiwa, mradi huo umezua ‘maneno’ kadhaa huku

kiongozi huyo akituhumiwa kulipendelea eneo analotoka, na baadhi ya wanasiasa wakidai kuwa

fedha za mradi huo hazikuidhinishwa na bajeti. Suala hili litajadiliwa kwa kirefu katika sura

ijayo.

Kwa kubana matumizi na kuongeza mapato ya serikali kwa kukusanya kodi sambamba na

kuwabana wakwepa kodi, serikali ya Dokta Magufuli imeweza kuboresha sekta mbalimbali za

huduma kwa jamii kama vile afya na maji hususan katika maeneo ya vijijini. Hata hivyo bado

kuna changamoto kubwa katika upatikanajai wa dawa mahospitalini sambamba na miundombinu

duni katika hospitali nyingi, huku uhaba wa madaktari na wauguzi ukiendelea kuathiri maeneo

mengi.

Kwa upande wa maji, huduma hiyo imeendelea kutokuwa ya uhakika sana huku taarifa

mbalimbali kwenye vyombo vya habari vikionyesha jinsi wananchi wanavyotaabika kupata maji.

Hata hivyo, serikali ya Dokta Magufuli imeendelea kufanya jitihada za kuanzisha au kuboresha

miradi kadhaa ya maji.

Kuna msemo wa Kiswahili usemao “Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni” ambao kwa

kiasi kikubwa unaweza kufaa kama wito kwa Watanzania wanapotathmini utendaji kazi wa

Dokta Magufuli, miaka miwili sasa tangu aingie madarakani Novemba 5, 2016. Kwamba,

pamoja na changamoto mbalimbali zilizopo, angalau kuna jitihada za kuridhisha zilizofanyika,

zinazofanyika na zinazotarajiwa kufanyika kumkwamua Mtanzania. Kwa hakika safari hiyo

bado ni ndefu na ngumu lakini angalau imeanza.

Kadhalika, ni rahisi ‘kumhukumu’ Dokta Magufuli iwapo ‘mtoa hukumu’ atapuuzia hali

ilivyokuwa kabla ya kiongozi huyo kuingia madarakani, na hali aliyoikuta alipoingia

madarakani. Na yawezekana kwamba miongoni mwa sababu zinazochelewesha kasi ya

mafanikio ya jitihada za Dokta Magufuli na serikali yake ni masalio ya mfumo wa kifisadi

uliodumu kwa takriban miaka 30.

Katika kuhitimisha sura hii, ni muhimu kubainisha kuwa kuna idadi kubwa ya Watanzania

wenye matumaini kuwa jitihada za Dokta Magufuli zinaweza kuiondoa Tanzania kutoka katika

kundi la nchi masikini kabisa duniani, na tegemezi wa misaada, na kupiga hatua kimaendeleo

pengine hadi kufikia kiwango cha kuwa miongoni mwa nchi wahisani. Ukweli ulio bayana ni

kwamba nchi hiyo imejaaliwa utajiri mkubwa wa raslimali ambao ukisimamiwa na kutumika

ipasavyo unaweza kusaidia mno maendeleo ya taifa.

Page 51: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Sura Ya Sita

Magufuli 2.0

Kwa kuazima lugha ya kompyuta, ambapo maendeleo ya mtandao huangaliwa katika vizazi

– Web 1.0 (kizazi cha kwanza kati ya mwaka 1990 hadi 2000 ambapo mtandao ulitawaliwa na

maandishi, na mawasiliano yakiwa ya upande mmoja, kutoka kwa mwandishi kwenda kwa

msomaji), Web 2.0 (kizazi cha pili kati ya mwaka 2000 hadi 2010 ambapo mtandao ulitawaliwa

na social interaction kati ya mwandishi na msomaji) na sasa Web 3.0 kizazi cha tatu kati ya

mwaka 2010 hadi 2020 ambapo mtandao umekuwa ukitumia akili kama mwanadamu kwa mfano

kutekeleza majukumu wenyewe baada ya kujifunza kutoka kwa mwanadamu) – tathmini ya

miaka miwili ya utawala wa Dokta Magufuli inaweza pia kuangaliwa kwa namna hiyo.

Haihitaji uelewa mkubwa wa siasa za Tanzania kutambua kuwa kuna tofauti za msingi kati

ya Dokta Magufuli ‘wa mwanzo’ na ‘huyu aliyetimiza miaka miwili madarakani mwezi uliopita,

Novemba 2017. Lakini kutambua tofauti hizo ni kitu kimoja, ilhali kufahamu sababu

zilizopelekea kubadilika huko ni kitu kingine kabisa. Hadi wakati ninaandika kitabu hiki

hakujapatikana maelezo ya kujitosheleza kuhusu kitu gani hasa kimepelekea mabadiliko ya

kiongozi huyo.

Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kwa kiasi kikubwa mwanasiasa

huyo alionekana kama mwanasiasa asiye na makuu, wa kawaida, anayesukumwa zaidi na hali

halisi na uchungu kwa nchi badala ya kuweka mbele itikadi za kisiasa. Hotuba zake mbalimbali

katika kampeni zilionyesha uelewa wake mkubwa kuhusu matatizo yanayoikabili Tanzania na

jinsi ya kuyatatua.

Japo kama mgombea urais alilazimika kuwanadi wagombea ubunge na udiwani kutoka

CCM lakini haikuwa vigumu kubaini kuwa kipaumbele chake kikubwa kilikuwa kuhusu

Tanzania zaidi kuliko chama chake. Na hilo lilileta matumaini makubwa baada ya ushindi wake

katika nafasi ya urais kwa sababu kwa muda mrefu itikadi za siasa zimekuwa zikiwekwa mbele

ya maslahi ya taifa.

Moja ya vitu vilivyoleta matumaini makubwa miongoni mwa Watanzania kuhusu urais wa

Magufuli ni hotuba yake aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa bunge la Jamhuri ya Muungano.

Katika hotuba hiyo, Dokta Magufuli alionyesha kuwa mtu anayezielewa vema shida za

Watanzania hususan janga la rushwa na ufisadi, na akaapa kushughulikia kwa nguvu zake zote.

Na alipoomba Watanzania wamwombee katika vita hiyo ngumu, yayumkinika kuhisi kuwa hata

miongoni mwa wale ambao hawakumpigia kura waliitikia wito huo wa kumfanyia maombi.

Baada ya hapo zikaja ziara ya kushtukiza - kama ilivyoelezwa katika sura iliyotangulia -na

taratibu Watanzania wengi wakaanza kuingiwa na matumaini mapya ya “mrithi halisi wa

Nyerere/Sokoine.”

Shangwe kuhusu Dokta Magufuli hazikuwa Tanzania pekee. Awali zilianza kusambaa

katika nchi jirani hususan Kenya ambapo baadhi ya wananchi walieleza waziwazi kuwa

walitamani wangeweza kumwazima kiongozi huyo asafishe nchi yao dhidi ya rushwa na ufisadi.

Kana kwamba hiyo haitoshi, umaarufu wa Dokta Magufuli ukasambaa takriban kila kona ya

dunia, na kilele kilifikiwa pale ilipoibuka alama #WhatWouldMagufuli Do iliyotamba kila kona

Page 52: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

ya dunia. Kiongozi huyo aliwagiwa sifa lukuki kutokana na uchapakazi wake sambamba na

chuki dhidi ya rushwa na ufisadi.

Kwa kufurahishwa na kuridhishwa na utendaji wake, mwandishi wa kitabu hiki aliamua

kuandika kitabu cha tathmini ya urais wa Magufuli, siku 55 tu baada ya kiongozi huyo

kuapishwa kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Watu kadhaa walikosoa

uamuzi huo wa kuchapisha kitabu chenye tathmini ya kiongozi aliyeingia madarakani muda

mfupi tu uliopita. Wengi waliona kwamba haikuwa sahihi kwa mwandishi kufanya tathmini hiyo

mapema kiasi hicho. Hata hivyo, kwa hali ilivyokuwa wakati huo, ilikuwa rahisi kwa mwandishi

kudhani kwamba waliomkosoa kuhusu suala hilo walikuwa kama wenye chuki binafsi dhidi ya

‘mkombozi’ Magufuli.

Dalili ya kwanza kwamba huenda kuna walakini katika utawala wa Magufuli ni pale

alipotangaza baraza lake la mawaziri ambalo ilichukua wiki kadhaa kulisubiri. Lilipotangazwa,

sio tu lilikuwa kubwa kuliko ahadi yake kuwa angeunda serikali ndogo tu ili kupunguza gharama

za uendeshaji wa serikali, bali pia lilijumuisha baadhi ya sura ‘zenye utata.’ Miongoni mwa sura

hizo ni Profesa Muhongo, ambaye awali alilazimika kujiuzulu katika serikali ya Awamu ya Nne

kutokana na kuhusishwa na skandali ya Tegeta Escrow.

Kadhalika, kuna waliouona uteuzi wa makada kama Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba

ulikuwa ni wa kisiasa zaidi, huku sura kama George Simbachawene, William Lukuvi na Profesa

Jumanne Maghembe zikijenga ishara kuwa huenda mambo hayajabadilika kama ilivyotarajiwa.

Kisha kukafanyika uteuzi wa mabalozi wa kuiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali

ambao ulionekana bayana kama kutumia nafasi hizo nyeti kuwaondoa watu flani kwenye

nyadhifa zao huko CCM. Baadhi ya watu wakaanza kujiuliza, “hivi hatujayashuhudia haya huko

nyuma?” Hata hivyo, hofu hiyo ilikuwa miongoni mwa watu wachache tu huku wengi

wakiendelea kuwa na matumaini kwa Dokta Magufuli.

Dalili ya kwanza kabisa kuwa pamoja na mazuri yake yaliyowavutia Watanzania wengi na

kona mbalimbali duniani, Dokta Magufuli ana mapungufu yake ni pale serikali yake kupitia

aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ilipozuwia haki ya

mamilioni ya Watanzania kusikiliza matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge. Awali

lawama kubwa zilielekezwa kwa Nape ambaye wadhifa wake ulimhusisha moja kwa moja na

zuwio hilo lililolaaniwa vikali na Watanzania wengi. Hata hivyo, baadaye Rais Magufuli alieleza

bayana kuwa uamuzi wa kuzuwia matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge ulikuwa

wake binafsi, na waziri alitelekeza tu maagizo ya Rais.

Baadaye likaja zuwio dhidi ya mikutano na maandamano ya vyama ya siasa. Awali baadhi

ya wananchi waliona kuna mantiki japo kidogo kwenye zuwio hilo, kutokana na hoja kwamba

“ah huu ni muda wa kuchapa kazi. Hayo maandamano na mikutano ni ya nini muda huu?”

Kujipa matumaini huko kulichangiwa pia na ukweli kwamba wananchi wengi wanaziona

shughuli za kisiasa kama mikutano na maandamano zikiwaathiri zaidi wao kuliko wanasiasa.

Kwahiyo, angalau kwa wakati huo, zuio hilo lilionekana kama lenye nia nzuri.

Kilichofanya zuwio hilo kuonekana kuwa mkakati wa dhati wa serikali ya Dokta Magufuli

dhidi ya vyama vya upinzani ni pale chama tawala kiliporuhusiswa kufanya maandamano na

mikutano bila kubughudhiwa huku vyama vya upinzani vikizuiliwa. Kwa maana hiyo, zuwio

hilo ni kama lililenga kuinufaisha CCM na wakati huohuo kuvikandamiza vyama vya upinzani.

Tukio jingine ambalo kwa hakika lilijenga picha isiyopendeza kuhusu Dokta Magufuli ni

pale Tanzania ilipokumbwa na janga la tetemeko la ardhi mkoani Kagera Septemba 2016.

Mshtuko wa tetemeko hilo ulisikika hadi Uganda, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia

ya Watu wa Kongo na Kenya. Kwa mujibu wa maelezo ya serikali, jumla ya watu 17 walipoteza

Page 53: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

uhai huku wengine 240 wakijeruhiwa. Kadhalika, nyumba 2063 zilibomoka kutokana na

tetemeko hilo la ardhi.

Kwa kuwa pamoja na majukumu mengine aliyonayo Rais, yeye pia ni ‘mfariji mkuu, Dokta

Magufuli alitegemewa kwenda kuwafariji wahanga wa tetemeko hilo, na hasa ikizingatiwa kuwa

yeye pia anatoka Kanda ya Ziwa. Siku ya maombolezo ya kitaifa, Rais hakwenda na badala yake

aliwakilishwa na Waziri Mkuu Majaliwa.

Lakini wakati Watanzania wakiungana na wenzao wa Kagera walioathiriwa na janga hilo la

tetemeko la ardhi, Rais Magufuli alitoa kauli isiyopendeza kuhusu janga hilo akidai kwamba

“serikali haikuleta tetemeko hilo la ardhi.” Hata hivyo, hakuna rekodi yoyote inayoonyesha mtu

yeyote aliyedai kuwa serikali ndio iliyosababisha tetemeko hilo.

Baada ya miezi minne hivi, hatimaye Dokta Magufuli alifanya ziara mkoani Kagera na

kujionea mwenyewe uharibifu mkubwa uliosababishwa na tetemeko la ardhi. Hata hivyo, wakati

akiongea na wananchi ikiwa ni pamoja na wahanga wa tetemeko hilo, Dokta Magufuli alidai

kwamba “hakuna mahali popote duniani ambapo tetemeko likitokea serikali inaanza kujenga

nyumba za wananchi.” Haikuwa mwafaka kwa Rais kutoa kauli kama hiyo kwa sababu kwa

mujibu na mila za Kitanzania, lugha inayopaswa kutumika wakati wa majonzi ni ya kuliwazana.

Kadhalika, Rais Magufuli hakusema ukweli alipodai kwamba hakuna mahali popote duniani

ambapo tetemeko likitokea serikali inaanza kujenga nyumba za wananchi. Ukweli ni kwamba

hata katika nchi zilizoendelea kama Marekani, Italia na Japan ambazo asilimia kuwa ya wakazi

wake wanajimudu kiuchumi, serikali huwasaidia wananchi wake bila kujali uwezo wao

kiuchumi. Ndio Tanzania ni masikini na haina uwezo wa kumjengea nyumba kila mtu

aliyeathiriwa na janga hilo la tetemeko la ardhi lakini angalau lugha iliyotumika kufikisha

ujumbe kwa wananchi ilipaswa iwe ya kiungwana.

Baadaye zilisikika taarifa kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania kuhusu tishio la upungufu

wa chakula na dalili za uwepo wa baa la njaa. Lakini waliotarajia kwamba huenda wangepata

maneno ya faraja kutoka kwa Rais wao, Dokta Magufuli aliweka bayana msimamo wa serikali

yake kwamba haitotoa chakula kwa vile “haina shamba.”

Ni kweli inapendeza kuwa na kiongozi ‘asiyeuma maneno,’ na anayeeleza vitu kama

vilivyo. Ni kweli pia kwamba kwa muda mrefu, Tanzania ilikuwa ikiongozwa na ‘kauli tamu’ za

baadhi ya viongozi ambazo zilipendeza masikioni mwa wananchi lakini nyingi ziliishia kuwa

porojo tu. Kwahiyo, tabia ya Dokta Magufuli kusema ukweli kama ulivyo ni. Hata hivyo, kuna

tofauti kati ya kusema ukweli, na kusema ukweli katika lugha isiyokwaza watu. Ilikuwa sahihi

kwa Dokta Magufuli kueleza kwamba serikali yake haiwezi kugawa chakula kwa wananchi

wanaokabiliwa na uhaba wa njaa lakini kiungwana, haikuwa mwafaka kusema kuwa “serikali

haiwezi kuwasaidia kwa sababu haina shamba.”

Januari mwaka huu akiwa Magu, Dokta Magufuli akiwa kwenye ziara yake ya kikazi,

wananchi walisimamisha msafara wake na baadhi yao kumlalamikia kuwa wana tatizo la njaa.

Wananchi hao wanasikika wakipaza sauti za 'njaa…njaa'' wakati akisalimia na kutoa shukrani

zake kwa kumchagua kuwa Rais. Hata hivyo, baada za kelele za njaa kuzidi, Dokta Magufuli

alisikika akisema ''njaa, unataka mimi nikakupikie chakula ule,'' kauli ambayo japo iliibua

vicheko ingeweza kujenga taswira kwamba kiongozi huyo hajali matatizo ya wananchi

anaowaongoza.

Kama ilivyoandikwa awali, licha ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu, Rais pia ni ‘mfariji mkuu’

kwa taifa. Kila linapotokea janga kubwa, inatarajiwa kuwa Rais atakuwa mstari wa mbele

kulifariji taifa sambamba na kuonyesha uongozi katika nyakati ngumu. Ni katika mazingira

Page 54: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

hayo, uamuzi wa Dokta Magufuli kutokwenda ‘hapo kwa hapo’ Kagera kushiriki maombolezo

ya kitaifa ya wananchi waliouawa na tetemeko la ardhi ulizua minong’ono ya hapa na pale.

Aprili mwaka huu, askari polisi wanane waliuawa kwa mkupuo huko Kibiti mkoani Pwani.

Tukio hilo liligusa hisia za Watanzania wengi lakini katika mazingira ya kushangaza, Dokta

Magufuli hakushiriki katika kuaga miili ya askari hao jijini Dar na badala yake akaenda kwenye

hafla ya uzinduzi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Amiri Jeshi

Mkuu ambaye pia ni mfariji mkuu kukosekana katika shughuli hiyo hakukujenga picha nzuri.

Mei mwaka huu, Tanzania ilikumbwa na msiba mkubwa kufuatia ajali iliyogharimu maisha

ya wanafunzi 33 wa Shule ya Lucky Vincent ya mkoani Arusha, walimu wawili na dereva

mmoja. Taarifa za ajali hiyo zilipata uzito mkubwa hadi kutangazwa na vyombo vya habari vya

kimataifa.

Hata hivyo, kwa mara nyingine tena, Dokta Magufuli hakuhudhuria maombolezo ya kitaifa

yaliyofanyika jijini Arusha na badala yake aliwakilishwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu

Hassan. Na kama ilivyokuwa katika tukio la Kagera na lile la polisi wanane, hakukutolewa

maelezo yoyote kwanini Rais hakuhudhuria katika maombolezo hayo.

Japo kuna hoja kwamba uwepo wa Rais katika matukio kama hayo hauwezi kurudisha uhai

wa waliopoteza maisha yao, mila na desturi zetu zinasisitiza mno umuhimu wa kuhudhuria

misiba, kitu ambacho husaidia kuwafariji wafiwa.

Septemba mwaka jana, zilipatikana taarifa za kupotea kwa kada mmoja maarufu wa

Chadema, Ben Saanane. Kada huyo alitokea kuivalia njuga shahada ya uzamifu ya Dokta

Magufuli, akidai kuwa ina walakini. Kijana huyo aliyekuwa na wafuasi wengi kwenye mitandao

ya kijamii pia aliunganisha ukosoaji wake huo na jitihada za Dokta Magufuli dhidi ya watumishi

wa umma waliogushi vyeti. Kwahiyo, Saanane alimtaka Rais athibitishe kwanza uhalali wa

shahada yake kabla ya kuwabana watumishi wa umma.

Hata hivyo, baadhi ya watu akiwemo mwandishi wa kitabu hiki walimsihi kada huyo kuwa

makini katika suala hilo kwani kulishaanza kuonekana dalili za Dokta Magufuli kutopenda

kukosolewa. Kwa bahati mbaya au makusudi, alipuuza ushauri huo.

Hadi wakati kitabu hiki kinaandikwa, haijulikani nini kimemsibu kijana huyo. Juhudi kubwa

zinazofanywa na familia yake, na Chadema kwa kiasi fulani, hazijazaa matunda. Jeshi la polisi

sio tu limekuwa halina msaada mkubwa katika kufuatilia ‘kupotea’ kwa kada huyo, lakini pia

limekuwa na wakati mgumu kupata ushirikiano kutoka Chadema hasa kutokana na mahusiano

mabaya kati ya jeshi hilo na chama hicho. Ugumu zaidi unatokana na ukweli kwamba jeshi hilo

linatuhumiwa na baadhi ya wafuasi wa chama hicho kuwa linahusika na kupotea kwa Saanane.

Hata hivyo, Chadema nao hawawezi kukwepa lawama katika suala hilo kwa jinsi

walivyozembea kulishughulikia. Kumekuwa na kauli zinazokinzana kutoka kwa baadhi ya

viongozi wa chama hicho kama ile ya mwenyekiti wa taifa, Freeman Mbowe kuwa Saanane

alitekwa huku Mbunge wa chama hicho Saeid Kubenea akidai kuwa kada huyo alikuwa

akionekana vijiweni. Haifahamiki kwanini chama hicho hakikuona umuhimu wa kuwabana

viongozi hao kufafanua kauli zao.

Kadhalika, taarifa alizonazo mwandishi wa kitabu hiki ni kwamba kiongozi mmoja wa ngazi

za juu wa chama hicho alifahamishwa na vyanzo vya kuaminika kuhusu kilichomsibu kada huyo

lakini hakuchukua hatua zozote.

Lakini kama kuna tukio lililompotezea heshima kubwa Dokta Magufuli ni lile la Mkuu wa

Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuvamia kituo cha redio na runinga cha Clouds akiwa

na askari wenye silaha, lakini siku chache baadaye, huku baadhi ya watu wakitarajia angemtimua

Page 55: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Makonda, Dokta Magufuli sio tu alimtetea Makonda na kumwita mchapakazi, pia aliwakebehi

wananchi waliotarajia angechukua hatua akieleza yeye ndo Rais, na hapangiwi kazi.

Tukio hilo liliwaacha midomo wazi Watanzania wengi kwani ilikuwa haiingii akilini kuona

Mkuu wa Mkoa huyo amevamia kituo cha habari, kitendo ambacho ni kosa la jinai, halafu Rais

anamtetea na kumsifu kuwa ni mchapakazi.

Uswahiba wa Dokta Magufuli na Makonda umechangia mno ugumu wa kuchunguza tuhuma

kuwa Mkuu huyo wa mkoa amegushi jina analotumia pamoja na cheti cha kuhitimu kidato cha

nne.

Katika hatua nyingine, Oktoba mwaka huu, Dokta Magufuli “alifunga rasmi mjadala kuhusu

vyeti na elimu ya Makonda” baada ya kusema kuwa anaridhishwa na utendaji wake na kwamba

kwake anamuona ni msomi mzuri.

Kauli hiyo ya Rais ilitafsiriwa kama jibu kwa tetesi kuwa Makonda alifeli kidato cha nne na

hivyo anatumia jina na vyeti vya mtu mwingine. Dokta Magufuli amekuwa akishauriwa angalau

kufanya uchunguzi kuhusu suala hilo, lakini mara zote amekuwa upande wa Mkuu wa Mkoa

huyo.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania

(ALAT), Dokta Magufuli aliwakosoa wanaomnyooshea kidole Makonda na kusema kwake yeye

ni msomi. “Wanasema hajasoma, mimi hata kama hajui A ila anakamata madawa ya kulevya,

kwangu ni msomi mzuri,” alisema Dokta Magufuli.

Kama kawaida yake, mkuu huyo wa nchi alimmwagia pongezi Makonda “kwa namna

anavyofanya kazi na kutatua changamoto za wananchi,” na kuwataka hatua wakuu wengine wa

mikoa kuja kujifunza kwake.

Hata hivyo, uswahiba kati ya Dokta Magufuli na Makonda umeendelea kuwakera watu

wengi, hasa ikizingatiwa kuwa Mkuu huyo wa Mkoa amekuwa akiutumia ipasavyo upendeleo

anaopewa na Rais, na hiyo kumpa jeuri ya kufanya dharau za waziwazi kama ile ya kupigiwa

saluti na vingozi wa ngazi za juu wa jeshi la polisi huku amevaa kofia aina ya ‘kapelo.’ Hiyo ni

dharau ya hali ya juu kwa vyombo vya dola.

Kwa upande mwingine, miaka miwili ya utawala wa Dokta Magufuli ilitawaliwa na wakati

mgumu kwa vyombo vya habari. Pengine dalili kwamba kiongozi huyu si rafiki wa vyombo vya

habari ni ukweli kwamba katika muda wote wa kampeni zake za urais mwaka 2015 hakufanya

mahojiano na chombo chochote cha habari.

Na hata baada ya kushinda kiti cha urais, Dokta Magufuli amefanya mkutano na waandishi

wa habari mara moja tu. Hata hivyo, kwa wananchi wengi, la muhimu sio kiongozi kusikika

mara kwa mara bali jinsi gani anawatumikia.

Ndani ya miaka miwili ya utawala wake, serikali yake imeshayafungia magazeti matano.

Agosti mwaka jana, serikali ililifungia gazeti la Mseto kwa miezi 36, kisha Juni mwaka huu

ikalifungia gazeti la Mawio kwa miaka miwili. Serikali ya Dokta Magufuli iliweka rekodi ya

aina yake kwa kufafungia magazeti matatu ndani ya kipindi cha takriban mwezi mmoja, ambapo

Septemba mwaka huu iliyafungia ya Raia Mwema (siku 90) na Mwanahalisi (miaka mwili) kisha

Oktoba mwaka huu ikalifungia gazeti la Tanzania Daima kwa siku 90.

Lakini hata kabla ya kuchukua hatua hizo zinazokandamiza uhuru wa vyombo vya habari

sambamba na kuwanyima wananchi haki ya kuhaharishwa, Dokta Magufuli alishavitahadharisha

vyombo vya habari kwamba uhuru walionao una mipaka.

''Serikali ya kutumbua majipu haiwezi kuacha kutumbua magazeti yanayofanya mambo ya

uchochezi hatuwezi kuiacha Tanzania ikawa dampo la eneo la kuweka maneno ya uchochezi

chini ya utawala wangu," alisema Dokta Magufuli.

Page 56: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

"Hilo halitakuwepo kuna magazeti mawili tu kila ukisoma wao ni kuchochea tu

ikizungumzwa habari hii wao wanageuza hii nasema na nataka wanisikie siku zao zimeshafika

kama wanasikia wasikie wasiposikia wasisikie lakini magazeti mengine na vyombo vyote

vingine vinatoa uchambuzi mzuri sana,” alitahadharisha kiongozi huyo katika kauli iliyotafsiriwa

kama yenye lengo la kuvitisha vyombo vya habari ili viandike habari zinazompendeza Rais

pekee.

Haya yametokea wakati Tanzania bado ipo kwenye mshtuko kufuatia jaribio la kumuua

mwanasiasa ambaye amekuwa mpinzani mkubwa wa Dokta Magufuli, mbunge wa Chadema

Tundu Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria cha TLS. Chuki inayopandikizwa

dhidi ya wapinzani imepelekea asilimia kubwa ya viongozi wa serikali na chama tawala CCM

kuogopa kwenda kumjulia hali Lissu huko Nairobi alikolazwa.

Kama ilivyokuwa kwa kada wa Chadema Ben Saanane ambaye ‘alipotea’ baada ya

kumwandama Dokta Magufuli kuhusu shahada yake ya uzamifu, Lissu nae alikumbana na

jaribio hilo dhidi ya maisha yake baada ya kujitokeza kuwa mwanasiasa mpinzani mkuu wa

Dokta Magufuli. Japo upinzani wao dhidi ya mkuu huyo wa nchi haumaanishi kuwa anahusika

dhidi ya yaliyowakuta, lakini haijengi picha nzuri.

Pengine kipimo halisi cha mambo kwenda kinyume na matarajio ya baadhi Ya Watanzania

kuhusu Dokta Magufuli ni kwamba katika miaka mwili ya utawala wake, zaidi ya viongozi na

wanachama 400 wa Chadema wamekamatwa na polisi. Japo tangu kuruhusiwa kwa mfumo wa

siasa za vyama vingi mwaka 1992, vyama vya upinzani vimekuwa vikiendesha shughuli zake

katika mazingira magumu, chini ya utawala wa Dokta Magufuli hali imekuwa ngumu zaidi.

Imefika mahala, wakuu wa wilaya wanakamata viongozi wa Chadema kila wanapojisikia.

Na pengine kibaya zaidi ni ukweli kwamba taratibu jamii inaanza kuzowea kuona viongozi na

wanachama wa upinzani – hususan Chadema – wakidhalilishwa na kukamatwa kiholela.

Jambo jingine la kusikitisha kuhusu utawala wa Magufuli ni utitiri wa sheria kandamizi

dhidi ya uhuru wa habari. Licha ya sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 ambayo ni

kazi ya Rais mstaafu Kikwete, kuna sheria mpya ya Huduma za Habari na kinachoitwa ‘Kanuni

za Maudhui ya Mitandao ya Kijamii,’ ambazo kwa kiasi kikubwa zinafanya uhuru wa habari na

mawasiliano kuwa suala la hisani ya serikali badala ya haki ya kikatiba.

Kwa kufuatilia jitihada zilizopo dhidi ya uhuru wa habari, na kwa kuzingatia ukweli

kwamba vyombo vya habari ‘vya asili’ kwa maana ya magazeti, redio na runinga zimedhitiwa

vyema na serikali, eneo ambalo linaweza kuwa mlengwa wa jitihada mpya na zaidi ni mitandao

ya kijamii.

Ikumbukwe kuwa Septemba mwaka jana, Dokta Magufuli aliweka wazi ‘hasira zake’ dhidi

ya mitandao ya kijamii aliposema kuwa anatamani malaika washuke na kuifunga mitandao hiyo

kwa mwaka mmoja. Uwepo wa mkataba kati ya serikali na kampuni moja ya Korea ya Kusini

inayoshughulika na teknolojia ya ‘kudhibiti mtandao’ unaweza kuashiria kuwa siku za uhuru wa

mitandao ya kijamii zinahesabika.

Kwa upande mwingine, huku Chadema ikishuhudia viongozi na wanachama wake

wakinyanyaswa mfululizo, kuna dalili kuwa mgogoro unaoendelea ndani ya chama cha CUF una

mkono wa serikali hasa kwa kuzingatia mwenendo wa ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

(taasisi ya serikali) kuibeba waziwazi kambi ya mwanachama aliyejiuzulu kwa utashi wake

Profesa Ibrahim Lipumba, ambaye alijiuzulu kwa hiari yake kabla ya kurudi chamani na kudai

yeye bado mwenyekiti wa taifa wa chama hicho cha upinzani.

Wiki chache kabla ya kuchapishwa kitabu hiki, Dokta Magufuli ‘alitoa siri’ kwamba kuna

siku aliombwa ushauri na Spika wa Bunge la Jamhuri, Job Ndugai kuhusu uteuzi wa wajumbe

Page 57: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

wa kamati moja ya bunge. Hiyo ina maana kuwa bunge limewekwa mfukoni na mhimili wa

serikali.

Kadhalika, kauli za Jaji Mkuu ‘mpya’ Profesa Ibrahim Hamis Juma baada ya jaribio la

mauaji dhidi ya Tundu Lissu yanajenga taswira ya mhimili wa mahakama nao kuwekwa mfukoni

na mhimili wa serikali.

Siku 15 baada ya Lissu kupigwa risasi na watu wasiojulikana, Jaji Mkuu aliitisha mkutano

na waandishi wa habari na kueleza kuwa mahakama haijalifumbia macho tukio hilo kwa kuwa ni

jambo ambalo litafikishwa mahakamani. Haikueleweka alikuwa na uhakika gani kama suala hilo

litafikishwa mahakamani ilhali hakuna juhudi zozote kwa upande wa vyombo vya dola kuwatia

nguvuni waliohusika na tukio hilo.

Jaji Juma alidai kwamba kwa mujibu wa kanuni jambo litakalofikishwa mahakamani kwa

ajili ya kutolewa ushahidi halipaswi kuongelewa au kutolewa maoni na kwamba tukio hilo la

Lissu litafikishwa mahakamani baada ya taratibu zote kukamilika.

Profesa huyo pia aliwataka wananchi wenye ushahidi unaohusiana na tukio hilo kuwasilisha

katika mamlaka husika badala ya kusambaza mitandaoni. Kwa tafsiri nyepesi, kauli za kiongozi

huyo wa mhimili wa mahakama zilikuwa kama zinazolenga kuwaziba mdomo wananchi

kuongelea suala hilo.

Lakini pengine cha kusikitisha zaidi ni ukweli kwamba hadi wakati kitabu hiki kinaandaliwa

kuchapishwa, Jaji Juma alikuwa hajaenda kumjulia hali Lissu, ambaye katika wadhifa wake

kama Rais wa TLS, ana mahusiano ya karibu kikazi na Jaji Mkuu.

Jambo jingine ambalo limetia doa miaka miwili ya utawala wa Dokta Magufuli ni uchaguzi

mdogo wa madiwani uliofanyika mwezi Novemba mwaka huu katika kata 43. Uchaguzi huo

utaingia katika vitabu vya historia kama uliotawaliwa na unyanyasaji, uonevu, vitisho na kila

aina ya uhuni dhidi ya vyama vya upinzani hususan Chadema.

Kana kwamba zuwio dhidi ya vyama vya upinzani kutofanya shughuli za kisiasa halitoshi,

kampeni za Chadema ziliandamwa na uonevu wa waziwazi uliofanywa na jeshi la polisi dhidi ya

viongozi, wagombea, mawakala na wanachama wa chama hicho.

Hadi wakati kitabu hiki kinaandaliwa kuchapishwa, kuna lundo la viongozi na wanachama

wa Chadema wenye kesi mbalimbali, nyingi kati ya kesi hizo zikiwa na dalili ya uhasama wa

kisiasa unaozidi kukua ndani ya CCM ya Dokta Magufuli dhidi ya vyama vya upinzani, hususan

Chadema.

Wakati wa kampeni zake za kuwania urais, na hata katika hotuba zake baada ya kushinda

urais, Dokta Magufuli amekuwa akimtaja sana Mungu, na kuwataka Watanzania kuendelea

kumwombea. Hilo ni jambo jema kwa sababu kiongozi mcha Mungu anakuwa katika nafasi

nzuri ya kuwatumikia anaowaongoza.

Hata hivyo, ‘ucha-Mungu’ wa Dokta Magufuli unashangaza kidogo kwa sababu wakati ni

ruhusa kwa wananchi kumwombea (kama anavywasihi mara kwa mara), serikali yake ilifikia

hatua ya kupiga marufuku maombi ya kiroho kwa ajili ya Lissu anayeugulia majeraha ya risasi

kufuatia jaribio la kumuuwa.

Japo Makamu wa Rais Samia na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi wamemtambelea mbunge

huyo wa Singida Mashariki, inaelezwa kuwa msimamo wa Dokta Magufuli kwa wabunge na

viongozi wa CCM dhidi ya ushirikiano na viongozi wa upinzani ni miongoni mwa sababu

zilizopelekea viongozi wengi wa chama hicho tawala kushindwa kumtembelea Lissu huko

Nairobi.

Kuna suala jingine ambalo japo halijaibuka waziwazi, linaweza kuzua maswali dhidi ya

utawala wa Dokta Magufuli. Suala hilo ni operesheni iliyoendeshwa na vyombo vya dola katika

Page 58: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Rufiji (MKIRU) ambayo yalikumbwa na mauaji mfululizo.

Serikali haijatoa taarifa rasmi kuhusu idadi kamili ya ‘magaidi’ waliouawa.

Hivi karibuni, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro alinukuliwa akieleza kuwa jumla

ya watoto 1,300 wa eneo la MKIRU hawajulikani walipo. Lakini cha kushangaza, mkuu huyo

wa jeshi la polisi aliwataka wazazi na walimu washirikiane kuwatafuta watoto hao. Watoto

ELFU MOJA NA MIA TATU watafutwe na wazazi na walimu?

Rekodi ya utendaji wa vyombo vya dola hata pale vinapopaswa kusimamia tu usalama

kwenye shughuli za vyama vya upinzani sio ya kupendeza. Kwahiyo kuna uwezekano kwamba

operesheni yao huko MKIRU ina mengi ambayo wananchi hawayafahamu japo ni haki yao

kufahamishwa.

Kwa upande mwingine, kumekuwa na manung’uniko japo hayajasambaa sana kuhusu dalili

za ukabila, ukanda na udini. Tangu aingie madarakani, Dokta Magufuli amezuru zaidi Kanda ya

Ziwa, eneo ambalo ni asili yake. Hata hivyo pengine ni mapema mno kumlaumu kwani bado

amekuwa madarakani kwa miaka miwili tu na bado ana takriban miaka mitatu kabla

hajahitimisha muhula wake wa kwanza.

Kingine kinachoongelewa kuhusu Dokta Magufuli ni hofu kuwa huenda akabadili Katibu

huko mbeleni ili aendelee kubaki madarakani. Japo yeye mwenyewe ameshaahidi kuheshimu

ukomo wa muda wa urais, ‘marafiki zake’ kama Rais Paul Kagame wa Rwanda na Yoweri

Museveni wa Uganda – wapinzani wakubwa wa ukomo wa muda wa urais – wanaweza

kumshawishi aendelee kubaki madarakani. Pengine kingine kinachochangia katika hofu hiyo ni

ukweli kwamba Dokta Magufuli ameweka msimamo wake bayana kuwa marekebisho ya Katiba

sio miongoni mwa vipaumbele vyake.

Sura hii ilijikita katika kuangalia upande mwingine wa Dokta Magufuli, mwanasiasa

aliyeingia madarakani wakati Tanzania ikiwa katika hali mbaya katika takriban kila nyanja,

akafanikiwa kurejesha matumaini ya Watanzania huko wengine wakimfananisha na Baba wa

Taifa Julius Nyerere, lakini tathmini ya miaka miwili ya utawala wake inaonyesha upande

mwingine usiopendeza.

Page 59: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Hitimisho

Kitabu hiki kimeandikwa kwa nia nzuri ya kutathmini utandaji kazi wa Rais Magufuli katika

kipindi cha miaka miwili tangu aingie madarakani. Mwandishi amekuwa akifuatilia kwa karibu

siasa za Tanzania, na kimsingi, kitabu hiki ni mwendelezo wa vitabu vingine viwili: kimoja

kilichoandikwa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 uliomwingiza madarakani Rais

Magufuli, na kingine kilichoandikwa siku 55 baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani.

Ni vigumu kufanya tathmini kwa kuangalia upande mmoja tu, na hilo lilikuwa kosa kuu la

kitabu cha pili cha mwandishi huyu ambacho japo pia kilikuwa kikifanya tathmini, kwa kiasi

kikubwa ilielemea kuangalia ‘mazuri’ tu. Lengo la kitabu hiki, kama ilivyokuwa kwa viwili

vilivyomtangulia katika mfululizo huu wa ufuatiliaji wa karibu wa siasa za Tanzania, si

kumchukiza au kumpendeza mtu flani,

Kwa vile kitabu kimeshaonyesha alikotoka Rais Magufuli, mchakato wa kuchaguliwa

kwake, siku za mwanzo za utawala wake na hali ilivyo miaka miwili tangu aingie madarakani.

Katika hitimisho hili, mwandishi anajaribu kueleza kwa kifupi kuhusu matarajio ya huko

mbeleni, na mustakabali wa Tanzania kwa ujumla.

Ndani ya CCM, Dokta Magufuli amefanikiwa kukamata hatamu za uongozi baada ya

kufanikiwa kufanya ‘mapinduzi ya mtu mmoja,’ kwa maana ya kuwezesha mabadiliko makubwa

ndani ya chama hicho peke yake, kwa kiasi kikubwa.

Moja ya mitihani mikubwa ya uenyekiti wake wa CCM Taifa ulikuwa kukabiliana na

makundi makubwa mawili: ‘masalia’ ya kambi ya Lowassa ndani ya chama hicho tawala na

wana-CCM wengine wenye nguvu katika chama hicho lakini ni wahanga wa sera mbalimbali za

Dokta Magufuli kama vile vita dhidi ya ufisadi.

Japo sio matumizi mazuri ya raslimali za taifa, taarifa zinaonyesha kuwa Idara ya Usalama

wa Taifa imekuwa na ufanisi mkubwa katika utekelezaji wa ajenda za Dokta Magufuli ndani ya

chama chake na serikalini.

Wakati CCM inaelekea katika hatua za mwisho za chaguzi zake za ndani, yayumkinika

kuhitimisha kuwa kiongozi huyo amefanikiwa kutengeneza mfumo aliohitaji katika kufikia

mageuzi ndani ya chama hicho. Na kama ilivyo serikalini, amefanikiwa kwa kiwango fulani

kurejesha nidhamu ndani ya chama hicho tawala.

Kumudu kufanikisha ajenda ya kutenganisha kofia mbili, yaani kiongozi wa chama asiwe na

majukumu mengine ‘full-time,’ kumemaanisha pia kwamba baadhi ya wanasiasa wenye nguvu

ndani ya chama hicho wamebaki wananachama wa kawaida tu licha ya baadhi yao kuwa na

madaraka makubwa serikalini.

Kwamba mabadiliko hayo yatakuwa na ufanisi kwa chama hicho itategemea mwelekeo wa

Dokta Magufuli ukoje. Na kwa hakika ni vigumu kubashiri kwa sababu kama sura mbili

zilizopita na hii zilivyoonyesha, kiongozi huyo sio mtu wa kutabirika kirahisi.

Mageuzi anayofanya ndani ya chama chake pia yanamaanisha kuwa nafasi yake ya

uenyekiti wa taifa wa chama hicho ipo salama, na licha ya utaratibu uliozoeleka wa rais aliyepo

madarakani kutopata mpinzani ndani ya chama hicho, nguvu kubwa aliyokwishatengeneza ndani

Page 60: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

ya CCM inamwondolea wasiwasi wa kuibuka upinzani dhidi yake katika kinyang’anyiro cha

kuwania tiketi ya urais kupitia chama hicho tawala.

Kwa upande mwingine, Dokta Magufuli anaendelea kunufaika na ‘sintofahamu’

inayovikabili vyama vya upinzani. Tukiweka kando ukweli kwamba vyama hivyo vinafanya kazi

katika mazingira magumu kutokana na kunyimwa fursa ya kufanya shughuli zake za kisiasa,

bado kuna kukosekana kwa dira kwa takriban vyama vyote vikuu vya upinzani.

Kwa upande wa Chadema, ukweli tu kwamba chama hicho kimeipa kisogo demokrasia kwa

kutofanya uchaguzi wake mkuu kwa miaka kadhaa sasa, inakiweka katika mazingira magumu ya

kufanya mabadiliko ya ndani ambayo ni muhimu kwa maendeleo na ustawi wa chama hicho.

Pamoja na mchango wake mkubwa kwa Chadema na siasa za upinzani kwa ujumla, lakini

kuna dalili zinazoashiria kuwa mwenyekiti wa taifa wa chama hicho Mbowe ‘ameishiwa pumzi.’

Haimaanishi aondoke madarakani lakini pengine apambane na changamoto mpya kutoka kwa

viongozi au wanachama wengine kupitia sanduku la kura, kwa maana uchaguzi mkuu wa chama

hicho.

Kwa kiasi kikubwa, Chadema imeshindwa kabisa kurudi zama zile ilipokuwa ‘mwiba’ kwa

CCM na serikali yake kutokana na kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Ajenda hiyo sio tu ilikifanya chama hicho kifahamike zaidi bali pia ilipelekea kikubalike

miongoni mwa Watanzania wengi kwani kilikuwa ‘msemaji’ wao, sambamba na kuonekana

mbadala wa kweli wa CCM.

Tangu kuisha kwa uchaguzi mkuu uliopita, Chadema kimekuwa zaidi chama cha kudandia

hoja kuliko kuanzisha hoja zake zenyewe. Hivi chama hicho kimeshindwa hata kulifanya suala la

kupotea kwa kada wake Saanane au jaribio la mauaji dhidi ya Lissu kuwa mijadala ya kitaifa?

Chama hicho kinapaswa kutambua kwamba kisipokuwa makini, kitakuwa katika wakati

mgumu kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020. Kwamba Dokta Magufuli ‘havipendi’ vyama

vya upinzani sio suala la mjadala, matendo yake yamejidhihirisha bayana. Kutarajia miujiza

kwamba labda atalegeza uzi ili vyama vya upinzani vifanye shughuli zake za kisiasa bila

bughudha ni ndoto ya alinacha.

Kama alivyosema aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dokta Willbrord Slaa,

mabadiliko ya kweli – kama ilivyokuwa ajenda kuu ya Chadema katika uchaguzi mkuu uliopita

– yataletwa na mikakati makini itakayotekelezwa na watu makini. Lakini kuilaumu tu CCM pasi

kufanya kitu mbadala kinachoweza kuwashawishi wananchi kuwa ‘hawa nafuu,’ hakuna ufanisi

wowote.

Mara kadhaa mwandishi wa kitabu hiki amekuwa akiwakumbusha wafuasi wa Chadema

kwamba ‘mabaya ya CCM hayamaanishi mazuri ya Wapinzani.’ Na kwa hakika, wapigakura

wanaweza kukubali kukivumilia chama kibaya lakini wanachokifahamu vema kuliko kukipatia

fursa ya majaribio chama ‘kizuri’ lakini kisichoeleweka kinasimamia nini.

Kubwa ambalo Chadema na vyama vingine vya upinzani vinapaswa kupigani ni Katiba

mpya. Kwamba Dokta Magufuli ameshaeleza kuwa Katiba hiyo sio kipaumbele chake, sio

sababu ya muhimu kukwaza jitihada za kudai Katiba mpya. Ikumbukwe tu ni jitihaza za

Chadema zilizoibuka suala la Katiba mpya kabla CCM hawajalipora na kulifanya ajenda yao.

Kadhalika, kama ilivyoelezwa awali, tangu kuanza kwa mfumo wa siasa za vyama vingi,

vyama vya upinzani vimekuwa vikifanya shughuli zao za kisiasa katik mazingira magumu, huku

takriban awamu zote za serikali za CCM zikifanya jitihada za kuvikandamiza vyama hivyo.

Mkazo mkubwa kwa vyama vya upinzani unapaswa kuwa kwenye kundi muhimu la wapiga

kura nchini Tanzania, yaani watu wasiojihusisha na chama chochote. Ni kwamba, CCM haihitaji

Page 61: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

kuwashawishi wanachama wake kuipa kura wala haijihangaishi sana na wanachama wa

upinzani. Walengwa wakuu wa kampeni za CCM huwa kundi hilo la watu wasio na vyama.

Ili kuweza kulishawishi kundi hilo, ni muhimu vyama vya upinzani vionekane vina cha

tofauti kulinganisha na CCM. Ugumu wa kukiondoa chama tawala madarakani huchangiwa na

hofu ya wapigakura kwamba ‘angalau huyu ni jini tunaye,mjua’ kwa maana angalau

wanakifahamu vema chama tawala pamoja na mapungufu yake. Kwa upande wa wapinzani,

huangaliwa kama ‘wageni’ fulani ambao hakuna mwenye uhakika iwapo wakiaminiwa

wataweza kufanya vitu tofauti na chama tawala.

Lakini pasipo Katiba mpya, hata kama vyama vya upinzani vitafanikiwa kumnasa kila

Mtanzania asiye na chama na kuwa na uhakika kuwa atavipigia kura vyama vya upinzani, pasipo

Katiba mpya itakuwa sawa na ‘kutwanga maji kwenye kinu.’ Kwahiyo jitihada za kupania

kuiondoa CCM madarakani sharti ziendane na jitihada ya kushinikiza kupatikana kwa Katiba

mpya.

Kwa upande mwingine, ni vigumu kuona mwana-CCM yeyote akijaribu kumshawishi Dokta

Magufuli kuhusu umuhimu wa vyama vya upinzani kwa siasa za Tanzania. Kuna dalili nyingi tu

za kuuangamiza upinzani hasa kupitia wimbi lililokuwa likiendelea wakati wa uandaaji kitabu

hiki, la viongozi mbalimbali wa upinzani kuhamia chama tawala.

Kwa vile Dokta Magufuli amefanikiwa ‘kupora’ sera ya vita dhidi ya ufisadi kutoka

Chadema, hakuna dalili zozote kwamba kukipa uhuru chama hicho cha upinzani, na vinginevyo,

kutamwathiri yeye binafsi au chama chake. Sana sana, ili kuepuka kupotea kwenye ramani ya

siasa, vyama vya upinzani vinaweza kuwa washirika muhimu wa Dokta Magufuli katika

utekelezaji wa sera mbalimbali kwa manufaa ya taifa. Siasa haipaswi kuwa uadui ilhali wote ni

Watanzania.

Kwa kumalizia kitabu hiki, pamoja na kusisitiza umuhimu mkubwa kwa serikali ya Dokta

Magufuli kuruhusu nafasi kwa vyama vya upinzani kufanya shughuli zake bila kubughudhiwa,

serikali yake pia ina wajibu wa kuwaelewesha Watanzania kuhusu jitihada mbalimbali

zinazofanyika katika kuiondoa kutoka katika mfumo wa uchumi wa kifisadi kuelekea uchumi wa

‘kila mtu atakula kwa jasho lake halali.’

Kwamba ili kufikia japo karibu na mahali Tanzania inapaswa kuwepo basi ni lazima

kutakuwa na machungu kadhaa ambayo ni lazima kuyapitia kabla ya kufika eneo kusudiwa.

Badala ya kuhangaika kuwahadaa wananchi kuhusu takwimu zinazoashiria kuwa uchumi upo

vizuri ilhali wao wanaoteseka, ni vema kuwa wakweli na kuwaelewesha wananchi kuwa hatua

zinazopitiwa ni lazima zitawathiri lakini kwa nia njema.

Kumwita ‘mpiga dili’ kila mtu anayelalamikia ugumu wa maisha sio kuwatendea haki

mamilioni ya wachapakazi wa Kitanzania ambao ufisadi pekee wanaofahamu ni ule unaofanywa

na vyama vya ushirika dhidi ya mazao yao.

Page 62: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala
Page 63: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Vitabu vingine vya mwandishi huyu

1. Uchaguzi Mkuu Tanzania 2015: Magufuli vs Lowassa

2. Dokta John Magufuli: Safari Ya Urais, Mafanikio Na Changamoto Katika Urais Wake

3. Afisa Usalama wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?

4. Makala Za Evarist Chahali Zilizovuma Magazetini: Toleo La Kwanza

5. Makala Za Evarist Chahali Zilizovuma Magazetini: Toleo La Pili

6. Mwongozo Wa Kitabibu Wa Jinsi Ya Kuacha Sigara Na Ushauri Wa Mvutaji Mstaafu

Page 64: Miaka Miwili ya Urais wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Auadelphil.com/wp-content/uploads/woocommerce_uploads/2018/01/Miaka... · maongezi, aidha kupitia maandishi ya kwenye makala

Ungana Na Mwandishi Mtandaoni

Ungana nami Facebook: http://facebook.com/evarist.chahali.1

Ungana nami Twitter: http://twitter.com/chahali

Ukurasa wangu Smashwords: https://www.smashwords.com/profile/view/Evarist

Blogu yangu: http://www.chahali.com

Nisikilize hapa (audio): https://www.spreaker.com/user/chahali


Recommended