Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
1
MAADILI YA KIKRISTO Maadili ni nini?
Maadili ni “Ni mpangilio wa kanuni bora
zinazotawala mwenendo wa kundi
maalum la watu.1” Fasili hii inamaanisha
kwamba maadili ni:
Kwa mujibu wa maana hii kumbe kila
kundi la watu lina kanuni zake
zinazotawala mwenendo mzima wa
kundi hilo. Kwa maana hiyo ni sahihi
kusema kuna maadili ya kikristo, maadili
ya kiualimu, maadili ya kiuongozi nk.
2maadili ni “maelekezo yanayofaa ambayo hutolewa kupitia wasilisho fulani.” Ukiangalia vizuri
zaidi fasiri hii utagundua kuwa mwandishi anakaza juu ya maelekezo yanayofaa, kwa maana
hiyo yale maelekezo yasiyofaa hayo siyo maadili.
Watu wengine hutumia neno ‘maadili’ kumaanisha mafundisho kuhusu ‘ukweli na uongo’ uzuri
na wema. Wengine wanasema kwamba maadili yanahusika na tabia za watu zilizo nzuri au
mbaya.
Kulingana na fasili hii tunaweza kupata maana moja ya maadili kwamba ni mpangilio wa kanuni
bora ambazo zimelenga kutoa maelekezo yanayofaa kwa ajili ya kundi fulani la watu katika
jamii husika.
Maadili ya kikristo ni mpangilio wa kanuni bora ambazo zimelenga kutoa maelekezo yanayofaa
kwa ajili ya wakristo. Wataalam wengine hudai kuwa Maadili ya Kikristo muhtasari wake
umetolewa na Wakolosai 3:1-6 : "Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo
juu Kristo aliko, ameketi mkon wa kuum wa Mungu. Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.
Kwa maan mlikufa na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. Kristo
atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu. Basi,
vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na
kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu3.
Huku zaidi ya orodha ya "kufanya" na ya "kutofanya ," Biblia inatupa maelekezo ya kina juu ya
namna tunapaswa kuishi. Biblia ndio kila kitu tunahitaji kujua kuhusu jinsi ya kuishi maisha ya
1 Kunhiyop, S.Y. (2008:). African Christian Ethics. Nairobi: Wordalive Publishers
2 Ndallu na wenzake (2014). Kamusi Teule ya Kiswahili Sanifu. NairobiL: EEP
3 www.gotquestions.org/Kiswahili/Maadili-ya-Kikristo.html
Na. mch. Daniel John Seni
Utangulizi
Maadili ya kikristo yamefupishwa katika kitabu cha Wakolosai 3:1-
6. Si kila kitu kiko wazi katika Biblia bali tunahitaji kusoma kwa
makini na kuweza kutumia katika maisha yetu ya kila siku. Kwa
mfano suala la madawa ya kulevya halijazungumziwa katika biblia
lakini tukiangalia madhara ya madawa ya kulevya tunaweza kujua
kwamba ni hatari kwa afya na hivyo kuharibu hekalu la Roho
Mtakatifu (1 Kor 6:19-20). Lakini pia Roho Mtakatifu aliye ndani
yetu aliye mafuta ndiye anatufundisha na hivyo tunaweza kujua
zaidi masuala ya kimaadili (1 John 2:27).
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
2
Kikristo. Hata hivyo, Biblia haifundishi kila hali ambayo sisi hukumbana nayo katika maisha
yetu. Ni jinsi gani sasa tunaweza kuamua hali kama hizo ambazo Biblia haiko wazi kihivyo
katika kuamua mambo? Hapa ndipo maamzi ya kikristo yanapokuja sasa kutumika!
Sayansi hudai maadili ni "seti ya kanuni za maadili, utafiti wa maadili." Kwa hiyo, maadili ya
Kikristo itakuwa kanuni inayotokana na imani ya Kikristo ambayo sisi hutenda. Wakati neno la
Mungu linaweza kukosa kuangazia kila hali sisi hupitia katika maisha yetu, kanuni zake
hutupatia viwango vya kujiendesha katika hali hizo ambapo hamna maelekezo ya wazi.
Kwa mfano, Biblia haisemi chochote kwa wazi kuhusu matumizi ya dawa za kulevya, lakini
kulingana na kanuni sisi hujifunza kwa njia ya maandiko, tunaweza kujua kwamba ni makosa.
Kwani Biblia inatuambia kwamba mwili ni hekalu la Roho Mtakatifu na kwamba tunapaswa
kumheshimu Mungu nao (1 Wakorintho 6:19-20).
Tunahitaji kujua wazi kwamba neno la Mungu halitoi kila hali ambayo sisi tunakumbana nayo
katika maisha yetu, Katika mambo mengi, tunaweza tu kuona ni nini Biblia inasema na kufuata
mwendo sahihi kwa kuzingatia kanuni hizo. Katika maswali ya kimaadili ambapo maandiko
hayatoi mwelekeo wa wazi, sisi tunapaswa kuangalia kanuni ambayo inaweza kutumika katika
hali hiyo. Tunapaswa kuomba juu ya neno lake, na kujiachilia sisi wenyewe kwa Roho wake.
Roho atatufundisha na kutuongoza katika Biblia kupata kanuni ambazo sisi tunahitaji kusimama
kwayo ili tuweze kuishi kama iwapasavyo Wakristo.
Maadili binafsi
Haya ni maadili yanayohusu mtu binafsi kwa kile ambacho anatakiwa kukifanya katika jamii.
Inahusu hasa na namna mtu anavyotakiwa kufanya kwa upande wake yeye kama yeye.
Maadili ya kijamii
Maadili haya yanahusu mwenendo mzima katika jamii. Katika nchi kama Tanzania mara nyingi
mkazo uko katika maadili ya kijamii kuliko maadili ya kibinafsi. Katika kufunza maadili
tunahitaji pia kujua maana ya maneno haya ili ya yatusaidie kujua zaidi mila na desturi za jamii
husika. Mara nyingi jamii zetu zinaongozwa na maadili ambayo yametawala kama mila na
desturi. Lakini swali la kujiuliza, je mila na desturi hizo ni nzuri? Tusichanganye maana ya
maadili na mila na desturi.
Tamaduni/Utamaduni: Ni desturi fulani za maisha zilizozoelewa au mila au ustaarabu.
Desturi ni kawaida ambazo jamii fulani inaona kuwa ni za lazima au ni jambo la kawaida
litendwalo na watu kila siku au ni ile hali ya mazoea. Desturi zinaweza kuwa nzuri au mbaya ili
mradi watu wamezoea hivyo!
Mila ni mambo yanayofanywa kulingana na chanzo na mazoea ya jamii asili.
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
3
Mila na desturi mara nyingi sana zinapingana na maadili ya kikristo. Wakati mwingine watu
unaweza kuwauliza kwa nini mnafanya hivi? Jibu watakalokwambia ni kwamba kwa sababu
tumekuta wazazi wetu wakifanya hivi, yaani mazoea! Mara nyingi mazoea yanaenda kinyume na
mwenendo wa kikristo. Wakristo wanaongozwa na neno la Mungu. Lakini hata katika neno la
Mungu wakati mwingine watu wanapofasili tofauti baadhi ya vifungu vya Biblia wanaibuka na
maana mpya na kupelekea kuwa na maadili tofauti tofauti ya kikristo. Kwa hiyo tunahitaji kujua
maana halisi katika kufasili baadhi ya vifungu vya kibiblia ili tuweze kufuata kile ambacho Neno
la Mungu limeagiza kuhusu maisha yetu kwa ujumla.
Kila jamii ina maadili yake lakini maadili ya kikristo ya pote! Si kwa watu wa sehemu fulani tu.
Kwa mfano hapa Tanzania tuna makabila zaidi ya 125 lakini ukiangalia kila kabila lina maadili
yake fulani ambayo yanaambatana na mila na desturi (ndani yake kuna miiko kadha wa kadha)
ndani yake lakini maadili ya kikristo yanahitaji kutumika katika hali zote katika makabila haya.
Tunahitaji pia kujua kwamba Biblia kama mwongozo wetu iliandikwa katika utamaduni wa watu
fulani, hata hivyo yapo mambo ya kitamaduni na mambo ambayo Biblia imekaza kama
mwongozo kwa kanisa. Jambo fulani inaweza kuliona jamii totauti na jinsi Biblia inavyolijadili.
Kwa mfano suala la kuacha mke/mume katika jamii nyingi za kiulimwengu ni jambo la kawaida
kabisa lakini Biblia inalijadili kwa upana zaidi.
Chanzo cha maadili ya Kikristo
Maadili ya kikristo chanzo chake kikuu Biblia. Biblia ndiyo kiongozi mkuu katika maadili ya
kikristo. Jamii inaweza kuliona jambo fulani kuwa ni zuri lakini Biblia ikaliona kuwa ni baya.
Kwa mfano suala la kuwa na Boy/Girl Friend na mkawa mnashiriki kimwili ni suala la kawaida
kabisa katika jamii yetu kwa leo lakini jambo hili kibilia linahesabika kama uasherati! Nadhani
katika jambo hili hakuna mjadala sana kwa sababu hakuna andiko lolote linashadidia dai kama
hilo katika maandiko. Kwa hiyo tunahitaji kujua Biblia inasema nini hasa katika jambo fulani
kuliko kuangalia jamii inasema nini.
Chanzo cha maadili yote ni Mungu mwenyewe. Kwa hiyo Mungu ndiye chanzo kikubwa cha
maadili. Mungu ameyafunua maadili hayo kupitia ufunuo wake. Tunajua wazi kwamba Mungu
amejifunua kwa mwanadamu kwa namna mbili; ufunuo wa kawaida/ujumla na ufunuo maalum.
1. Ufunuo wa Kawaida
Ufunuo wa kawaida ni ule ufunuo ambapo Mungu amejifunua mwenyewe kupitia asili, historia
na dhamira za watu. Zab. 19:1 inasema Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, na anga
laitangaza kazi ya mikono yake. Soma pia maandiko haya.Zaburi 147:8-9, Mdo 14:15-17, Rum
2:14-15, Rum 1:21. Nadhani baada ya kusoma mafungu haya umepata kitu pale kwamba Mungu
amejifunua kwa watu kwa namna ya jinsi alivyoumba vitu vyote duniani na kwa dhamira ndani
ya kila mtu. Ni dhahiri kwamba kila mtu anao ufahamu wa ndani kuhusu Mungu. Hakuna mtu
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
4
anayeweza kusema kwamba hakumjua Mungu kwa sababu Mungu ameweka ufahamu wake
ndani yako.
2. Ufunuo maalum
Mungu amejifunua katika ufunuo huu kwa njia ya Neno. Kwa nini ni ufunuo maalum? Kwa
sababu ni njia ya pekee kabisa ambayo Mungu ameitumia ili kujifunua kwa wanadamu, yaani
njia hii inaonyesha suluhisho la dhambi za mwanadamu kwa kumtuma Yesu KRISTO kama
Neno la Mungu halisi yaani lililo hai na kuwa kuwa mwili (Yn 1:14) “Neno akafanyika mwili,
akakaa kwetu” Ufunuo wa Mungu kwa njia ya Neno umegawanyika katika aina mbili:
2.1.Neno lililo hai
Neno lililo hai ni Yesu KRISTO mwenyewe aliyekuja kwa jinsi ya Mwili huku akiwa Neno
halisi yaani akiwa Mungu. Yohana 1:1,14. “hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno
alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu…naye Neno akafanyika mwili akakaa
kwetu”
2.2.Neno kama Biblia. Maandiko yote yameandikwa kwa msaada wa Roho Mtakatifu
(2Petro1:20-21) yaani wanadamu waliandika yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho
Mtakatifu (2Tim 3:16).
Katika kutafuta maarifa katika neno la Mungu tunahitaji kusoma kwa makini, kwa kuzingatia
kanuni za kisarufi na tafsiri ya neno la Mungu kwa wakati huo na wakati wa leo. Inashauriwa
unaporejelea Biblia uwe na usuli wa Biblia nzima. Huwezi kupata usuli huo bila ya kusoma
Biblia nzima. Inashauriwa kusoma Biblia yote ili kujua jambo fulani katika maandiko. Kwa
mfano ukisoma katika Agano la Kale peke yake unaweza kujikuta ukakubaliana na hoja
kwamba kuoa wake wengi ni sawa kwa sababu Biblia inasema hivyo jambo ambalo
linatakiwa liangaliwe katika Biblia nzima. Kwa hiyo kuwa makini kusoma fungu au mstari
mmoja katika Biblia na kutoa mahitimisho yake kwa haraka haraka. Hitimisho lolote lile
linalohusiana na masuala ya kimaadili lazima yafikiwe kama tu Neno la Mungu limeshadidia
suala hilo katika mawanda yake.
Kila unaposoma neno la Mungu lazima ukusudie kulitii na wala sio kwa kufuata mawazo
yako. Watu wengi sana hufuata mawazo yao badala ya neno la Mungu. Biblia katika Zaburi
119:11 inasema Moyoni mwako nimeliweka Neno lako nisije nikakutenda dhambi. Kwenda
kinyume na kile ambacho neno la Mungu linasema inaweza kusababisha wewe kutenda
dhambi hivyo unapolisoma uwe na lengo la kutii na kukubali matokeo yoyote yale
yatakayotokea.
Hata hivyo katika kutatua masuala ya kimaadili tunahitaji kuwa makini zaidi. Kwa mfano
katika maadili ya kikristo kutoa mimba ni kitendo kiovu ambacho ni dhambi kwa mtoaji
lakini je itakuwaje kama ujauzito huo ukiendelea kuwepo tumboni mwa mama inaweza
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
5
kupelekea kifo chake? Je atoe mimba ili kutunza mama
au mama afe na mtoto abaki? Haya ni baadhi tu ya
mambo ambayo yanahitaji kujadiliwa kwa makini sana
kabla ya kutolewa maamzi sahihi huku maadili ya
kikristo yakizingatiwa.
CHANGAMOTO ZA KIMAADILI
ZINAZOKABILI UKRISTO SIKU HIZI
Kuna changamoto za kimaadili nyingi sana ambazo
katika kitabu hiki hatuwezi kuzijadili kila moja. Ni
kweli kwamba katika Ukristo kila siku changamoto
mpya inazaliwa/inajitokeza. Sasa ni vigumu sana
kushughulikia changamoto hizi kwa muda wa siku nne
na hata kama tungepata muda wa kutosha si rahisi sana
kuzimaliza. Nadhani watu wanaoshughulika na masuala
ya ushauri wanajua ni mambo gani wanapambana nayo
kila siku. Unaweza kushangaa kila siku watu wanakuja
kupokea ushauri lakini kila mtu ana hoja yake ya pekee
kabisa. Hivyo basi kwa minajili ya kozi ya Biblia
nimechagua baadhi ya changamoto tu. Zifuatazo ni
changamoto za kimaadili kwa kanisa la leo
1. Masuala ya Siasa
Hatuwezi kujua zaidi kuhusu masuala ya siasa bila kujua kuhusu serikali. Serikali ni watu
waliochanguliwa kwa ajili ya kuwaongoza watu wengine. Kunhiyop (khj)4 anafafanua kuwa kazi
kubwa ya serikali ni kuwaadhibu wale ambao wanavunja sheria za nchi fulani. Sheria hizo
zinakuwa zimeandaliwa kwa ajili ya kuwaongoza watu wa makundi yote katika nchi. Yaani
hakuna cha dini fulani bali watu wa dini zote huunganishwa na kuwa wamoja kwa kutii sheria
moja. Serikali imetawaliwa na wanasiasa. Wanasiasa ndio wanaoshika nchi kwa sasa, bila siasa
hakuna serikali. Sasa kanisa linajikuta likiwa katikati ya siasa na kushindwa cha kufanya.
1.1. Kanisa na siasa
Kanisa wakati mwingine limekuwa katika changamoto katika siasa. Baadhi ya marais
wamekuwa wakitangaza hadharani upande wa dini wanaoushadidia. Katika historia kwa
mfano,mwaka 1991 raisi wa Zambia Fredrick Chiluba alitangaza kuwa Zambia ni taifa la
4 Khj-kirefu chake ni kama hapo juu au keshatajwa
Kanisa kwa sasa liko katika
hali ngumu kwa upande wa
maadili. Maadili
yanaendelea kumomonyoka.
Mfumko wa makanisa
duniani unatishia usalama
wa maadili ya Kikristo kwani
si jambo rahisi kwa sasa
kuamua katika hali ya
maadili. Hata hivyo sisi
kama watumishi wa Mungu
tunahitaji kujua masuala
mbalimbali ya kimaadili
ambayo yanatishia maadili
ya kikristo. Kwa ajili ya kozi
hii tutaangalia masuala
yafuatayo:
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
6
Kikristo.5 Huku akitubu kwa ajili ya uovu ambao umewahi kufanywa na watu wa taifa la
Zambia. Mfano mwingine ni raisi wa Nigeria, Obasanjo alidai kuokoka baada ya kufungwa kwa
makosa ya kijeshi. Katika kipindi cha uchaguzi alitangaza
kwamba yeye atakuwa raisi wa kikristo jambo ambalo
lilisababisha wakristo wengi kumpigia kura.
inawezekana kabisa mchungaji ukawa na kanisa halafu
ukaingia katika siasa? Je kanisa linaweza kutoa
mwongozo wa jinsi ya kuchagua kiongozi anayefaa katika
serikali?6Haya ni baadhi ya maswali ya msingi
tunapoendelea kujadili suala la siasa katika maadili ya
kikristo.
Katika maandiko serikali imeelezwa katika mazingira
kadha wa kadha. Ukianzia katika agano la Kale wakati wa
utawala wa Wafalme inadhihilisha wazi kwamba Mungu
alikubali tawala za wanadamu katika mazingira hayo.
kuna makundi mawili yanayozungumzia ujihusishaji wa
kanisa katika siasa. Kuna kundi la kwanza linadai kuwa ni
kanisa linapaswa kujihusisha kikamilifu katika siasa na
wale wanaokataa kwamba kanisa halipaswi kujihusisha na
siasa.
Hoja kwa wale wanaokubali
kujihusisha na siasa.
Wanaoshadidia upande huu
wanadai kuwa kila mkristo
lazima awe hai katika mambo
ya kiulimwengu. Wanadai
kuwa kanisa haliwezi kukaa
nje ya ulimwengu kwa sababu
linahitaji kuonyesha upendo
wa Mungu kwa watu wa
ulimwengu. Wanadai kuwa
bila kanisa kujihusisha na siasa
na pamoja na serikali wakristo
5 Paul Freston (2001). Evangelicals and Politics in Asia, Africa and Latin America. Cambridge: Cambridge University
press, Uk 158 6 Mwaka 2010 kanisa Katoliki liliandika ilani kwa washirika wake kuonyesha aina gani yakiongozi aweze
kuchaguliwa
Katika kipindi cha nyuma,
watumishi wengi wa Mungu
walikuwa wakiogopa sana
kuingia katika siasa kwa sababu
ya uovu ulio ndani ya siasa.
Huku wengine wakiwa na
misemo kwamba ‘siasa ni
mchezo mchafu’ swali la msingi
je wakristo wajihusishe na
mambo ya siasa?
Hoja za wanakataa kujihusisha
na siasa
Wale wanaoshadidia upande huu
wanadai kuwa kanisa limetengwa
kabisa na Yesu Kristo na hivyo
lenyewe si la ulimwengu huu.
Katika Yohana 17:16 “ninyi si wa
ulimwengu huu.” Warumi 12:2
inasema “wala msiifuatishe
namna ya dunia hii bali mgeuzwe
upya nia zenu mpate kujua hakika
yaliyo mapenzi ya Mungu yaliyo
mema ya kumpendeza na
ukamilifu.” Pia katika 2Kor 6:17
inasema “tokeni kati yao
mkatengwe nao asema Bwana.”
Kulingana na maandiko haya
wanaoshadidia upande huu
wanadai kuwa kanisa haliwezi
kujihusisha na mambo ya siasa
wala watumishi wake kuhusika
katika siasa kwa sababu wao ni
watu tofauti katika ulimwengu
huu.
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
7
hawawezi kuishawishi jamii kubadilika.kwa mfano katika Biblia akina Mordekai na Danieli
waliweza kubadilisha serikali zikawa za kumtii Mungu. Kwa upande mwingine wanakaza
kwamba kanisa halingii kichwa kichwa tu katika siasa bali linahusika na mambo ya siasa kwa
namna ifuatayo:-
i. Kuombea serikali na watu wake kwa ujumla
ii. Kuikosoa serikali kama inaenda kinyume na maadili yanayotakikana
iii. Kushirikiana na serikali katika kuondoa maovu katika nchi
Kambi hii pia ina misingi mingine kutoka katika maandiko ikidai kwamba:
i. Serikali inaanzia kwa Mungu Mwenyewe. Rom 13:1
ii. Serikali hufanya kazi kwa niaba ya Mungu. Rom 13:4
iii. Serikali ipo kwa ajili ya kuhamasisha mazuri kufanyika. Rum13:4-5.
Kwa minajili ya kozi hii nakubaliana na kambi pili kwamba kanisa linaweza kujihusisha na
siasa. Kanisa lijihusisha katika siasa ili kupata nafasi katika masuala ya kiuchumi, kijamii na
kiafya. Kama kanisa likipata nafasi kama hizo ndani ya kanisa basi ufalme wa Mungu hapa
duniani utaendelea kuinuliwa zaidi na zaidi.
Maswali la mjadala:
1. Je mchungaji anaweza kugombea uongozi katika siasa, kwa mfano ubunge huku akiendelea
kuongoza kanisa? Kubali au kataa kwa hoja kuntu.
2. Tunawezaje kukemea viongozi wanaofanya maovu zaidi katika nchi zetu zinazoendelea? Je
unaweza kumkabili raisi kama amefanya ubaya?
3. Kama tukikubaliana kwamba serikali zote zinatoka kwa Mungu, je unasema nini kuhusu
serikali za kijeshi ambazo wakati mwingine huua umati wa raia wasio na lawama?
4. Msimamo wako ni upi kuhusu kanisa na siasa? (hakikisha unatumia maandiko)
1.2.Vita na maasi
Suala la vita na maasi linahitaji mjadala mkubwa sana. Kuna watu wengine wanaodai
kwamba mkristo haruhusiwi kujihusisha na vita vya aina yoyote ile isipokuwa vita vya
kiroho tu. Lakini wengine wanadai kwamba wakristo wanaweza kwenda kwenye vita ili
kusaidia kukomboa katika vita.
1.2.1. Vita katika agano la kale
1.2.1.1.Waisrael waliagizwa kuwafukuza Wakanaani kwa vita ( Hes 33:50-56)
1.2.1.2. Mfalme Sauli aliagizwa kuwaua Waamaleki kwa vita (Isam.15:2-3)
1.2.1.3. Mungu ni mtu wa vita nk
1.2.2. Vita katika agano jipya
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
8
1.2.2.1.Kununua panga. Luka 22:36-38
1.2.2.2.Ufalme wa Yesu sio wa dunia hii ( Yoh. 18:36)
Kanuni za kutumia kunapotokea vita kati ya wakristo na wasio wakristo
1.2.3. kutafuta suluhu kila inapowezekana. Math 26:52
1.2.4. kuhamasisha haki duniani
1.2.5. Kuondoa ukabila ndani ya kanisa (Gal 3:28)
1.2.6. Upendo na msamha kwa maadui
Swali la mjadala
Je mkristo anaweza kwenda katika vita? Kama anaweza kwenda ni kwa namna gani
anaweza akatunza amri inayosema usiue? Jadili kwa hoja maridhawa.
B. Masuala ya Kiuchumi
Uchumi ni kipengele kingine muhimu katika kanisa la leo. Kuna mambo mengi yanayohusiana
na masuala ya kiuchumi ambayo yaliyo mengi yanahitaji mwongozo wa kimaadili. Yafutayo ni
baadhi ya mambo hayo:-
2.1. Umaskini
Suala la umasikini katika jamii nyingi za kiafrika ni suala tete. Watu wengi wengi wanahangaika
kwa sababu ya maisha magumu. Wakati mwingine wanakosa hata mavazi, malazi na hata
chakula. Lakini je ni mapenzi ya Mungu watu kuwa maskini? Nafikiri sio mapenzi ya Mungu
bali ni matokeo ya dhambi, na kwa sababu hiyo Mungu aliamua kuweka utaratibu wa namna ya
kutoka katika hali ya umasikini. Wakati Mungu alipomuumba mwanadamu alikusudia aishi
maisha tele lakini anguko limesababisha matatizo makubwa sana katika jamii zetu. Lakini swali
la msingi,je kwa nini nchi nyingi za kiafrika ni maskini sana kuliko za Ulaya? Je madhara ya
anguko yako kwetu tu? Kwa nini hali ya maisha ni tofauti kiasi hicho? Je matajiri wamewaibia
maskini mali zao? Je nini maadili ya kikristo katika jambo hili?
Je Mungu amepanga umaskini kwa watumishi wake? kwa nini tunahangaika na
umaskini? jadili
2.3.Rushwa
Siku hizi watu hujaribu kupunguza ukali wa neno ‘rushwa’ ‘hongo’ kwa kusema; zawadi,
hongera, maji, chai nk. Watu wengi hutoa na kupokea rushwa kwa namna tofauti tofauti.
Wengine hudai ni shukrani tu, wengine hudai ni mshahara kwa kazi yangu na wengine hudai ni
haki yangu kupokea rushwa. Ili rushwa iitwe rushwa mazingira ya utoaji wake yanahitaji
yaangaliwe. Kazi ya rushwa ni kununua haki
Biblia imekataza kupokea rushwa ya aina yoyote ile na kwa mazingira yoyote yale. (soma
mafungu haya Kumb. 10:16-18, 2Nyak 19:7, Mhub. 7:7, Zab 62:10) nk
Swali la mjadala: 1. Je unakubaliana na msemo kwamba “rushwa haiepukiki katika jamii
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
9
yetu?”
Tuchukulie unaendesha gari, unasimamishwa na trafiki na gari lako linaonekana lina kosa
dogo tu la rangi kuchubuka. Na asikari anakuomba faini ya shilingi 30.000/= hapo hapo
anakwambia ‘hebu naomba unipe ya maji nikuache uende na safari zako, leta 2000/- ‘ je
utakubali kumpa? Kama utakubali toa hoja madhubuti na kama hautakubali toa hoja kuntu.
1.3. Harambee/fund rising
Harambee au kwa lugha nyingine ‘changizo’ ina asili yake. Jamii nyingi za kiafrika zina
utamaduni wa kusaidiana kwa pamoja kama kazi inahitaji watu wengi. Hiyo nayo tunaweza
kusema kuwa ni aina fulani ya harambee. Kila kabila lina aina yake ya kufanya harambee; kwa
mfano katika jamii ya wasukuma kuna maneno maalum yanayotumika kuelezea harambee ya
aina hiyo kwa mfano ‘lubili’ ‘buyobe’ ‘ikhuma lya busiga’ nk. Kwa Wakulya wanasema’irika.’
Kwa hiyo suala la harambee si suala geni katika jamii nyingi za kiafrika. Watanzania wana
msemo ‘umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu’
Changizo au kufanya kitu katika hali ya umoja ni jambo la kawaida katika ukristo. Katika biblia
kuna sehemu nyingi ambapo changizo liliweza kufanyika kwa ajili ya kuinua huduma fulani
iendelee kwa nguvu.
a) Musa alifanya harambee kwa ajili ya ujenzi wa hema. Kut. 20-34
b) Mfalme Daudi alifanya harambee kwa ajili ya ujenzi wa hekalu. INyak. 28:12, 19. 29:2-9
c) Nehemia alifanya harambee kwa ajili ya kurekebisha mji wa Yerusalemu. Neh. 1:4-11,
2:1-18; 3:1-5 nk (au soma kitabu chote cha Nehemia)
d) Ezra alifanya harambee kwa ajili ya ujenzi wa hekalu. Ezra 2:68-69
e) Hagai naye katika huduma yake alifundisha watu kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu.
Hag. 1:1-14
f) Yesu pia alihudumiwa katika huduma yake na wanawake kadha wa kadha. Luka 8:1-3
g) Mitume nao walihitaji fedha kwa ajili ya kuendeleza huduma yao. Mdo. 4:32-5:11
h) Mtume Paul alifanya changizo kwa ajili ya huduma. I Kor 16:1-3, 2Kor 8:1-24
Swali la msingi ni kwamba kwa nini suala hili liko katika maadili ya kikristo?
Kwa kuwa ni muhimu katika huduma ya BWANA kuwa na changizo la watu wengi, au mtu
mmoja/supporter, au kanisa maalumu linaweza kukusapoti lakini bado kuna mambo ya kimaadili
ambayo yanahitaji kuzingatiwa katika upataji wa huduma hizo. Mambo yafuatayo yanahitaji
kuangaliwa kwa makini sana katika huduma
a) Kuomba msaada kwa wasio wakristo
Swali ambalo mara nyingi tunapaswa kujiuliza ni je tunaweza kwenda kuomba msaada
wa kifedha labda kwa ajili ya kujenga kanisa kwa watu wasio waamini? Je mtu ambaye
pengine tunajua wazi kwamba labda amepata fedha kwa njia ya rushwa/au jambo lolote
lile baya, je tunaweza kuzipokea fedha kama hizo? Je tunaweza kuwaendea Waislamu
matajiri na kuwaomba wachangie huduma zetu?
Maswali haya yote yanahitaji uchunguzi wa hali ya juu sana. Wengi wanaoshadidia
upande wa kwamba inawezekana kuchukua fedha kwa wasio waamini wanadai kwamba
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
10
fedha walizo nazo watu sio za kwao. Wanatoa mfano wa Ezra na Nehemia waliopokea
msaada wa mfalme wa Babel ambaye alikuwa mwabudu miungu. Hili ndilo suala la
kimaadili katika harambee!
b) Kutangaza fedha zilizotolewa katika harambee au kama ni msaada wa mtu.
Hii inatokea hasa kama katika changizo umeita MC anayejulikana kabisa. Anahamasisha
watu na watu wanatoa fedha nyingi. Je fedha hizo zitangazwe?
c) Mhubiri kuomba fedha ili aje kufanya kwenye mkutano
Hili nalo siku hizi linasumbua sana jamii za Kikristo. Watumishi mbalimbali wanaomba
fedha kabla ya kufika katika mkutano wa Injili. Waimbaji wengi wa injili siku hizi bila
kuweka chochote kwenye akaunti yake hawezi kwenda kwenye mkutano wa Injili. Je
hayo ni maadili ya Kikristo. Je ni maadili ya kikristo kutoa namba zako za akaunti za
benki kwa umati wa watu? Je ni sawa kwa mtu akitaka kuombewa atoe kwanza fedha
kwa ajili ya huduma hiyo? Haya ni baadhi ya maswali ya msingi ambayo tunahitaji
kujiuliza na kuyatolea majibu sahihi.
Watumishi wa Mungu tunahitaji kuwa makini katika masuala haya ya kimaadili. Lakini
kwa ujumla tunaweza kusema kwamba, mambo yafuatayo katika masuala ya kifedha
katika huduma yanapaswa yafuatwe:-
Angalia nia ya mtoaji ni ipi? Kama ni ya kisiasa zaidi au anataka kumteka
mchungaji/mwinjilisti au anataka kupata sifa fulani ndani ya kanisa hilo? Usipokee fedha
ovyo ovyo maana ni hatari sana!
Kwa wewe unayepokea lazima uwe mwaminifu na muwazi. Kama umepewa fedha kwa
ajili ya kujenga kanisa unapaswa kujenga kanisa tu. Kuna wachungaji wengi wakishapata
misaada ya aina hiyo tayari wanaibadilishia matumizi, wananunua magari nk. Jambo hili
ni hatari sana.
Kuwepo na mrejesho kwa kile ulichotumia. Ni vizuri zaidi kuelezea vizuri kile ambacho
umetumia. Ikiwezekana andika kila kitu, itakusaidia sana maana kuna wafadhili wengine
wanataka kujua kila kitu.
Baada ya kuangalia mambo ambayo ni ya muhimu; epuka mambo yafuatayo:-
Epuka kupotosha ukweli. Kama una mradi utagharimu shilingi laki tano sema laki
tano.
Epuka kuwashawishi watu kutoa hata pale wasipotaka kutoa. Kuna watu
makanisani wanatoa vitu huku wakinugh’nuka mioyoni mwao
Epuka kuwa ombaomba/ Mungu hasemi kwamba tuombe kwa watu.
C. Masuala ya familia na ndoa
Suala la familia na ndoa ni suala ambao linahitaji kujadiliwa kwa undani zaidi. Ndoa ni taasisi
pekee ambayo Mungu huitumia kuendeleza uumbaji wake hapa duniani. Lakini wakati mwingine
ndoa hizi hizi zinakuwa na changamoto nyingi ambazo zinapelekea mambo fulani fulani ambayo
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
11
sio mazuri kutokea katika maisha ya kila siku. Katika sehemu ya familia na ndoa tutaangalia
masuala ya utasa, mitara, talaka na mahusiano.
3.1. Utasa/Ugumba
Utasa katika nchi nyingi za kiafrika ni suala mtambuka. Kwa maana ya kwamba waafrika
wanaamini kwamba watoto ndio urithi wa pekee kabisa. Sasa inapotokea kwamba kuna tatizo la
utasa mambo haya yanakuwa ni shida kubwa. Watu wengi wametoa talaka kwa sababu ya
kutokupata watoto kwa wake zao wa kwanza. Watu wengi wanaamini kwamba ndoa bila kuwa
na mtoto bado haijawa ndoa sahihi bali ni ndoa nusu. Tunahitaji kujifunza na kujua mapenzi ya
Mungu nini katika maisha ya ndoa zetu. Kama tukikaza kwamba lazima tuwe na watoto je
inapotokea hakuna watoto inakuwa ni laana au? Watu wengi wanatembea usiku na mchana
kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kutafuta watoto. Lazima tuwe makini katika
jambo hili. Kuna wachungaji wengi ambao wamejikita katika huduma ya kuombea tu watu wasio
na watoto huku wakikaza kwamba mtu asiyekuwa na watoto ana laana kutoka kwa Mungu na
yeye anaondoa laana hizo.
Chanzo cha utasa/ ugumba
Kabla ya kwenda mbali zaidi hebu tuangalie maana ya utasa na ugumba. Kwa mujibu wa kamusi
ya Kiswahili sanifu (2004:398)7 tasa ni “kiumbe chochote cha kike kisichoweza kuzaa” kwa hiyo
tunapozungumzia tasa tunamaanisha mwanamke asiyeweza kuzaa. Neno ‘mgumba8’ maana yake
ni “mtu aliyefikia umri wa kuzaa lakini akawa hajazaa wala kupata au kutia mimba” kwa hiyo
neno ugumba ni kwa watu wote. Sasa tuangalie kwa ufupi sababu za kuwa mgumba kwa:-
Kwa wanaume
Uhanithi-huyu ni mwanaume asiyekuwa na nguvu za kiume kabisa, yaani ni dhaifu.
Uume wake hauwezi kusimama sawasawa na hivyo hawezi kufanya mapenzi na mke
wake. tatizo hili husababishwa na masuala ya kiafya,kwa mfano kupiga punyeto kwa
muda mrefu na hata masuala ya kisaikolojia. Kama mtu akiwa na tatizo hili tunawashauri
kwenda kupima hospital ili kubaini chanzo cha tatizo.
Swali: wewe kama mchungaji ukiletewa suala la mtu ni kuwa
hanithi utafanyaje ili uweze kunusuru ndoa yao? Utawashauri vipi?
Tatizo katika kutoa mbegu- wanaume wengine hawawezi kuwapa wake zao uja uzito kwa
sababu shahawa/mbezi zao haziwezi kufikia yai la mtoto. Yaani katika kutoa
mbegu/shahawa hazina spidi ya kufikia yai.
Kukosekana kwa mbegu katika shahawa-wanaume wengine hawana mbegu katika
shahawa zao. Wanamwaga shahawa kama kawaida lakini hazina mbegu. Hili nalo ni
tatizo kubwa.
7TUKI (2004). kamusi ya Kiswahili sanifu. Nairobi: Oxford
8 khj
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
12
Kuharibika kwa mbegu za kiume-wakati mwingine mbegu za kiume zinaharibika na kufa
kabisa. Wanaume wengi wanaopenda kuvaa chupi zinazowabana hupatwa na tatizo hili
mapema sana. Maana kwa kawaida mbegu haziwezi kukaa katika joto kali.
Matatizo ya kiroho, wakati mwingine masuala ya kiroho yanaweza kusababisha kuwa
mgumba mwanaume
tafuta sababu za kiroho za ugumba katika maandiko matakatifu
kisha yaelezee kwa undani na chanzo cha matatizo hayo.
Kwa wanawake
Wanawake wengi wanakuwa matasa kwa sababu zifuatazo
Tatizo la homoni za uzazi
Tatizo la tumbo la uzazi/hakuna kizazi
Maambukizi katika uke
Chango la kike
Tatizo kiroho
Namna ya kushughulikia ugumba/utasa
Kila kundi la watu lina namna yake ya kutatua tatizo hili kubwa katika jamii. Jamii
nyingi zisizoamini hukimbilia kwa waganga wa kienyeji na kujikuta wanagawa ngono
kwa kudanganywa ili wapate watoto. Wanaume wengine wanaambiwa mashariti
magumu. Kwa mfano jamaa mmoja alienda kwa mganga wa kienyeji akaambiwa
kwamba alale na mama yake mzazi ndipo kizazi cha mke wake kitafunguka. Kwa ushauri
wangu ni bora:-
Kumwomba Mungu sana na kutambua nini hasa kusudi la ndoa katika maisha yenu.
Kwenda kuwaona wataalamu wa afya ili waone suala hili kitabibu zaidi. Na kama hakuna
tatizo la kitabibu basi ni vizuri kusubiri mpango wa Mungu
Kujifunza namna ya kujua siku ambazo mwanamke anaweza kuchukua mimba au la
Kujua kusudi la Mungu katika uumbaji. Kila kitu kinachokuja duniani kinakuwa na kusudi
la Mungu katika maisha ya mwanadamu. Kwa mtu aliyeokoka si jambo la kulazimisha
upate mtoto wakati Mungu hajaamua kufanya hivyo. Usije ukachanganyikiwa na kuanza
kukimbilia maombezi kila kukicha
3.2. Mitara (ndoa za wake wengi)
Waafrika wengi hawaoni kwamba ni jambo geni kuingia katika ndoa za mitara. Hii ni kutokana
na ukweli kwamba mwanaume wa kiafrika anaweza kuoa mwanamke mwingine wakati wowote
ule bila shida. Hili nalo ni tatizo kwa wakristo wengi. Nakumbuka kanisa moja niliwahi kusali
nilipokuwa kijana mdogo lililoitwa Last Church/Batola mhali (kwa kisukuma) lilikuwa
linahalalisha kabisa kuoa wake zaidi ya mmoja. Mwinjilisti kanisa hilo alikuwa na wake wawili
Ada na Sila. Kuna siku waligombana sana hao wake zake na kubebeana mapanga na hapo hapo
ndipo kikawa chanzo cha familia yetu kuhama kanisa hilo!!
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
13
Mpango wa Mungu haikuwa kwamba mwanadamu aweze kuoa wake wengi, kwani
alipomuumba Adamu alimwomba na Hawa nao walikuwa wawili tu. Hata hivyo kwa sababu ya
anguko la mwanadamu, kwa sababu ya dhambi mwanadamu alijitwalia wake zaidi kwa kadri
alivyotaka. Hebu tuangalie ndoa za mitara katika biblia na madhara yake.
Ndoa ya Lameki Mwanzo 4:19-25
Huyu ndiye mtu wa kwanza kabisa kujitwalia wake wawili. Ukisoma mistari hiyo utaona
kwamba huyu jamaa alikuwa roho ya kisasi kama ya Kaini. Kwa hiyo moja kwa moja makosa
yake yanaelekezwa kwa uasi aliokuwa nao. Matokeo yake yeye mwenyewe anakiri kwamba
anaweza kulipizwa kisasi na Mungu. Hapa tunaona kwamba madhara yake ilikuwa kwenda
kinyume na Mungu.ukoo wa Kaini mara nyingi imeonekana katika maandiko kwamba ni ukoo
wa kigaidi uliokataa kwenda katika sheria ya Mungu.
Ndoa ya Ibrahimu Mwanzo 16-17 na 28-30
Ni dhahiri kwamba Ibrahimu alizaliwa katika familia yenye kushika msimamo wa ndoa za wake
wengi(20:12). Katika ndoa yao Ibrahimu alichelewa sana kupata mtoto wa ahadi, lakini mke
wake Sarah,kwa sababu tayari ndani yake yalikuwepo mawazo ya kuwa na wake wengi kwa
mume wake,alimshauri amchukue Hajiri. Hapa ndipo chanzo cha matatizo ya ndoa hii.
Katika agano jipya hakuna mahali popote ambapo tunakuta kuna mtu alikuwa na wake zaidi ya
mmoja. Lakini tukiangalia maandiko inaonekana kwamba kuna waliokuwa na wake zaidi ya
mmoja. Hebu soma mafungu haya (I Kor 5:1-9) hapa tunaona jamaa ambaye alikuwa ni mzinzi
kiasi cha kulala na mke wa baba yake, je wewe unadhani ni mama yake mzazi? Labda nafikiri
kwamba huyu baba yake alikuwa hawara/nyumba ndogo. Sio hapo ukisoma katika I Tim 3:1ff
utaona sifa za asikofu na shemasi kwamba wawe waume wa mke mmoja. Hii inatudhihilishia
kwamba kulikupo na watu ndani ya kanisa wenye wake zaidi ya mmoja.
Maandiko hakuna sehemu ambapo yameruhusu mwanaume kuoa wake wengi au mwanamke
aolewe na wanaume wengi, kinachofanywa na binadamu ni ugumu wa mioyo yao. Wengine
katika kipindi hiki kwa sababu ya changamoto za ndoa wanaamua kuwa na nyumba ndogo ili
kunusuru maisha yao. Hii ni hatari sana, kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na neno la
Mungu.
Kwa kawaida hakuna mtu anayeweza kugawa upendo wake katika sehemu mbili. Na ndiyo
maana ndoa za wake wengi zinakuwa na matatizo mengi sana. Unakuta wanawake hao
hawaelewani kila siku. Kuna mifano mingi katika agano la kale ambayo inaonyesha madhara ya
ndoa za mitara. Ushauri wangu ni kwamba ni lazima tufundishe watu wafuate utaratibu wa
Mungu kwamba ndoa ni ya mke mmoja. Hakuna sababu ya kuoa mke wa pili. Na kuoa mke wa
pili ni kwenda kinyume na neno la Mungu.
Swali: je kama kanisani kwako kuna waumini ambao kabla ya kuokoka walikuwa na
wake zaidi ya mmoja, utawashauri wawaache au utafanyaje? Jadili kwa mapana huku
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
14
ukizingatia maadili ya kikiristo ni pamoja na hekima ya Roho Mtakatifu kufanya kazi
Wewe kama mchungaji umeitwa kwenda kumbatiza mtu aliye na wake zaidi ya mmoja utafanyaje?
3.3. Talaka
Suala la talaka ni suala nyeti sana katika kanisa. Watumishi wengi wanahangaika kutatua
masuala yanayohusiana na talaka. Katika kipindi hiki suala la talaka ni jambo la kawaida
miongoni mwa wapendwa. Hasa kunapokuwa na tatizo ambalo wanandoa wamekosana na jamii
pamoja na kanisa inaliona wazi basi talaka hutolewa.
Nini sababu ya talaka?.
Kwa ujumla kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha talaka kutolewa. Nitajaribu kutaja baadhi
ya hayo matatizo kama ifuatavyo;-
Kukosekana kwa watoto miongoni mwa wanandoa ni sababu kwa Waafrika. Na hasa
lawama zinapelekwa kwa wanawake
Kusalitiana kimapenzi, yaani kama kuna mmoja anatoka nje ya ndoa basi yule mwingine
anaamua kuachana naye
Kulazimishwa na wazazi wa upande mmoja kuachana kwa sababu za kimila na kitamaduni
Mmojawapo wa wanandoa hao kupatwa na magonjwa ya kuambukizwa hasa UKIMWI
Sababu za kiuchumi katika wanandoa. Wengine wanapooana huonekana wakiwa na mali
mara baada ya kuisha mali hizo huachana mara moja
Huko Ulaya wengine wanaona kwamba kama mtu amemchoka mwenzake anaamua
kuachana naye tu bila hata sababu za msingi
Ugomvi wa mara kwa mara ndani ya nyumba hupekea talaka kwa wanandoa hao. Ugomvi
huo unaweza kusababishwa na tabia sugu za wanandoa hao kutokubadilika ili kuendana
pamoja.
Matumizi ya mabavu ndani ya nyumba husababisha talaka miongoni mwa wanandoa. Kwa
mfano kwa waafrika walio wengi kumpiga mwanamke ni jambo la kawaida sana, lakini
kuna wakati inafikia hali ngumu ndipo mwanamke huamua kuondoka na kudai talaka. Ni
mara chache kukuta familia mwanaume anapigwa na mwanamke japo kuna familia za
namna hii nyingi.
Kunyimana kitandani. Nazungumzia hapa ile hali ya kumnyima mwenzi tendo la unyumba
hupelekea talaka miongoni mwa wanandoa. Hii inatokea pale ambapo miongoni mwa
wanandoa anatoa tendo la ndoa kama silaha ya kumwadhibu mume/mke wake. jambo hili
huvunja ndoa nyingi kila siku.
Wivu wa kimapenzi huvunja ndoa nyingi, unaweza kukuta miongoni mwa wanandoa
anakuwa na wivu kiasi kwamba hataki kumwona mwenzi wake anaongea na mtu mwingine.
Mfano unakuta baba akimwona mke wake ana mtu mwingine wa kiume basi moja kwa moja
anasema kwamba huyu anakutongoza na hivyo kudai talaka kwa haraka sana.
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
15
Ndoa za mitara huvunja ndoa ya kwanza. Mara nyingine kwa wapenzi ambao
hawakukusudia kuwa ndoa yao itakuwa ya wake wengi wakiona kwamba kuna mwanamke
mwingine ameletwa ndani mara moja hudai talaka.
Ulevi wa kupindukia, hili mara nyingi linatokea hasa ikiwa mmojawapo wa wanandoa hao
akiwa mlevi kupindukia na mwingine hana tabia za ulevi ikifikia hatua fulani mmoja
anachoka kumvumilia mwenzake kwa ajili ya ulevi wake basi huamua kuvunja ndoa
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yanasababisha ndoa nyingi kuvunjika. Kwa mfano
matumizi mabaya ya simu yanavunja ndoa za watu. Nakumbuka kijana mmoja alikosea
akatuma massage ya mapenzi katika simu ya mke wa mtu, ujumbe huo ulileta mtafaruku
ndani ya ndoa hiyo. Pia matumizi ya mitandao ya kijamii kama vile facebook na twitter
yanasababisha kuvunjika ndoa. Pale ambapo mmoja wa wanandoa anasahau ku-log out
kama alikuwa ameingia mtandaoni na mtu mwingine mbaya akiingia kwenye akaunti yake
na kuweka picha mbaya itampa shida kubwa sana.
Watoto wa kambo huvunja baadhi ya ndoa za watu. Hii inatokea pale ambao mmoja wa
wanandoa hao alikuwa na mtoto wakati wa kuolewa, watoto wa aina hiyo wakati mwingine
huleta matatizo makubwa ya kuchonganisha wanandoa hao
Hizi ni sababu chache tu miongoni mwa sababu nyingi zinazosababisha kuvunjika kwa ndoa. Na
kumbuka kwamba kila ndoa ina sababu yake ya pekee ambayo haifanani na nyingine
inayopelekea kuvunjika kwa ndoa hiyo.
Fungu la kwanza ambalo linazungumza juu ya talaka kwa mara ya kwanza ni katika
Kumbukumbu la Torati 24:1-5 mahali ambapo tunaona kwamba Musa aliwaelekeza watu namna
ambavyo wanaweza kuwapa talaka wake zao. Lakini jambo hili Yesu alisema kwamba sababu za
Musa kuruhusu talaka ilikuwa ni ugumu wa mioyo ya watu
Mitazamo mbalimbali kuhusu talaka
Kuna wanaosema hakuna kutoa talaka kabisa katika maisha ya mwanadamu. Soma
Warumi 7:2-3,I kor 7:39, Mal 2:16
Kuna wanaosema kuwa ni ruksa kutoa talaka lakini usioe tena. Hawa nao wanasimama
na mafungu mbalimbali, mfano. Math 19:9 wanafafanua kwa namna ya pekee sana
Kuna wale wanakubali kwamba kama mwanamke/mwanaume umemkamatisha kwenye
uzinzi unaachana naye mara moja. Nao wanasimama na fungu hili la Math 19:9 na Kumb
24:1-5 wakifasiri neno OVU kuwa ni uzinzi
Kila kundi la watu wana msimamo wao juu ya suala hili lakini cha kuzingatia ni kwamba
tunahitaji kumwomba Mungu hekima ya pekee katika kujadili suala la talaka makanisani
huku tukijua mambo yafuatayo:-
Ndoa ya kikristo imekusudiwa kuwa ni ya milele. Mal 2:16
Kuna wakati inaweza kutokea talaka. Math 19:8
Talaka ni hatari sana kwa wanandoa
Hatuwezi kujumuisha moja kwa moja masuala ya talaka lazima yaangaliwe kwa
undani zaidi
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
16
Kuna matumaini ya ziada baada ya talaka na kuoa tena, kwa maana ya kwamba hilo
si suluhisho la maisha ya mwanadamu
Kabla ya kufanya uamuzi wa haraka wa kuvunja ndoa yako, fikiria. Mara nyingi
talaka haimalizi mahangaiko ya maisha. Badala yake, inatatua tatizo moja, na
kutokeza lingine. Katika kitabu chake, The Good Enough Teen, Dakt. Brad Sachs
anaonya hivi: “Wenzi wa ndoa wanaotalikiana huwazia kwamba kufanya hivyo
kutafaa kabisa, yaani, talaka yao itawaondolea kabisa huzuni na ugomvi mkali, na
badala yake wapate utulivu mwanana. Lakini kutarajia hilo ni sawa tu na kutarajia
kuwa na ndoa kamilifu, haiwezekani.” Hivyo, ni muhimu kuwa na habari kamili na
kuona talaka kihalisi.
Talaka huweka majeraha yasiyokoma mpaka kaburini
Nini madhara ya talaka kwa maisha ya wanandoa?
Huharibu afya ya kiroho
Huharibu afya ya kimwili
Kuchanganyikiwa miongoni mwa wanandoa
Watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili
Matatizo ya kifedha. Daniella, anayeishi Italia, alikuwa katika ndoa kwa miaka
12 alipogundua kwamba mume wake alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na
mfanyakazi mwenzake. Daniella anasema hivi: “Nilipogundua jambo hilo,
mwanamke huyo alikuwa na mimba ya miezi sita.”
Kuna matatizo ya kifedha.hebu ona mfamo huu baada ya kutengana kwa muda,
Daniella aliamua kumtaliki mume wake. “Nilijaribu kuiokoa ndoa yangu,” anasema,
“lakini mume wangu hakuacha kuwa na uhusiano nje ya ndoa.” Daniella anahisi
kwamba alifanya uamuzi unaofaa. Lakini anasema hivi: “Mara tu tulipotengana, hali
yangu ya kiuchumi ikawa mbaya. Nyakati nyingine nilikosa hata mlo wa jioni.
Nilikunywa tu maziwa.”9
Swali:1 je kama miongoni mwa washirika wako amepatikana na ugonjwa wa UKIMWI ilhali mwenzi
wake hana, utaamuaje suala la kuzuia talaka isitolewe?
swali 2. Hebu tuchukulie kwamba umemkamata mume/mke wako ana kwa ana (ready handed) akiwa
katika kifua cha kahaba utavumilia kuishi naye au utampa talaka?
Swali 3.wewe kama mwanadamu umewahi kufumaniwa? Ulimalizaje mgogoro huo nyumbani kwako?
D. MATUMIZI YA VILEO
Matumizi ya vileo ni jambo la kawaida kwa watu wengi, wakristo na wasio wakristo. Ni jambo
ambalo ni la muda mrefu hata kabla ya histori ya binadamu kuanza kurekodiwa katika
maandishi.
9 http://www.jw.org/sw/machapisho/magazeti/g201002/mambo-manne-kuhusu-talaka/
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
17
Kinaachofanya unywaji wa pombe/divai uwe ni wa kawaida ni kwa namna ambavyo
inatengenezwa. Pombe/divai nyingi inatengenezwa kutokana na nafaka, kwa mfano mtama
huweza kutengeneza aina mbalimbali ya vileo. Kwa mfano kwa wasukuma mtama huweza
kutengeneza pombe iitwayo ‘gongo’ au ‘mapuya’ au ‘mataputapu’ nk. Pia nafaka za mahindi
hutengeneza pombe. Lakini zamani za siku hizi nimesikia kwamba watu hutengeneza hata
pombe kwa kutumia kinyesi cha wanyama na wanadamu. Hii ni katika kuhakikisha kwamba
wanaongeza ukali katika vileo hivyo.
Maendeleo ya viwanda yamehamasisha unywaji wa pombe za kawaida na pombe kali kwa
kutengeneza vileo hivyo kwa njia ya kisasa kabisa. Hapa Tanzania, kampuni ya bia inatengeneza
aina mbalimbali ya bia kwa mfano Safari lagar, Serengeti larga, tusker lagar. Bia hizi zote utafiti
unaonyesha kwamba sio kali sana. lakini nimewahi shuhudia mtu amekunywa bia mbili aina ya
‘Ze bingwa’ na kuishiwa nguvu kabisa. Kuna vinywaji vingine vinatoka nje ya nchi kama vile
whisky ambayo ina 50% ya kileo. Daniel Jakes nk. Hata konyaji ni kileo kikali sana .
Kileo katika maandiko matakatifu
Kileo kinaonekana kutajwa katika maandiko kwa namna mbalimbali na kuonyesha umuhimu
wake kwa watumiaji.
Divai inatajwa kama dawa ya tumbo kwa anayesumbuliwa na tumbo na kwa ushauri wa
daktari anaweza kutumia. I Tim 5:23
Yesu alitengeneza divai kwenye arusi ya kana ya Galilaya na watu wakanywa na kulewa.
Yoh 2:1-11
Divai inatumika kuponya vidonda/majeraha ya vidonda. Lk 10:31
Divai inasaidia kupoteza mawazo ya umasikini. Mith 31:7
Divai hufurahisha moyo wa mwanadamu. Zaburi 104:15
Divai ilitumika katika sadaka kwa Bwana. Hes. 15:5-7
Japokuwa divai/pombe imeongelewa kwa mlengo chanya katika mafungu haya lakini pia
tukumbuke kwamba kwa upande mwingine imeongelewa kwa mlengo hasi. Yaani kwamba
ina madhara kwa maisha ya wanadamu. Mfano mafungu haya yanaonyesha hivyo, Kumb
21:20 IKor 6:7-9 nk
Mkristo na kunywa pombe.
Swali hili limekuwa ni swali la siku nyingi na kila siku wakristo wengi wanapingana katika
hili. Kwa baadhi ya madhehebu ya Kikristo yanaruhusu kunywa pombe ila usilewe tu. Lakini
kwa upande mwingine wengine wanasema kwamba kunywa pombe ni dhambi kubwa mbele
za Bwana. Hku wengine wakidai kwamba kunywa pombe ni tabia mbaya tu ila siyo dhambi.
Hebu tujaribu kuangalia hoja za kila upande unavyodai.
a) Misingi ya mkristo kunywa pombe
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
18
Biblia haikatazi unywaji wa pombe bali inakataza ulevi wa pombe. Ndiyo maana katika I
Tim 3:3 ‘si mtu wa kuzoelea ulevi’ kuzoelea ni kitenzi cha ‘kuzoea’ maana yake kuendekeza
tabia ya kufanya hivyo. Na hapa Paul anatoa sifa za kiongozi wa kiroho. Kumbe wakiristo
wengine wasio viongozi wanaweza kunywa pombe.
Biblia imeagiza mkristo aweze kujitawala sio kuacha kunywa pombe, hivyo basi kama
mkristo anaweza kunywa bia moja na akalala bila kumbughudhi mtu basi anaweza
kunywa ili mradi tu atawale hali yake.
Biblia inatambua kwamba pombe inaweza kutumika kama dawa, basi si mbaya
kunywa pombe kwa ajili ya afya10
.
Si kila mtu anayekunywa pombe anakuwa mlevi. Na biblia imekataza ulevi sio
unywaji wa pombe.
Kukataa kunywa pombe unaweza kujitenga na jamii. Kwa mfano kuna jamii zingine
kama ukienda kwenye sherehe lazima uzimue kidogo ndipo uonekane unashirikiana
nao.
Unapokunywa pombe unatuliza akili yako na hivyo kukufanya siku nyingine ukitaka
kufanya kazi ufanye kwa bidii kubwa
Suala la kunywa pombe halihusiani na masuala ya uzima wa milele. Kwa kuwa mtu
amempokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake basi amehesabiwa haki
na ana uzima wa milele. Hivyo si dhambi kunywa pombe.
b) Misingi ya mkristo kutokunywa pombe
Biblia inaonya juu ya matokeo ya matumizi ya pombe
Mtu aliyeweka nadhiri haruhusiwi kunywa kileo. hES 6:2-3
Makuhani hawakuruhusiwa kunywa vileo. LAW 10:9
Wafalme hawakupaswa kunywa vileo katika falme zao. MIT 31:4
Kileo hupotosha watumishi wa Mungu wanaojaribu kunywa. ISA 28:7
Si vizuri mtu aliyekusudiwa kuwa mkuu kutumia kileo. LK 1:15
Kunywa pombe kwa mkristo ni kuonyesha na kuendelea kuishi maisha ya zamani. 1PET
4:3-4
Pombe huleta magomvi katika nyumba za watu
Ulevi huua idadi kubwa ya watu. Nadhani hata wewe umeshuhudia watu ambao wamekufa
kwa sababu ya pombe
Pombe huvunja ndoa nyingi sana
Hakuna anayeanza kunywa pombe na kusema kwamba hatakuwa mlevi bali hustukia mlevi
tu
10 Mtu mmoja anaitwa nabii Tito (Nabii wa pombe- a prophet of beer) ni nabii anayehubiri watu kunywa pombe akitumia
maandiko matakatifu ya Biblia na kudai kuwa Biblia inaruhusu kunywa pombe.Hufanya mahubiri yake maeneo ya posta mpya
hapa jijini Dar es Salaam.
Nabii Titto yeye anadai kuwa ameoteshwa na mungu kuwa watu wanywe pombe kwani ni tiba sahihi tosha kwa magonjwa
mbalimbali na si pombe tu mpaka sigara. Dini yake aliyoianzisha inarushu watu kuoa wake wengi,kuvuta sigara na kunywa
pombe.Huyu ndiye nabii Tito (a prophet of beer)
Maadili ya Kikristo/ mch. Daniel John Seni/ Calvin Theological College DSM-Tanzania
19
Matokeo ya ulevi ni mabaya mno. Mfano kwa habari ya Lutu kulala na watoto wke wakati
wa ulevi na Nuhu wakati wa ulevi alilaani mjukuu wake Kanaani.
Kila mlevi unayemwona alianza kama mnywaji halafu polepole akawa mlevi mkubwa.
Tanbihi: ushauri kuhusu pombe
kwa kuwa hoja zinazopinga kunywa pombe ni nyingi sana, kwa ushauri wangu
usijaribu kunywa pombe hata siku moja. Usijaribu hata kutaka kujua ladha yake
ikoje. Achana na misemo ya wataalam soda ni hatari kuliko bia kwa afya!! Eti uache
kunywa soda ugeukie kunywa bia ni hatari sana.
------------------------------------------Mwisho--------------------------------------------------
Mch: Daniel John Seni
S.L.P 32807/[email protected]/ 0786684062 na 0769080629
Dar es salaam
Ni mchungaji wa kanisa la Shekinah Presbyterian Church Tanzania
Ni mwandishi wa kitabu cha ‘uwezekano wa mkristo kupagawa na pepo’moja ya
vitabu muhimu sana kwako na hupaswi kukikosa